ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 6, 2014

SHINDANO LA UONJAJI BIA KWA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MWANZA LAFANA: AIDAN MUHANDO WA MWANANCHI AIBUKA MSHINDI 2014.

Umakini katika kutambua rangi akiuhusisha huyu ni mshindi wa kwanza wa shindano la Beer Tasting Competition kwa wanahabari (Muonjaji Bora wa Bia) Aidan Mhando wa Mwananchi Communications akizibainisha bia katika ungwe ya pili ya na ya mwisho ya shindano hilo.
Awali kabla ya shindano la uonjaji bia,  Mpishi mkuu wa Kampuni ya Bia TBL tawi la Mwanza Oscar Kilasi alitoa somo kwa waandishi hao juu ya kuzibaini tofauti za bia kupitia ladha, rangi, harufu na viwango vya alcohol.
Kupitia Big screen hivi ndivyo somo la uonjaji bia lilivyokuwa likiendeshwa ndani ya ukumbi wa mikutano TBL Mwanza.
Kupitia Big screen hivi ndivyo somo la uonjaji bia lilivyokuwa likiendeshwa ambapo hapa bia aina ya Castle Light ilikuwa ikitolewa maelezo ya vihusishi vilivyohusika hadi ukamilifu wake na maelezo ya viwango vyake.
Kupitia Big screen hivi ndivyo somo la uonjaji bia lilivyokuwa likiendeshwa ambapo hapa bia ya Safari Lager ilikuwa ikitolewa maelezo ya vihusishi vilivyohusika hadi ukamilifu wake na maelezo ya viwango vyake.
Bia mbalimbali zinazo tengenezwa na TBL Tawi la Mwanza.
Philbert Kabago (mbele) akiongoza Waandishi wenzake wa habari kutembelea vitengo mbalimbali vya uzalishaji bia kupitia kiwanda cha kutengeneza bia TBL kilichopo wilayani Ilemela mkoani Mwanza.
Waandishi wa habari wakipata maelezo ya namna ya upikaji bia kupitia kiongozi wa kitengo cha maabara kiwanda cha kutengeneza bia TBL kilichopo wilayani Ilemela mkoani Mwanza.
"Hii ndiyo maabara ya TBL Mwanza"
Mtaalamu wa Ubora wa Bia kiwanda cha TBL Mwanza, David Keregeseni akitoa maelezo kwa waandishi wa habari William Bundara wa RFA (katikati) na Wilson Elisha wa Star Tv (kulia) ndani ya maabara ya kiwanda hicho kilichopo wilayani Ilemela mkoani Mwanza. 
Shughuli za uzalishaji zikiendelea ndani ya kiwanda cha kisasa cha kuzalisha bia TBL Mwanza.
Blogger Gsengo ndani ya mjengo wa uzalishaji bia Kampuni ya TBL Mwanza.
Blogger William Bundala aka Kijukuu cha Bibi ndani ya mjengo wa uzalishaji bia Kampuni ya TBL Mwanza.
Uzalishaji ukiendelea ndani ya mjengo.
Chupa zikiwa kwenye mstari kuelekea njia ya usafishaji ndani ya mjengo wa uzalishaji bia Kampuni ya TBL Mwanza.
Wakiwa shughulini hawa ni wataalamu kitengo cha uwekaji lebo za bia ndani ya mjengo wa uzalishaji bia Kampuni ya TBL Mwanza.
Philbert Kabago wa Passion Fm kikazi zaidi katika shindano la Muonjaji Bora wa Bia kiwandani TBL Mwanza.
Mashaka Bartazar anayeandikia magazeti ya Majira na Jambo leo akifanya yake.
Harufu na uonjari ni sehemu ya kubaini aina ya bia.
Biskuti maalum ni nyenzo kwaajili ya kufuta ladha ya bia uloionja awali kabla ya kuionja bia nyigine.
We Katulanda, unaonjaaaa au unakunywa? Tehe...teee!!
 Beer Tasting Competition.
Meneja Mawasiliano na Habari wa TBL Edith Mushi (kulia) akikusanya karatasi za mtihani wa shindano la Uonjaji bia kwa waandishi wa habari.
Meneja msaidizi katika uzalishaji kampuni ya bia TBL Mwanza, Jemedari Waziri akimkabidhi zawadi mshindi wa kwanza wa shindano la Beer Tasting Competition kwa wanahabari (Muonjaji Bora wa Bia) ambapo Aidan Mhando wa Mwananchi Communications ndiye aliyeitwaa nafasi hiyo kwa mwaka huu 2014-2015.
Carolyne Mhonoli ambaye ni Meneja ubora wa bia wa TBL Mwanza, akikabidhi zawadi kwa mshindi wa pili wa shindano la Beer Tasting Competition (Muonjaji Bora wa Bia) Fredrick Katulanda ambaye ni Mhariri wa magazeti ya New habari Kanda ya Ziwa, katika hafla fupi iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika kiwanda hicho kilichopo Ilemela mkoani Mwanza.
Afisa Habari na Matukio TBL Mwanza, Mr. Erick  akimkabidhi zawadi mshindi wa tatu wa shindano la Beer Tasting Competition (Muonjaji Bora wa Bia) Philbert Kabago wa Passion Fm Mwanza, katika hafla fupi iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika kiwanda hicho kilichopo Ilemela mkoani Mwanza.
Kila mmoja alitoka na zawadi yake.
Mzigo umeuonaaaa!!? 
Bia tayari kwa kuingia sokoni. 
Tukipata U-PichaZ. 
Wanyama.
Picha ya pamoja ya waandishi wa habari na wadau wa TBL mara baada ya kumaliza matembezi katika kiwanda cha Tanzania Breweries Limited Mwanza.
MPANGO MZIMA KWA UFUPI.
MWEZI wa Sita wa kila mwaka kampuni ta Tanzania Breweries Limited (TBL) inaandaa mashindano kwa waandishi wa habari kwa ajili ya kubaini vinywaji vya kampuni hiyo kwa kuonja ladha tofauti kisha kutambua ni bia gani. 

