ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 2, 2013

MAANDALIZI YA TAMASHA LA KING OF BOLD CHUO CHA SAUT LITAKALO PIGWA JIONI HII





SERENGETI BREWERIES LIMITED KUPITIA BIA YA PILSNER LAGER WAKISHIRIKIANA NA UONGOZI WA CHUO CHA SAUT WANAKULETEA BORN FIRE DAY
TAMASHA HILI NI MAHUSUSI KATIKA KUWAKARIBISHA WANACHUO MWAKA WA KWANZA.
KWENYE STAGE SASA:- KUTAKUWA NA MASHINDANO YA KUFREE STYLE KWA WANAUME NA AKINA DADA ZETU WAKIONYESHA UMAHIRI WA KUKATA NYONGA KWA MIONDOKO YA TAARABU AMBAPO ZAWADI MBALIMBALI NZITONZITO ZITATOLEWA.

PIA KUTAKUWA NA DROO KUBWA KUMTAFUTA MSHINDI WA LAPTOP NA ZAWADI NYINGINEZO KWA WALE WALIOJIUNGA NA PILSNER LAGER MEMBERSHIP.

USIKU MNENE SASA: SUPRIZES ZA MA-DJ
ON THE STAGE ROMA, KASIMU MGANGA, JAMBO SQUARD WATAKISANUKISHA MPAKA BASssss....!!
HAKUNA KIINGILIO.

NI CHINI YA UDHAMINI MKUBWA WA SERENGETI BREWERIES LIMITED KUPITIA BIA YA  PILSNER LAGER
PILSNER LAGER KING OF BOLD.

Kumbuka kunywa Pombe kupita Kiasi ni hatari kwa Afya yako, Haiuzwi kwa wenye umri chini ya miaka 18, tafadhali kunywa kiistarabu.

KHADIJA KOPA NA ISHA MASHAUZI WALIVYO ITIFUA VILLA PARK

Isha Mashauzi akikisanukisha ndani ya Villa Park Mwanza katika usiku wa Taarabu Nani zaidi kati yake na Khadija Kopa.
Khadija Kopa akiimba na mashabiki wake katika usiku wa Taarab Nani zaidi kati yake na Isha Mashauzi.
Mzuka wa taarab...
Watu weeeeee......!!!
Hapa ilikuwa hatariii...Isha na Shabiki ake.
Mambo ya midundo...!
Khadija ni kwa hisia zaidi...
Shabiki wakituoka kumtunza ngawira...
'Ni Mpambano usio rasmi'

Khadija Omary Kopa akimzawadia  chupa ya kinywaji cha Zanzi mmoja kati ya mashabiki waliotinga Villa Park usiku wa Taarabu Nani zaidi. Wa kwanza Kulia ni Meneja wa Villa Park Mwanza 'Manager Ramma' 
Khadija Omary Kopa akimzawadia  chupa ya kinywaji cha Zanzi mmoja kati ya mashabiki waliotinga Villa Park usiku wa Taarabu, kushoto katika picha anaonekama Mc Mama Steve.
Isha Mashauzi akimzawadia  chupa ya kinywaji cha Zanzi mmoja kati ya mashabiki waliotinga Villa Park usiku wa Taarabu Nani zaidi. Zanzi ni Sehemu ya Wadhamini wakuu wa burudani hii.
Isha Mashauzi akimzawadia  chupa ya kinywaji cha Zanzi mmoja kati ya mashabiki waliotinga Villa Park usiku wa Taarabu Nani zaidi. Zanzi ni Sehemu ya Wadhamini wakuu wa burudani hii.
Mc Magoma akimwaga sera zake kwa wadau waliohudhuria Usiku wa Taarabu Villa Park Mwanza.
Ze colour ya nyomi iliyotinga hapa.
'Rusha roho usitupe .......'
Bob White mkali wa pamba za mabinti dunia nzima (L)  na prizenta wa Passion Fm Philbert Kabago, wakishow love kwa kamera ya G. Sengo Blog.
Mashauzi (L) na Mc Mama Steve (R)
Khadija Omar Kopa (L) na Blooger & Prizenta wa RFA Kijukuu  cha bibi....Haha-ha..
Kulia na kushoto ni Maticha wa masuala ya cat-wox na mitindo Mwanza wakiwa na mdau wao pale kati

"Niruke nisiruke....?"

