ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 10, 2013

WALIO MWAGIWA TINDIKALI ZENJI WAENDA UINGEREZA

Raia wawili wa Uingereza, Katie Gee (18) na Kirstie Trup (18) waliomwagiwa tindikali visiwani Zanzibar juzi na kulazwa Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam, wamesafirishwa kwenda kwao kwa matibabu zaidi.
Aidha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imetangaza zawadi ya Sh10 milioni kwa mtu yeyote atakayesaidia kukamatwa wahalifu waliowamwagia tindikali raia hao wa Uingereza. Akizungumza na wanahabari mjini Zanzibar, Waziri wa Habari, Utamaduni na Utalii wa SMZ, Said Ali Mbarouk alisema wanafanya hilo kwa lengo la kupata ushirikiano kutoka kwa wananchi ikiwa pia moja ya njia za kukomesha matendo hayo.
Taarifa zilizopatikana jana zilidai kuwa raia hao ambao walidhurika katika maeneo ya kifuani, usoni na mikononi baada ya kumwagiwa tindikali na vijana waliokuwa wakiendesha pikipiki, maeneo ya Shangani Zanzibar, walichukuliwa hospitalini hapo juzi saa 1 usiku.
Raia wa Uingereza waliomwagiwa tindikali wakiwa kisiwani Zanzibar 
Habari za uhakika kutoka Hospitali ya Aga Khan, zilithibitisha kuwa Katie na Kirstie walichukuliwa na kusafirishwa kwenda Uingereza kwa matibabu zaidi. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Mkumbwa Ally alisema kuwa wizara hiyo haikuhusika kuwasafirisha na kwamba amepata taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa wameondoka nchini.
“Nilisikia tu kwenye vyombo vya habari kwamba wamekwenda kutibiwa nje, sisi hatukuhusika hiyo ni mipango yao,” alisema Ally.
Hata hivyo, gazeti la The Telegraph la Uingereza jana liliripoti kuwa raia hao walikuwa njiani kuelekea nchini humo na kwamba wazazi na ndugu wa vijana hao walipokea kwa mshituko taarifa za tukio hilo.
Taarifa iliyotolewa kwa niaba ya familia hizo ilisema kuwa wamesikitishwa na kilichotokea wakikitaja kitendo hicho kuwa ni tukio lisilotamkika kuwatokea mabinti zao waliokwenda Zanzibar kwa nia njema.

BENDI YA MSONDO NGOMA ILIVYO PAGAWISHI WAPENZI WAKE SIKUKUU YA IDDI

Waimbaji wa bendi ya msondo ngoma wakitoa burudani wakati wa onesho lao la Iddi lililofanyika katika ukumbi wa DDC Kariakoo Dar es salaam kushoto ni Eddo Sanga na Hasani Moshi.
Tumba, bass na solo shughulini...


Wapuliza hara wa bendi ya msondo ngoma wakitoa burudani wakati wa sikukuu ya idi kushoto ni Hamisi Mnyupe na Romani Mng'ande. 


Saddy Ally akiwajibika katika drums... Picha na SUPER D


BONDIA FRANCIS MIYEYUSHO AKKALISHA MZAMBIA KWA K,O RAUNDI YA 8

Bondia Mtanzania Francis Miyeyusho kulia  akipambana na Fidelis Lupupa wa Zambia wakati wa  mpambano wao wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika wakati wa Sikuku ya Iddi katika ukumbi wa Dar Live Mbagara Miyeyusho alishinda kwa K,O ya raundi ya nane.


Bondia Mtanzania Francis Miyeyusho kushoto  akipambana na Fidelis Lupupa wa Zambia wakati wa  mpambano wao wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika wakati wa Sikuku ya Iddi katika ukumbi wa Dar Live Mbagara Miyeyusho alishinda kwa K,O ya raundi ya nane 

Bondia Kasimu Rajabu akipambana na Kevin Fabian wakati wa mpambano wake uliofanyika jana sikukuu ya Iddi katika ukumbi wa Dar Live Mbagara Fabian alishinda kwa point.

