ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 14, 2014

MAENDELEO YA KWIMBA YATALETWA NA WANAKWIMBA WENYEWE: ASEMA HAMISI MZEE.

Mkuu wa wilaya ya kwimba ambaye vilevile ni mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani humo Hamisi Mzee akiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa idara, viongozi wa dini toka madhehebu mbalimbali na baadhi ya wakulima mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kwanza cha mwaka huu kujadili maendeleo ya wilaya, chakula, ulinzi na  usalama.
PICHA NA ZEPHANIA MANDIA 
Katika kikao hicho Mkuu wa wilaya ya Kwimba Bw. Hamisi Mzee amesisitiza kuimarisha ulinzi shirikishi ndani ya jamii, akiwaasa viongozi wa dini kuweka msisitizo katika ibada zao na kukazia elimu ya kuepuka masuala ya imani potofu inayo chochea mauaji na ukatili kwenye jamii pamoja na kuasa vijana kuepukana na madawa ya kulevya.

Ili kuwa na jamii yenye afya, amani na maendeleo  amewasisitiza wananchi wa wilaya ya hiyo kuzingatia kanuni bora za kilimo kinachozingatia hali ya hewa na jiografia ya maeneo kwa wakulima hao kulima mazao yanayo stahimili ukame kama mtama kwa chakula, alizeti na pamba kama zao la biashara.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.