ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 27, 2014

SAFARI NYAMA CHOMA - ARUSHA NA MOSHI

Jaji kiongozi, Laurent Salvi akitoa maelezo ya mfano wa namna ya
kukagua nyama iliyoiva kwa washiriki wa warsha ya nyama choma,
iliyoandaliwa na waandaaji wa mashindano ya Safri Lager Nyama choma
Festival.(picha na mpiga picha wetu).
Jaji kiongozi akimkabidhi cheti cha ushiriki, mwakilishi wa Baa ya
Makanyaga, Freeman Rogarth, baada ya kumalizika kwa warsha hiyo.(picha na mpiga picha wetu).
Jaji kiongozi akimkabidhi mwakilishi wa Baa ya East Afrika, Beda
Paschal cheti cha ushiriki katika hafla ya kufunga mafunzo ya namna ya
kuchoma nyama.(picha na mpiga picha wetu).
Na Mwandishi Wetu. 
Moshi na Arusha.
KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Safari Lager jana imetoa mafunzo kwa wachomanyama kutoka Baa mbalimbali za Mkoa wa Moshi na Arusha ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya Safari Nyama Choma kwa mwaka 2014 yatakayo fanyika katika viwanja vya General Tyremachi 15 na viwanja vya CCM mkoa kwa Mkoa wa Kilimanjaro machi 16 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja masoko wa TBL, Leia Hermenegild alisema lengo la kutoa mafunzo ni kutoa elimu kwa wachoma nyama ukizingati auchomaji nyama ni moja sehemu ya kujiingizia kipato katika Bar.

Leiya alisema kutokana na hali hiyo wakaona ni vema wakaendesha Semina kwa wachoma nyama ili waweze kukidhi vigezo vya mahitaji ya Wateja ili waweze kufurahia Nyama choma kama ilivyo kwa vyakula vingine ili kuendana na kauli Mbiu ya Bia ya Safari Lager isemayo“ Safari Lager bila nyama choma haijakamilika.”

Aliongeza kuwa baada ya mafunzo hayo yaliyo tolewa kwa wachoma nyama wa Baa ambao walitunukiwa vyeti vya ushiriki  pia kutakuwa na mashindano ya kuchoma nyama ambapo washindi 10 watapatikana kutokana na watakaofuzu vigezo namasharti waliyopewa katika semina hiyo.

Alisema Fainali za Mashindano zitafanyika Machi15 kwa mkoa wa Arusha na machi 16 kwa mkoa wa kilimanjaro, Mwaka huu ambapo washindi watapewa zawadi kuanzia mshindi wa kwanza atakaye jinyakulia Shilingi Milioni moja na Kikombe, mshindi wa pili Lakinane, Mshindi wa tatu Laki 6, 

Mshindi wa nne laki nne na Mshindi wa Tano shilingi laki mbili huku mshindi wa Sita hadi wa Kumi watajinyakulia kifuta jasho cha shilingi 50,000/= kwa kila mkoa.

Alisema namna ya kuwapata washindi ni kutokana na wateja kupiga kura katika utaratibu utakaobandikwa katika Baa shiriki ambapo mteja atapiga kura kupitia simu ya mkononi ili kuichagua baa inayo choma nyama vizuri.

Kwaupande wake Mkufunzi wa Mafunzo hayo, Laurence Salvia mbaye pia ni Jaji Mkuu wa mashindano hayo amesema huwezi kuandaa mashindano bila ya kutoa Elimu, hivyo TBL wamefikiria jambo la msingi sana lenye manufaa kwa waandaaji yaani wachoma nyama mpaka kwa watumiani yaani mlaji.

Bwana Lawrence binfsi aliishukuru TBL kupitia bia ya Safari Lager kufikiria jambo zuri la kufadhili elimu kwa wachoma nyama jambo ambalo sifaida kwa wachomanyama tubali hata watumiaji sasa watakula nyama inayostahili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.