ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 12, 2013

BONNAH TRUST FUND YAZINDULIWA RASMI LEO JIJINI DAR

Muasisi wa Mfuko wa Elimu ya Bonnah Trust Fund,Bi. Bonnah Kaluwa ambaye pia ni Diwani wa kata ya Kipawa,jijini Dar es Salaam akizungumza machache wakati wa hafla fupi ya Uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Kuhamasisha elimu ya Tanzania ili isonge mbele uitwao Bonnah Trust Fund,uliofanyika mapema leo asubuhi kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
Mgeni Rasmi katika Hafla hiyo ya Uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Kuhamasisha elimu ya Tanzania ili isonge mbele uitwao Bonnah Trust Fund,Meya wa Ilala,Mh. Jerry Silaa akisisitiza jambo muda mfupi kabla ya kuzindua Mfuko huo,mapema leo asubuhi kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Kutoka Kushoto ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Makongoro Mahanga,Meneja wa Huduma kwa Jamii kutoka kampuni ya Tigo,Bi Woinde Shisael,Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Mh. Mushi,Muasisi wa Mfuko wa Elimu ya Bonnah Trust Fund,Bi. Bonnah Kaluwa pamoja na Mgeni Rasmi kwenye hafla hiyo,Meya wa Ilala,Mh. Jerry Silaa wakifurahia jambo mara baada ya kufanyika kwa Uzinduzi Rasmi wa Mfuko wa Bonnah Trust Fund,mapema leo asubuhi kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Friday, October 11, 2013

HUKUMU - ALIYEKUWA MEYA WA JIJI LA MWANZA NA WENZAKE WAACHIWA HURU

Picha ya moja ya hukumu zilizosomwa mwaka 2010 ikimuonyesha aliyekuwa Meya wa jiji la Mwanza Bihondo (kushoto) na watuhumiwa wengine (waliofunika nyuso).
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imewaachia huru watuhumiwa wanne akiwemo aliyekuwa meya wa jiji la mwanza LEONARD BIHONDO waliokuwa wakikabiliwa kesi ya mauaji ya aliyekuwa katibu wa CCM kata ya isamilo marehemu BAHATI STEPHANO aliyeuawa kikatili mei 14 mwaka 2010 kwa kuchomwa kisu katika ziwa lake la kushoto akiwa ofisini kwake katika eneo la Nera jijini Mwanza.
 
Akitoa hukumu ya kesi hiyo namba 79 ya mwaka 2011 Jaji mfawidhi wa mahakamu kuu kanda ya Mwanza AISHIEL SUMARI amesema kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri umeshindwa kuwatia hatiani washitakiwa wote wanne na hivyo kuwaachia huru.
 
Jaji SUMARI amesema kuwa  maelezo ya shahidi namba 16 na 18 ambao walikuwa  askari polisi waliokabidhiana mtuhumiwa namba moja ulikuwa na mkanganyiko kutokana na  hatua ya Jamhuri kushindwa  kumpeleka mahakamani aliyekuwa mkuu wa polisi wilaya ya Nyamagana THADEO MALINGUMU ambaye angeweza kuondoa mkanganyiko huo kuhusu mtu aliyechukuliwa na Polisi na mtuhumiwa aliyetolewa ziwani.
 
Amesema kuwa ushahidi uliotolewa na Jamhuri ni utambuzi wa mahakamani na siyo wa eneo la tukio ambapo mahakama haiwezi kumtia hatiani mshitakiwa huyo wa kwanza ambaye awali alipatikana  na kesi ya kujibu.
 
Kuhusu washitakiwa wengine BALTAZAR SHUSHI, ABDUL AUSI pamoja na mshitakiwa wa nne aliyekuwa meya wa jiji la mwanza LEONARD BIHONDO ambao waliunganishwa kwenye kesi hiyo namba 79 ya mwaka 2011 baada ya kutajwa na mshitakiwa wa kwanza jaji SUMARI amesema kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa jamhuri umeshindwa kuwatia hatiani.
 
