ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 22, 2014

HUU HAPA WIMBO MAHUSUSI KWA KOMBE LA DUNIA 2014


La La La (Brasil) wimbo wake mwanamama Shakira ndiyo utakuwa wimbo maalum kwaajili ya Kombe la dunia la FIFA 2014.

Hii si mara ya kwanza kwa Shakira kwani mnamo Tarehe 10 mwezi Juni 2010 njini Soweto, Shakira na Freshlyground walitumbuiza wimbo maalum katika tamasha la uzinduzi kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la dunia.

Nyimbo kadhaa zisizo rasmi tayari zimesikika sehemu mbalimbali ikiwa ni pamoja na ule ulioimbwa na John Barnes Kwa fainali za Kombe la dunia mwaka 1990, World in Motion by New Order.

Wimbo rasmi wa mwisho wa England katika Kombe la Dunia ulioitwa "World At Your Feet" wa kundi la Embrace ulikamata nafasi ya tatu katika chati za muziki mwaka 2006. Pia mwanamuziki Tony Christie na Crazy Frog walifanya jitihada kadhaa za kutoa nyimbo za kuhamasisha kampeni ya England.

Mwaka 2002, wimbo "We are on the ball" ulirekodiwa na watangazaji wa Tv, Ant na Dec.

Mwaka 1998, kundi la Spice Girls waliimba wimbo (How Does it feel To Be) on Top Of The World, ulioandikwa na Endo na ian McCulloch wa kundi la Bunnymen.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.