Bondia Godfrey Pancho kushoto akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Hamisi Mohamedi wakati wa mpambano wao uliofanyika sikukuu ya Iddi mosi katika ukumbi wa Dar Live Mbagara

Bondia Godfrey Pancho kulia akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na Hamisi Mohamedi wakati wa mpambano wao uliofanyika sikukuu ya Iddi mosi katika ukumbi wa Dar Live Mbagara

Bondia Chipaki Chipindi akiwa na mashabiki wake baada ya kumkarisha raundi ya kwanza bondia Ramadhani Kido.

Bondia Fidelis Lupupa wa Zambia akiwa chini amekaa akijifikilia kuwa aendelee au asienderee baada ya kupigwa na bondia Mtanzania Francis Miyeyusho wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagara Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa K,o ya raundi ya nane 

Bondia Mtanzania Francis Miyeyusho kulia  akipambana na Fidelis Lupupa wa Zambia wakati wa  mpambano wao wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika wakati wa Sikuku ya Iddi katika ukumbi wa Dar Live Mbagara Miyeyusho alishinda kwa K,O ya raundi ya nane

Bondia Fidelis Lupupa wa Zambia akiwa chini amekaa akijifikilia kuwa aendelee au asienderee baada ya kupigwa na bondia Mtanzania Francis Miyeyusho wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagara Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa K,o ya raundi ya nane
Bondia Mtanzania Francis Miyeyusho kushoto  akipambana na Fidelis Lupupa wa Zambia wakati wa  mpambano wao wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika wakati wa Sikuku ya Iddi katika ukumbi wa Dar Live Mbagara Miyeyusho alishinda kwa K,O ya raundi ya nane 


Miyeyusho akishangilia ushindi. 


Miyeyusho katika pozi.Picha zote na SUPER D

Friday, August 9, 2013

FBME WASABABISHA TABASAMU KWA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU WA KITUO CHA AL MASJID IBRAHIM BUTIMBA MWANZA

Meneja wa tawi la FBME Bank Mwanza Ndugu Joseph Gwalugano (kulia) akimkabidhi Imam Abeid Musa Mafuta ya kupikia kwenye hafla fupi iliyofanyika katika msikiti wa Al Masjid Ibrahim Butimba Mwanza.

Jumanne Hassan mfanyakazi wa benki ya FBME Mwanza akimkabidhi mtoto Abdalla, katoni ya amaji ya kunywa

Mfanyakazi wa FBME Bank Mwanza Lena Gahanga (wa pili toka kushoto) akimkabidhi mbuzi mtoto Salima Hamad.

Wafanyakazi wa FBME Bank - Tawi la Mwanza wakiwakabidhi vitu mbalimbali watoto yatima katika msikiti wa Al Masjid Ibrahim - Butimba ikiwa ni maalum kwaajili ya kusherehekea sikukuu ya Eid El Fitri

Meneja wa Tawi la benk ya FBME Mwanza akifafanua jambo wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika msikiti wa Al Masjid Ibrahim Butimba huku wafanyakazi wenzake wakimsikiliza

Mfanyakazi wa benki ya FBME Mwanza Mazigo Musiba akimkabidhi Mbuzi mtoto Fatma Fereji kama ishara ya kuwatakia kheri watoto hao na sikukuu ya Eid El Fitri.

Wafanyakazi wa Bank ya FBME tawi la Mwanza wakifurahia jambo baada ya kukabidhi vyakula kwa watoto yatima waliopo msikiti wa Al Masjid Ibrahim Butimba Mwanza

Wafanyakazi wa benki ya FBME tawi la mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto yatima viongozi wa msikiti Al Masjid Ibrahim - Butima Mwanza.

Wafanyakazi wa Benki ya FBME wakifuatilia tukio, kuanzia kulia ni Lena Gahanga, Rehema Mbalike, Jumanne Hassan, Mazigo Musiba na Peter Nkenguye - Mwan Nzengo

Watoto wa msikiti wa Al Masjid Ibrahim wakitafakari.

Watoto wanaoishi mazingira magumu wa msikiti wa Al Masjid Ibrahim Butimba wakipokea vitu mbalimbali vilivyo tolewa na Benki ya FBME Mwanza kwa ajiri ya sikukuu ya Eid El Fitri ambapo hii imekuwa ni moja ya taratibu za benki hiyo inazozifanya zama za sikukuu mbalimbali.
Blogu hii inatoa pongezi kwa Benki ya FBME kwa utaratibu huu unaofanyika kila mwaka kwa watoto wetu waishio mazingira magumu.