DODOMA NA MAPOKEZI YA TIMU YA TAIFA SAFARI POOL

Wachezaji wa Pool,wapenzi na mashabiki wa mchezo wa Pool wa Mkoa wa Dodoma wakiwapokea wachezaji wa timu ya Taifa ya Safari Pool kwa mbwembwe za aina yake na matarumbeta mara baada ya kuwasili mkoani humo wakitokea Malawi kwenye mashindano ya Pool ya Afrika ambapo walipata ubingwa wa mchezaji mmoja mmoja(Singles) na nafasi ya tatu upande timu juzi.
Wachezaji wa Pool,wapenzi na mashabiki wa mchezo wa Pool wa Mkoa wa Dodoma wakiwapokea wachezaji wa timu ya Taifa ya Safari Pool kwa mbwembwe za aina yake na matarumbeta mara baada ya kuwasili mkoani humo wakitokea Malawi kwenye mashindano ya Pool ya Afrika ambapo walipata ubingwa wa mchezaji mmoja mmoja(Singles) na nafasi ya tatu upande timu juzi.
Wachezaji wa Pool,wapenzi na mashabiki wa mchezo wa Pool wa Mkoa wa Dodoma wakiwapokea wachezaji wa timu ya Taifa ya Safari Pool kwa mbwembwe za aina yake na matarumbeta mara baada ya kuwasili mkoani humo wakitokea Malawi kwenye mashindano ya Pool ya Afrika ambapo walipata ubingwa wa mchezaji mmoja mmoja(Singles) na nafasi ya tatu upande timu juzi. 
Mchezaji wa timu ya taifa ya Safari Pool, Patrick Nyangusi akisalimia wapenzi na mashabiki wa jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili kwenye Party ya kupongezwa iliyokuwa imeandaliwa katika Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar es Salaam jana.

Friday, November 1, 2013

HIVI NDIVYO SIMBA SC. WALIVYOGEUKA AL-SHABAAB UWANJA WA TAIFA JANA

Mmoja wa mashabiki wa Klabu ya Simba SC. akishushwa jukwaani na Askali wa Usalama baada ya kusababisha fujo iliyopelekea kung'oa viti zaidi ya 50 na kuwatupia askali hao ambao walikuwa wakiwatuliza ili wasiendelee kuleta fujo iliyotokana na penaliti waliyopewa wapinzani wao uwanjani hapo jana kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambapo walikuwa wakipambana na timu ya Kagera Suger na uliomalizika kwa sare ya 1-1.
Askali Polisi wakijaribu kutumia uwezo wao katika kuwatawanyisha baadhi ya mashabiki wa Klabu ya Simba SC.baada ya kuzua tafrani iliyotokea baada ya mwamuzi wa mchezo huo kuruhusu penati ipigwe na timu ya Kagera Suger,ikielekezwa langoni mwa Simba.
PICHA ZAIDI BOFYA http://mateja20.blogspot.com/

Thursday, October 31, 2013

USIKU WA TAARAB LEO VILLA PARK HAPATOSHI

Ndiyo hivyo tena muda huu majira ya saa moja jioni, Khedija Omary Kopa na Isha Mashauzi wametoka kufanya sound cheki' hapa villa park nao mashabiki nambari moja wa Mwanza hawakukosekana.
Another photo....kachaaa...Kuelekea mpambano wa Muziki wa Taarab wa Nani zaidi kati ya Isha Mashauzi na Khadija Omar Kopa ndani ya Villa Park Mwanza leo (Tarehe 31/10/2013)
Isha Mashauzi akiwa na shabiki ake Amina Mundele na shosti ake.
Kutoka kushoto ni Dj Chriss, Khadija Omary Kopa na Dj John ambao leo watasimamia mpango mzima kiingilio ni shilingi 10,000/=
'Kattchaaaaa'.....mlio wa kamera ulisikika..
Mwanamuziki nguli wa muziki wa dansi nchini Mzee Kitime akiwa na vijana wake Dj Chriss na Dj John.