Jaji SUMARI ametolea mfano hatua ya jamhuri kushindwa kuwasilisha vielelezo vinavyothibitisha  kuwepo kwa mawasiliano ya simu baina ya mshitakiwa wa kwanza JUMANNE OSCAR na mshitakiwa wanne LEONARD BIHONDO.

Kutokana hali hiyo,Jaji Sumari amesema kuwa ameridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri kuwa haukuwatia hatiani na hivyo kuwaachia huru washitakiwa wote wanne na kutoa fursa kwa upande wa jamhuri kukata rufaa ikiwa haujaridhika na uamuzi huo wa mahakama.
 
Bahati Stephano aliyekuwa katibu wa CCM kata ya isamilo aliuwawa kikatili mei 14 mwaka 2010 kwa kuchomwa kisu katika ziwa lake la kushoto akiwa ofisini kwake katika eneo la nera jijini mwanza.

SAFARI NJIA YA KATI NA UTALII WA NDANI.

Mifugo.

Harakati za maisha.

Wanakijiji.

Hapa chini sijui ni minara ya kumbukumbu gani?

Nyumba zetu.

Mjengo.

House.

Biashara.

Ni mafuta ya alizeti.

Mkaa full kiwango.

Hatua za ujenzi pango la biashara.

YALIVYOKUWA MAZISHI YA BABA MZAZI WA MWANDISHI PETER FABIAN

Peter Fabian (mwenye koti ya brown) akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu baba yake mzazi katika ibada ya mazishi iliyofanyika kisiwa cha Ukerewe  mkoani Mwanza.

Ndugu wa marehemu wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu.

Kusanyiko katika ibada ya mazishi nyumbani alikozaliwa marehemu.

Ibada ikiendelea.

Mwili wa marehemu ukishushwa kwenye yake makazi ya milele.

Kaka wa marehemu akiweka mchanga.

Peter Fabian ambaye ni mwandishi wa habari wa gazeti la Mtanzania na Mzawa la jijini Mwanza akiweka mchanga kwenye kaburi la marehemu baba yake.

Huduma muhimu  katika ibada ikiendelea.

'Kwaheri' ni kauli ambayo inamtoka mama huyu.

G. Sengo iliwakilisha kwenye msiba huu.


Dada wa marehemu. wakiweka mashada ya maua.

Watoto wa kiume wa marehemu.

Mtoto wa marehemu ambaye ni kaka mkuu naye akiweka shada la maua kwenye kaburi.

Wajukuu wa marehemu.

Kaka wa marehemu.

Mwakilishi wa wanahabari Mwanza Albert G. Sengo naye akiweka shada la maua kwenye kaburi la baba wa mwandishi wa habari mwenziye.

Mwisho kabisa Shangazi alikuwa na neno kwa wana familia. (Sauti kuwajia punde)