MWANZA YAONGOZA MBIO ZA BAISKELI ZA SAFARI LAGER KANDA YA ZIWA ZILIZOFANYIKA SHINYANGA.

Akinamama wakiwa tayari kuanza mbio zilizotia fora kuzunguka uwanja mara 10 wakiendesha baiskeli na ndoo za majikichwani.
Wanaume wakijipinda katika mbio za baiskeli kilometa 210 chini ya Udhamini wa Safari Lager. 


Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli kilometa 210 wanaume Masunga Dubha kutoka mkoa wa Mwanza akifurahia kitita cha shilingi milioni moja alichotwaa mara baada ya kunyakuwa ushindi wa kwanza kwwenye mbio hizo chini ya Udhamini wa Safari Lager. 


Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli kilometa 130 wanawake Matha Anthony kutoka wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza akifurahia kitita cha shilingi laki saba alichotwaa mara baada ya kunyakuwa ushindi wa kwanza kwwenye mbio hizo upande wa wanawake chini ya Udhamini wa Safari Lager. 


Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli walemavu kuzunguka uwanja mara 30 wanaume Ngalu Ngamba kutoka mkoa wa Shinyanga akipokea kitita cha shilingi laki moja alichokitwaa mara baada ya kunyakuwa ushindi wa kwanza kwwenye mbio za walemavu baiskeli za miguu mitatu kwa Udhamini wa Safari Lager. 


Mshindi wa akinamama waliokimbiza baiskeli kuzunguka uwanja mara 10 Eliza Shilu akipokea zawadi yake toka kwa mgeni rsmi wa mbio za Baiskeli za Safari Lager 2013 zilizofanyika mkoani Shinyanga.


Ilikuwa ni majira ya saa 1:30  asubuhi mbio za baiskeli za miguu mitatu zilitimua vumbi ndni ya uwanja wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga ambapo washiriki walizunguka uwanja mara 30.


Mbio za baiskeli miguu mitatu zilivyokuwa.


Hawa ndiyo washindi wa mbio hizo kutoka kulia ni mshindi wa kwanza Ngalu Ngamba, mshindi wa pili ni Peter Thomas na mshindi wa tatu Makende Ndelema.


Mshindi wa mbio za baiskeli kuzunguka uwanja mara 10 na ndoo kichwani Eliza Shilu (kushoto) akijitutumua katika raundi ya tisa ambapo hapa alikuwa tayari kesha wazidi wenzake raundi mbili hatimaye akamaliza mbio hizo akiwa mshindi.


Ni mbio za aina yake ambazo zilitia nakshi mashindano ya mbio za Baiskeli na Safari Lager mkoani Shinyanga.


Kadri muda ulivyokuwa ukisonga umati wa watazamaji ulikuwa ukiongezeka hatimaye ikafikia kipindi uwanja ukafunga kabisa na nyomi ya kutosha.


Macho yalielekezwa geti kuu.


Nyomi la wahudhuriaji mbio za baiskeli za Safari Lager 2013 mkoani Shinyanga.


Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli kilometa 130 wanawake Matha Anthony kutoka wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza  akimaliza mbio...


Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli kilometa 130 wanawake Matha Anthony kutoka wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza  hapa ni wakati akienda kukabidhiwa namba ya ushindi wa kwanza, pembeni yake ni mwandishi wa Star Tv Shinyanga Shahban Ley akichukuwa matukio.


Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli kilometa 210 wanaume Masunga Dubha kutoka mkoa wa Mwanza akifurahia kumaliza mbio na ushindi alio upata kwenye mbio hizo.


Washiriki wengine mbio za baiskeli wanaume.


Meneja wa TBL Mkoa wa Shinyanga Robert Kazinza akizungumza na maelfu ya watazamaji wa Mashindano ya Mbio za Baiskeli za Safari Lager 2013 zilizofanyika na kufana mkoani Shinyanga.


We ulikuwa wapi..?


Au hapa...?


Wadau wote wa nguvu wa TBL Kanda ya Ziwa wote waliweka maskani mjini Shinyanga.


Mambo ya Safari lager.