MWENYEKITI NA KATIBU WA TACOGA WAKAMATWA BARIADI

Mwenyekiti wa TACOGA Elias Zizi.
 MWENYEKITI wa Chama cha Wakulima nchini (TACOGA) na Katibu wake  wamekamatwa na jeshi la Polisi Wilayani hapa baada ya kufanya Mkutano wa hadhara kuzungumzia umuhimu wa wakulima kutumia Mbegu za manyoya na kukataa kutumia zile zisizo na manyoya za UK 91(Quton) kutokana na bei yake kuwa shilingi 1,200 kwa kilo moja.

Askari polisi walifika na kumsomba mwenyekiti huyo na katibu wake.
Hatua hiyo ya kukamwatwa kwa mwenyekiti huyo wa TACOGA Elias Zizi inafuatia kauli ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Erasto Sima kutoa tamko la kuwakamata baadhi ya watu wakiwemo wanasiasa wanaofanya mikutano ya hadhara na kuwahamasisha wakulima kukataaa kutumia mbegu bora iliyopitishwa na Bodi ya Pamba  nchini.
Haooo wakatembea.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi Erasto Sima akijibu maswali ya wananchi.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi Baiskeli kwa wakulima wawezeshaji 35 kutoka vijiji 20 vya maeneo ya Wilaya ya Bariadi na Itilima Mkoani Simiyu zilizotolewa na Bodi ya Pamba nchini kupitia ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya (EU) ili kusaidia kutoa elimu na mafunzo ya kilimo bora cha zao la pamba katika maeneo mbalimbali.

Sima alisema kwamba kumekuwa na tabia ya kuwahamasisha wakulima kukataa kutumia mbegu bora ya Quton ambazo katika maazimio ya vikao mbalimbali vya wadau na Bodi ya pamba viliadhimia kutumika kwa mbegu hiyo katika msimu wa kilimo unaoanza mwezi Novemba mwaka huu ili kuboresha pamba na kuwa na tija kwa mkulima.

“Nimepewa taarifa kuwa Mwenyekiti amekamatwa na askari polisi akiwahutubia watu kwenye mkutano wa hadhara lakini imeonekana amekiuka kibali chake na kuanza kuwahamasisha wakulima na wananchi kuwapiga mawe maafisa wa Bodi ya pamba na wataalamu watakaopeleka mbegu za Quton kwenye vijiji ili kuziuza na kuzipanda” alisema

Mkuu huyo alisema kwamba taarifa za kukamatwa kwa Zizi hazihusiani moja kwa moja na kile alichokisema siku moja tu baada ya kukabidhi baiskeli zilizotolewa na Bodi ya Pamba katika Mradi wa kilimo cha Biashara sehemu ya Pili (TASP II) katika Wilaya za Meatu, Maswa na Bariadi katika Mkoa wa Simiyu kama ilivyoelezwa na Mratibu Renatus Luneja.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TACOGA Zizi alisema kitendo cha kukamatwa kwake kimemushanghaza sana na kudai kuwa juhudi za  kuendelea kuwapigania wakulima ataendelea nazo kwa kuwa yeye ndiye kiongozi wao aliyepo madarakani kikatiba kamwe hatarudi nyuma
Naye Katibu wa TACOGA , George Mpanduji amesema kwamba wakulima wanahaki ya kufahamu kupitia viongozi wao juu ya nini cha kufanya kabla ya msimu wa kilimo kuanza mwezi Novemba mwaka huu hivyo kufanyika kwa mikutano hiyo  imelenga kuwahamasisha wakulima kulima na kutumia mbegu bora na si kama inavyodhaniwa.


“Tuwaache wakulima kuchaguwa mbegu watakazotumia kwenye kilimo badala ya kuwalazimisha kutumia mbegu za Quton ambazo bie yake ni kubwa kutokana na baadhi yao kushindwa kumudu bei hiyo kutokana na kuwa na gharama kubwa kuliko uwezo” alisisitiza Mpanduji .