ZAWADI ZA ROCK CITY MARATHON 2013 ZATANGAZWA

Mratibu wa mbio za Rock City Marathon 2013, Bw. Mathew Kasonta (kulia) akipokea mfano wa tiketi ya ndege kutoka kwa Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika la Ndege la Precision Air (PW), Bw. Patrick Ndekana (kushoto), ambayo itatolewa kwa mshindi wa mwaka huu atakaevunja rekodi ya 1:04:02 iliyowekwa na Kopiro Mwita katika mbio za kilometa 21 za Rock City Marathon mwaka jana. PW pia ni msafirishaji mkuu wa mbio za Rock City Marathon 2013. Wapili kushoto ni Mkuu wa Idara ya Masoko na Uhusiano wa Precision Air, Bi. Linda Chiza, na Meneja Matukio wa kampuni ya Capital Plus International Ltd, Bi. Grace Sanga.
Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika la Ndege la Precision Air (PW), Bw. Patrick Ndekana (katikati), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya udhamini wa shirika lake katika mbio hizo kama wasafirishaji wakuu katika mbio hizo na kutoa tiketi bure kwa mshindi wa mwaka huu atakaevunja rekodi ya 1:04:02 iliyowekwa na Kopiro Mwita katika mbio za kilometa 21 za Rock City Marathon mwaka jana. Kulia ni Mratibu wa mbio hizo Bw. Mathew Kasonta aliyetangaza zawadi zilizoboreshwa kwa mshindi wa mwaka huu, na kushoto ni Mkuu wa Idara ya Masoko na Uhusiano wa Precision Air, Bi. Linda Chiza.
Mratibu wa mbio za Rock City Marathon 2013, Bw. Mathew Kasonta (Kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kutangaza zawadi za mbio za Rock City Marathon mwaka huu. Kushoto ni Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika la Ndege la Precision Air (PW), Bw. Patrick Ndekana  ambaye alieleza juu ya udhamini wa shirika lake katika mbio hizo kama wasafirishaji wakuu katika mbio hizo na kutoa tiketi bure kwa mshindi wa mwaka huu atakaevunja rekodi ya 1:04:02 iliyowekwa na Kopiro Mwita katika mbio za kilometa 21 za Rock City Marathon mwaka jana. 
Mratibu wa mbio za Rock City Marathon 2013, Bw. Mathew Kasonta (wapili kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kutangaza zawadi za mbio hizo kwa mwaka huu. Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika la Ndege la Precision Air (PW), Bw. Patrick Ndekana  ambaye alieleza juu ya udhamini wa shirika lake katika mbio hizo kama wasafirishaji wakuu katika mbio hizo na kutoa tiketi bure kwa mshindi wa mwaka huu atakaevunja rekodi ya 1:04:02 iliyowekwa na Kopiro Mwita katika mbio za kilometa 21 za Rock City Marathon mwaka jana. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Masoko na Uhusiano wa Precision Air, Bi. Linda Chiza na kulia ni Meneja Matukio wa kampuni ya Capital Plus International Ltd, Bi. Grace Sanga. 
Zawadi za Rock City Marathon 2013 zatangazwa
Na Mwandishi Wetu.
Waandaji wa mbio za Rock City Marathon 2013, kampuni ya Capital Plus International (CPI) wametangaza kutenga shilingi milioni kumi kama zawadi katika mbio hizo zilizopangwa kufanyika mwezi Oktoba tarehe 27 katika viwanja vya CCM Kirumba mkoani Mwanza. 

Katika kunogesha mbio hizo na kuifanya iwe ya ushindani zaidi, shirika la ndege la Precision Air (PW), mbali na kuwa wasafirishaji wakuu wa Rock City Marathon 2013, limetangaza kutoa tiketi ya kwenda na kurudi jijini Dar es Salaam kwa mshiriki atakaevunja rekodi ya muda wa 1:04:02 iliyowekwa na Kopiro Mwita katika kilometa 21 mwaka uliopita.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana wakati wa kutangaza zawadi hizo, Mratibu wa mbio hizo Bw. Mathew Kasonta alisema zawadi kwa mbio za mwaka huu zimeboreshwa zaidi na kuongeza kuwa washindi katika mbio za kilometa 21 kwa wanaume na wanawake watajinyakulia shilingi milioni 1.5/- kila mmoja, 900,000/- kwa washindi wa pili na 700,000/- kwa washindi wa tatu.

“Tunahamasisha washiriki kujitokeza kwa wingi kwa sababu zawadi kwa mbio za mwaka huu zimeboreshwa baada ya kupata mwitikio mzuri kutoka kwa wadhamini wetu ambao ni NSSF, Africa Barrick Gold (ABG), Precision Air, Airtel, Bank M, PPF, Nyanza Bottling Ltd, New Mwanza Hotel, Sahara Communications, Continental Decoders na Umoja Switch,” alisema Bw. Kasonta.