Jijini Mwanza mashindano hayo yamefanyika jana katika kiwanda cha TBL na kushirikisha wawakilishi wa vyombo vya habari  zaidi ya Ishirini kutoka vyombo mbalimbali vya habari jijini mwanza. 


Katika mashindano hayo yaliyodumu takribani dakika thelathini yalimalizika kwa waandishi watatu kulingana point hali iliyopelekea mchuoano kurudiwa kwa watu watatu ili kumpata mshindi. 


Katika marudio hayo mwandishi na Mtangazaji wa kituo cha Passion Fm Filbert Kabago aliibuka mshindi wa tatu hali iliyopelekea kutafuta mshindi wa kwanza na pili kati ya mwandishi wa gazeti la mwananchi Aidan Muhando na Mwandishi wa Gazeti la Mtanzania Fedrick Katulanda. 


Baada ya kupambana Aidan Mhando aliibuka mshindi wa kwanza na Fedrick Katulanda akakamata nafasi ya pili. Baada ya mashindano hayo waandishi walipata nafasi ya kutembelea eneo la maabara na eneo la uzalishaji ili kujionea namna bia za kampuni ya TBL zinavyozalishwa na kupata nafasi ya kuuliza Maswali ili kutumia kalamu zao kutoa elimu kwa jamii. 


Licha ya kubainisha kuwa ziara hiyo imesaidia kutambua masuala ya biashara takayo saidia kufikisha ujumbe kuhusu bidhaa zinazo zalishwa na kampuni hiyo, mmoja wa waandishi wa Clouds Fm jijini Mwanza ambaye pia ni mmiliki wa G.Sengo Blog, Albert Sengo amesema ziara hiyo ya wazi kwa waandishi wa habari ambao ni wadau wa kuibua taarifa na changamoto zilizopo ndani ya jamii, ni ushahidi tosha kwamba kiwanda hicho cha kutengeneza bia kinajiamini katika masuala yote ya teknolojia, afya, usafi na uzalishaji makini, kwani kungekuwa na magumashi (ubabaishaji) basi TBL wasinge thubutu kuwapa uhuru wadau hao kujiachia katika kuuliza maswali na kunasa matukio mbalimbali kiwandani humo.....

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.