WAFANYAKAZI WA KONYAGI WALIOENA KUANGALIA LIVE MCHEZO WA BARCELONA VS REAL MADRID

Mfanyakazi wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Khadija Madawili ambaye alikuwa kiongozi wa msafara wa wafanyakazi wa TDL waliokwenda kushuhudia pambano la Ligi ya La Liga ya Hispania kati ya Barcelona na Rael Madrid, akirejea jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam. Wafanyakazi watano wa TDL, waliteuliwa baada ya kampuni hiyo kushinda  Tuzo ya SABMILLER AFRICA MB COMPLEMENTARY BEVERAGE CATEGORY AWARD FOR F 13)
Joseph Chibehe (kushoto) akilakiwa na mkewe baada ya kuwasili
Chibehe akiwa na furaha baada ya kulakiwa na mkewe
Bavon Ndumbati (kushoto), akilakiwa na ndugu yake. Katikati ni Michael Mrema.
  Bavon akiwa na furaha
Mwesiga Mchuruza.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Konyagi ya Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa (katikati), akiwa na mabosi wa kampuni mama ya SABMILLER AFRICA.wakiwa wameshikilia tuzo hiyo ya  MB COMPLEMENTARY BEVERAGE CATEGORY AWARD FOR (F 13).
KAMPUNI ya Tanzania Distilleries Ltd, (KONYAGI) ambayo ni miongoni mwa kampuni tanzu za Kampuni ya Sabmiller South Africa, imeshinda tuzo ya utendaji bora wa bidhaa (SABMILLER AFRICA MB COMPLEMENTARY BEVERAGE CATEGORY AWARD FOR F 13). Sabmiller inamiliki zaidi ya viwanda 60 vya bia na vinywaji vingine duniani.

Baada ya ushindi huo, Mkurugenzi Mkuu wa TDL, Mgwassa ambaye alipambana mpaka kupata ushindi huo, aliamua kuwazawadia baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo, kwenda Hispania kushuhudia pambano la timu kubwa za Barcelona na Real Madrid lililofanyika mwishoni mwa wiki.

Wafanyakazi waliokwenda Hispania  na kurejea jana usiku kwa ndege ya Afrika Kusini ni; Joseph Chibehe, Khadija Madawili, Bavon Ndumbati, Michael Mrema na Mwesiga Mchuruza.

Wafanyakazi hao, walipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, walionekana kuwa na bashaha na kupokelewa na ndugu zao pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzao.

Akizungumza kwa niaba ya wenzie,Michael Mrema wa Kanda ya Kaskazini, alisema kuwa wanashukuru uongozi kuwapa zawadi hiyo, ambayo imewafanya kuwa na morari mpya wa kazi.

Pia anaseama walifurahi sana kushuhudia mechi hiyo kubwa ya timu za Barcelona na Real Madrid ambapo timu ya Barcelona waliyokuwa wanaishabikia kushinda mabao 2-1.

Wednesday, October 30, 2013

RIHANNA AJITWIKA NYOKA KUTENGENEZA KAVA LA GAZETI LA BURUDANI UINGEREZA

Ikiwa ni kipindi cha msimu wa Halloween, the "Diamonds" mwimbaji maarufu nchini Marekani mwanadada Rihanna ametokelezea katika pozi moja matata la kushtusha pale alipoamua kujitwisha nyoka wadogo wadogo kichwani akiwasimika mithili ya kitambaa au kofia kufunika nywele na nyoka mwingine mkubwa akijitwika shingoni kutengeneza mwonekano matata wa cover la gazeti la Burudani la nchini Uingereza linalokwenda kwa jina la GQ.
Hili ni toleo maalum kwa mwezi December linalotoka kusherehekea miaka 25 ya jarida hilo. (hitting newsstands Dec. 31). The shoot was styled by reclusive U.K. artist Damien Hirst, whom some think may be the most wealthy living artist in the world.
Jarida la GQ lilianzishwa mnamo mwaka 1988.