Kasonta alisema washindi katika kilometa 5 wa mbio maalum kwa wafanyakazi kutoka makampuni mbali mbali, watapatiwa zawadi za kiheshima na fedha wakati washindi kwenye mbio za kilometa 3 ambazo washiriki wake ni wazee na watu wenye ulemavu wa ngozi wataondoka na zawadi ya shilingi  elfu 50,000/- kwa mshindi wa kwanza, 30,000/- kwa wa pili na 20,000/- wa tatu.

“Kwa mbio za kilometa 2 kwa watoto kati ya umri wa miaka 7 mpaka 10, mshindi atajinyakulia shilingi elfu 30,000/-, 20,000/- kwa mshindi wa pili na 15,000/- kwa mshindi wa tatu,” aliongeza.

Alisema mbali na zawadi ya fedha taslim, wasindi watakaoshika nafasi ya kwanza hadi ya tatu katika vipengele vyote (wanawake kwa wanaume) watapatiwa vingamuzi vya Continental, isipokuwa washindi wa kwanza wa kilimeta 21.

Aidha, Mkurugenzi wa Biashara wa Shirika la Ndege la Precision Air, Bw. Patrick Ndekana alisema kuwa udhamini wa shirika lake katika mbio hizo unadhihirisha jitihada za shirika lake za kuendeleza michezo nchi nzima.
“Tunafuraha kuwa sehemu ya wadhamini wa mbio za Rock City Marathon 2013 na tunaamini udhamini wetu utasaidia kuendeleza mchezo wa riadha  katika mikoa ya kanda ya ziwa na nchi nzima kwa ujumla.

"Tunajivunia kuunga mkono mbio hizi tukiwa kama shirika la ndege la wazawa kwa kufanya upendeleo kwa wananachi wetu katika kukuza vipaji vyao vya michezo, wakiwa ni mabalozi wazuri wa nchi yetu kama Precision Air inavyoendelea kupeperusha vyema bendera ya nchi hii kwa zaidi ya miaka 22 sasa. Mbio hizi pia zinalenga kukuza utalii katika kanda ya ziwa na kwa vile Mwanza ni kitovu cha pili cha biashara ya Precision Air, shirika tayari limejidhatiti kukuza maendeleo ya mkoa huu. Tayari tunasafiri mara 30 kwa wiki, tukiwa na uhusiano madhubuti na watalii wetu kwa kuwapatia usafiri wa uhakika na ulio salama.

“Shirika linatambua umuhimu wa kuunga mkono jititaha za kufufua mchezo wa riadha ambao ulilitetea taifa heshima kubwa siku za nyuma,” aliongeza Ndekana.  
      
Fomu za usajili wa mbio hizo zinapatikana katika ofisi za kampuni ya Capital Plus International jijini Dar es Salaam, Viwanja vya Nyamagana mkoani Mwanza. Fomu pia zinanunuliwa kwa kupitia Airtel Money kwa kutuma fedha kwenye neno fumbo ‘MARATHON’.

“Utakapomaliza muamala huo, utapokea ujumbe ambao utauwakilisha pale utakapochukua fomu yako ya usajili katika ofisi kuu za Airtel jijini Dar es Salaam pamoja na maduka yote ya Airtel yaliyopo Dodoma, Zanzibar, Mbeya, Arusha na Mwanza,” alisema Kasonta.

