ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 18, 2014

STAND UNITED TAYARI IPO BUKOBA KUUMANA NA KAGERA KAITABA LEO

PICHA na Faustine Ruta: Bukoba
JUMLA ya wachezaji wa Timu ya Stand United wametua Mjini Bukoba siku ya tatu leo kwa ajili ya Kipute cha Ligi kuu Vodacom msimu wa 2014-15 na Wenyeji wao Kagera Sugar jana asubuhi walifanya yao kwa mara ya kwanza wakiwa mkoani Kagera kwenye Uwanja wa Kaitaba. 

Wachezaji hao 26 wakiongozwa na Kocha Mkuu Emmanuel Massawe pamoja na Viongozi wengine 6 wanaounda kikosi cha timu mpya iliyoionja ligi kuu ya Tanzania bara kwa mara ya kwanza baada ya kuwa miongoni mwa timu tatu zilizopanda ligi kwa msimu wa 2013-2014, wameahidi kuonyesha soka safi kwa mashabiki huku wakiahidi kuendelea kuonyesha maajabu kwa kung'oka na ushindi katika madimba ya ugenini.

Timu ya Kagera Sugar ambao ndio wenyeji wa mchezo huo wanashika nafasi ya nane nyuma ya Stand United walio nafasi ya saba wakizidiwa magoli ya kufunga wao wameamua kujichimbia nje kabisa ya mji wa Bukoba.
BOFYA PLAY SIKILIZA TAARIFA ILIYORUKA LIVE JANA SPORTS XTRA CLOUDS FM.


Stand United.
Wachezaji wa Stand United wakifanya mazoezi 
Kocha Mkuu wa timu ya Stand United Emmanuel Massawe (kushoto) akiwacheki Vijana wake Wakijifua kwenye Uwanja wa Kaitaba 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.