ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 19, 2014

KIFO CHA MWANAMUZIKI WA FM ACADEMIA KINE DIGITAL CHAWAUMIZA WENGI.

"Umeondoka ukiwa mdogo sana..mpole..mkimya..sauti nzuri..smart..bye Kine Digital..leo nimededicate kipindi kizima cha Tanzania Stars kwako brother...poleni sana Ngwasuma na wapenzi wote wa dansi....one love Dogital..sikiliza wimbo chuki ya nini uisikie sauti yake tamu..aaaghhh" Ameandika Mtangazaji wa Star Tv Bernard James katika ukurasa wake wa facebook.

Mwanamuziki mwenye sauti kali na yenye hisia wa bendi ya FM Academia 'Wazee WaNgwasuma' aitwae Digital amefariki dunia jana ikiwa ni kipindi mfupi tangu alipokuwa amelazwa katika hospital ya Muhimbili jijini Dar, awali tangu wiki iliyopita alikimbizwa hospitali ya Mwananyamala baada ya kuzidiwa na maradhi, na chanzo cha kifo chake hakijaelezwa! poleni FM Academia, ndugu na jamaa katika kipindi hiki kigumu.

Hebu fuatilia video ifuatayo ya wimbo Chuki ya nini ambapo marehemu anaonekana vyema katika dakika ya 6:35
Kwa habari zaidi nitaendelea kuwajuza zaidi, Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu Digital, Ameni!!

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.