FILAMU YA DASMILA KUTINGA SOKONI MWISHONI MWA MWEZI HUU

FILAMU  ya DASMILA inatarajia kuingia sokoni mwishoni mwa mwezi huu akizungumza katika safu hiiMkurugenzi wa  DJ Marketing & Promotion ambao ndio wasambazaji wa kazi hiyo,Haulle Daniel amesema kazi hiyo ime kamilika kwa asilimia zote hivyo wapenzi wa filamu wakae mkao wa kula kwani imewashilikisha wasanii wengi akiwemo Shamsa Frod,Jack Pentzel, Elias Mkali, Shaban Dicosta na wasanii wengine wanaotamba katika anga za filamu nchini
Filamu hiyo ya mapenzi ambayo kuna mambo mbalimbali ya kuelimisha jamii ya kitanzania  ambapo
DASMILA aliyeuawa kipindi cha nyuma kidogo, arudi tena kama mzimu, na mengi yanatokea. Fuatilia.. Familia, vichekesho na vimbwanga, mapenzi, kukosa uaminifu, visa na mikasa kibao
 ambayo yatapatikana katika filamu hiyo ambayo imetengenezwa kwa ubora wa ali ya juu na itakayokuwa ikisambazwa na kampuni ya kizalendo ya DJ Marketing ya jijini Dar es salaam

P-SQUARE KUGONGA SHOW TZ MWEZI UJAO.

Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi (Zembwela)akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza ujio wa wasanii wa muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – Square kutoka nchini Nigeria pamoja na mdhamini Mkuu,Tarehe 23 Mwezi ujao ndipo watawasili nchini. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo. Pamoja nae katika Picha ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa ambo ndio wadhamini wa onesho hilo.
Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza ujio wa wasanii wa Muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – square kutoka nchini Nigeria chini ya udhamini wa Vodacom, watakaowasili Tarehe 23 Mwezi ujao. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo. Pamoja nae katika picha ni Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi (Zembwela).

Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini maelezo kutoka kwa wazungumzaji Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi (Zembwela). Na Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa , wakati wa Kutangaza ujio wa wasanii wa Muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – square kutoka nchini Nigeria, Tarehe 23 Mwezi ujao. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo. 

AIRTEL YATOSHA BABA LAO YATANUA KIFUA ZAIDI TENA

Airtel Yatosha Baba lao yazidi kutanua kifua

*        Kwa beil ile ile ya shilingi 999 unapata  SMS bila kikomo, dakika 55 na MB 500 kuperuzi mitandao upendavyo
Airtel Tanzania kupitia vifurushi vyake vya Yatosha imeendelea kujiimarisha zaidi ikiwa ni siku chache tangu kumalizika kwa promosheni yake kabambe ya shinda nyumba 3.

Akiongea kuhusiana na BABA LAO ilivyozidi kufunguka kwa kuboreshwa zaidi Mkurugenzi wa Masko  wa Airtel Tanzania Levi Nyakundi  alisema "Airtel Yatosha baba lao imenogeshwa zaidi tena! 

Tunasema yaani Ni Airtel yatosha ni Baba lao na bado itaendelea kubakia hivyo, kwa sasa kwa shilingi 999 tu mteja atapa SMS bila kikomo kwenda mtandao wowote, MB 400 za kuperuzi intanet na pia atapata dakika 55 zakupiga simu kwenda mtandao wowote nchini Ikumbukwe kuwa vifurushi vyote vya siku vya yatosha vinadumu kwa masaa 25 tangu mteja anapojiunga hii ni kwa lengo maalum kabisa kumfanya mteja wetu yeyote aweze kufurahia thamani ya pesa yake katika huduma zetu

Lengo letu ni kuona Huduma yetu ya Airtel yatosha baba lao inaendelea kuwafaidisha watanzania kuendelea kuokoa pesa nyingi zaidi walizokuwa wakitumia kwenye mawasiliano na kuanza kuzitumia katika shughuli nyingine za uchumi wa taifa na jamii kwa jumla Kujiunga na kifurushi chochote cha SIKU, WIKI au MWEZI piga *149*99# 

