ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 4, 2014

MWANZA YATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MCHUNGAJI DAUDI ISAYA ONYANGO ALIYEFARIKI KWA AJALI.

Wachungaji wa makanisa mbalimbali ya AICT Kanda ya Ziwa wakiwa katika ibada maalum ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mchungaji Daudi Isaya Onyango aliyefariki kwa ajali akiwa safarini mkoani Geita ambako alikwenda kwaajili ya kazi ya kusambaza vitabu vya neno la Mungu.
Mwili wa Mchungaji Daudi Isaya Onyango ukiingia katika kanisa la AICT Makongoro kwaajili ya ibada ya kuagwa na wakazi wa Mwanza kisha kusafirishwa kuelekea mkoani Mara kwaajili ya mazishi.
Mchungaji Daudi Isaya Onyango alizaliwa mnamo mwaka 1963 tarehe 3 mwezi march.
Mama Rose ambaye ni mjane wa marehemu (wa pili kutoka kushoto) akiwa na wanae kwenye ibada hiyo.
Waumini walio hudhuria ibada hiyo iliyofanyika leo asubuhi katika kanisa la AICT Makongoro Mwanza.
Wananchi na watu wa mataifa mbalimbali wako hapa.
Upande wa akinamama.
Ibada ikiendelea.
Historia ya marehemu Mchungaji Isaya Onyango ikisomwa.
Wachungaji wa makanisa mbalimbali, waumini na marafiki waliomjua wameshiriki ibada hii.
Askofu Mussa Magwesela wa Dayosisi ya Geita aliongoza ibada hiyo kwa kumfananisha marehemu Mchungaji Onyango na mwanariadha aliyesubiri kuvikwa taji la uzima mara baada ya kumaliza mbio.
Jiografia ya kanisa wakati wa ibada.
Sifa kuu ya kila mchungaji aliyepata nafasi kumzungumzia Mchungaji Daudi Isaya Onyango alimzungumzia kama rafiki. 
Mwakilishi wa Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Alliance Mission alimzungumzia Mchungaji Daudi Isaya Onyango kama mfano wa kuigwa kwa kupenda watoto na kuwasaidia kutatua matatizo yao kwa ukaribu akiwaonyesha upendo wa kweli.
Kwaya ya Vijana AIC Makongoro ikiimba wimbo maalum.
Ni wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Mchungaji Daudi Isaya Onyango.
Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza Jackson Songora akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mchungaji Daudi Isaya Onyango katika ibada iliyofanyika Kanisa la AICT Makongoro Mwanza. 
Kwaya ya Makongoro akinamama.
Familia ya Marehemu Mchungaji Onyango ilipata nafasi kutoa heshima za mwisho na hapa wanaonekana vijana wa marehemu  wakiwa na mjomba wao Allen Olimo (mwenye koti kulia).
Mjane wa marehemu akipata usaidizi kuuaga mwili wa marehemu mumewe.
Hali ilikuwa mbaya kwa mabinti wa marehemu.
Maaskofu na wachungaji wakiuaga mwili wa marehemu mchungaji  Daudi Isayo Onyango.
Askofu Mussa Magwesela wa Dayosisi ya Geita akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu mchungaji Daudi Isaya Onyango katika ibada takatifu iliyofanyika katika kanisa la AICT Makongoro Mwanza.
Mbele ni Mchungaji toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambaye alilelewa na kanisa la AIC Tanzania akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Mchungaji Daudi Isaya Onyango ambaye alimtaja marehemu kuwa alikuwa ni rafiki yake kipenzi katika ushauri. 
Ibada ya kuhitimisha ibada ilifanyika kanisani hapa kisha safari kuelekea kijiji cha Songoro kata ya Buruma, wilaya ya Butiama mkoani Mara kwa mazishi ilifanyika. 
Safari kuelekea kijiji cha Songoro kata ya Buruma, wilaya ya Butiama mkoani Mara kwa mazishi ilifanyika.
Meya wa jiji la Mwanza ambaye pia ni diwani wa kata ya mkolani Mhe. Stansalaus Mabula (mwenye miwani kulia) akikumbushana mambo muhimu na marafiki zake mara baada ya ibada hiyo iliyofanyika katika kanisa la AICT Makongoro kumalizika.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.