ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 24, 2014

NDIKILO KUONGOZA HARAMBEE YA UBORESHAJI WA HUDUMA ZA JAMII KATA YA NYAMSWA WILAYA YA BUNDA MKOA WA MARA ITAKAYO FANYIKA MWANZA JIONI YA LEO.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Eng. Evarist ndikilo.
MKUU wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo hii leo anatarajiwa kuongoza harambee ya kuchangiaha fedha kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za jamii kwa kata ya Nyamswa wilaya ya Bunda mkoa wa Mara itakayofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania - B.O.T tawi la Mwanza uliopo Capri Point wilayani Nyamagana.

Akizungumza na GSENGO blog Mwenyekiti wa Kamati Inayoandaa Harambee hiyo ya kuchagiza Maendeleo kata ya Nyamswa Bw. Juma Makongoro amesema kuwa nia ya kufanya tukio hilo ni kwaajili ya kuboresha huduma za kijamii kupitia changamoto zinazowakabili watu wa kata hiyo baada ya kuzibaini kuwa ni sugu zinazo rudisha nyuma maendeleo ya wakazi wa eneo hilo sambamba na kuzidi kuwadidimiza katika lindi la umasikini na kusababisha vifo vinavyoweza kuzuilika. BOFYA PLAY KUMSIKILIZA.

Washiriki mbalimbali wamealikwa katika hafla hiyo wakiwemo:-
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwemo Mhe. Wassira.
Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Baadhi ya Wanasiasa kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania.
Wananchi, Vijana wa Kikizu na Nyamswa waliokuja kutoka Dar, Arusha, Mwanza nk.
Wakereketwa wa Maendeleo bila kujali kabila wala itikadi.
Wafanyabiashara na Wafanyakazi (mbalimbali).

MATARAJIO NA FAIDA
Uboreshaji wa Ujenzi wa Miundo Mbinu ya utoaji huduma za kijamii katika Sekta ya Elimu, Afya na Maji.
Kuboresha hali maisha kwa jamii ya wakazi wa wilaya ya Bunda hususani kata ya Nyamswa.
MICHANGO YOTE IELEKEZWE KATIKA A/C 30110000521 NMB-BUNDA MFUKO WA WAZEE WA MAENDELEO KATA YA NYAMSWA, M PESA 0753 520448

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.