Nae meneja Masoko wa Airtel Bi, Anethy Muga alisema "Ikiwa utajiunga na vifurushi hivi vilivyoongezewa muda na dakika ni hakika kabisa kuwa utaokoa pesa nyingi na utaweza kujiweka katika nafasi nzuri sana yakupanga mambo mengi ya kiuchumi kwa kuwa unaokoa pesa nyingi" Airtel yatosha inaendelea na mkakati wa kutosha zaidi kumtimizia mtanzania haki yake ya mawasiliano kwa kumpa mawasiliano nafuu huku Airtel pia ikihakikisha mawasiliano madhubuti yanapatikana alieleza Bi, Muga

Promosheni ya Airtel yatosha sjhinda nyumba 3 ilikwisha mwanzoni mwa wiki hii, laikini bado huduma ya yatosha inaendea na sasa vifurushi vya huduma hiyo vimeongewa zaidi kwa lengo la kuifanya huduma hiyo kuwanufaisha wateja zaidi.

Thursday, October 10, 2013

ALIYEMCHOMA MWENZAKE NA KISU HADI KUMUUA NAYE AUAWA MWANZA.

TUNAOMBA RADHI PICHA ZINAZOFUATA ZINATISHA
Huyu ndiye marehemu kijana maarufu kwa jina la 'Mkandarasi' anayesadikika kufanya mauaji kwa mumchoma kijana mwenzake kisu naye aliuawa na wananchi wenye hasira katika mtaa wa Msikiti wa Ijumaa jijini Mwanza.
NA ALBERT G. SENGO: MWANZA

Watu wawili wameuawa katika tukio la utata lililotokea jana asubuhi majira ya saa 3 na dakika kadhaa, katika eneo la barabara ya msikiti wa Ijumaa jijini Mwanza.

Chanzo cha mauaji hayo kinadaiwa kuwa kilisababishwa na kijana mmoja maarufu kwa jina la Mkandarasi kumchoma kisu kijana mwenzake ambaye alikuwa mgeni akifanya kazi za usaidizi kwa mamantilie wanaopika chakula katika moja ya viunga vya ndani eneo la vichochoro vya mtaa wa Msikiti wa Ijumaa kufuatia majibizano ambayo yalisababisha kijana Maarufu kwa jina la 'Mkandarasi' amchome mwenzake kisu cha shingoni na sehemu nyingine za mwili.

Kijana huyo alipoona amezidiwa alitafuta upenyo na kukimbia huku damu zikimchirizika, hata hivyo hakufika mbali kwani alizidiwa na hatua chache baadaye alianguka chini nakuaga dunia.

Wananchi wenye hasira walimzingira muuaji ambaye naye alikuwa akijihami kwa kisu alichokuwa nacho mkononi na ndipo walipofanikiwa kumbwaga chini na kumshambulia kwa mawe hadi umauti. 

Akisimulia juu ya mkasa huo mmoja kati ya mashuhuda Peter Nyamoko anahadhithia. (Msikilize kwa kubofya play)


Naye ndugu wa marehemu aliyeuawa kwa kuchomwa kisu alipohojiwa na G. Sengo alijibu kwa ufupi. (Msikilize kwa kubofya play)


Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza linataraji kuja na taarifa kamili ya Uchunguzi wake hii leo.
Maafisa polisi na wananchi wakiwa wameuzingira mwili wa marehemu Mkandarasi.

Umati wa watu mtaa wa Msikiti wa Ijumaa.

Mashuhuda wakiutizama mwili wa kijana aliyeuwa kwa kuchomwa kisu.

Mwili wa kijana aliyekuwa akifanya kazi kwa mamalishe mtaa wa Msikiti wa Ijumaa ukiwa umelowa damu  mara baada ya kuchomwa kisu kufuatia majibizano na jamaa (maarufu kwa jina la 'Mkandarasi') ambaye naye aliuawa na wananchi wenye hasira waliojichukulia sheria mkononi.

Mashuhuda.

Polisi walifika eneo la tukio na kisha wakaondoka na miili ya marehemu hao nao wengine wakibakia eneo la tukio kubaini nini chanzo.

Mwananchi akifukia damu zilizotapakaa kwenye barabara.