ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 11, 2013

CLOUDS MEDIA GROUP YAZINDUA MSIMU WAKE MPYA KWA KISHINDO MJINI DODOMA LEO, YAFANYA SEMINA DHIDI YA UHARAMIA WA KAZI ZA WASANII


Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh Zitto Kabwe ambae pia ni mdau kubwa wa Muziki hapa chnini,pia alikuwa ni mmoja wa wazungumzaji kwenye semini hiyo iliyohusu na  harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi za wasanii,iliyofanyika mapema leo kwenye ukumbi wa hoteli ya African Dreams,nje kidogo ya mji wa Dodoma. Kutakuwepo na kampeni ya matembezi ya hisani ya harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi za wasanii yatakayofanyika kesho,wabunifu na wavumbuzi mbalimbali, mseto wa shuguli mbalimbali zitahusishwa.  Aidha pia mchana huu kutakuwepo na burudani hadhara ya sanaa za kisasa na za kitamaduni,mpira, chakula na bidhaa mbalimbali za kitanzania katika uwanja wa jamhuri .


Mmoja wa wasemaji kwenye semina hiyo aliyejitambulisha kwa jina la   Patrick Ngowi  kutoka kampuni ya Helvetic Solar Contractors, akizungumzia fursa mbalimbali kuhusiana na mambo ya ujasiliamali na pia alielezea ni namna gani amefanikiwa mpaka kufikia kumilimiki lampuni yake binafsi kupitia fursa alizokuwa akikumna na nazo na kuzifanyia kazi vilivyo.

Mmoja wa washiriki wa semina hiyo akiuliza swali kwa Mh Zitto Kabwa kuhusiana na mambo mbalimbali ya ujasiliamali na namna ya kuzitumia fursa hizo katika kujikwamua kimaisha.
Mh Zitto kabwe akimsikiliza mmoja wa washiriki wa semina hiyo alipokuwa akiulizwa kuhusiana na suala la fursa zinazopatikana kwa vijana na namna ya kuzitumia katika ujumla wa kujikwamua na ugumu maisha,ambapo watanzania wengi wamekuwa wakizilalamikia.



Mtangazaji wa clouds FM kupitia kipindi cha Power Breakfast-Gerald Hando akiikaribisha Meza kuu pamoja na wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye uzinduzi wa msimu mpya wa Clouds Media Group unaokwenda sambamba na ujumbe wao thabiti kabisa  ulioitwa MADE IN TANZANIA,ikiwa na hamasa kubwa ya kuleta msingi wa fursa kwa watanzania, msukumo ikiwa ni kuwashawishi watanzania kuanza kuzifanyia kazi fursa hizi kwa umoja na maendeleo ambapo TWENZETU, inakuwa neno rasmi la mawasiliano.Kama vile haitoshi kutakuwepo na kampeni ya matembezi ya hisani ya harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi za wasanii yatakayofanyika kesho,wabunifu na wavumbuzi mbalimbali, mseto wa shuguli mbalimbali zitahusishwa  ikiwemo semina ya fursa kwa watanzania,burudani hadhara ya sanaa za kisasa na za kitamaduni,mpira, chakula na bidhaa mbalimbali za kitanzania zitapatikana uwanja wa jamhuri mapema leo mchana.

Mmoja wa wasemaji kwenye semina hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Zenno  Ngowi kutoka kampuni ya Tanzania Home Expo akizungumzia fursa mbalimbali kuhusiana na mambo ya ardhi,ujenzi,na mengineyo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria kwenye semina hiyo leo mjini Dodoma.



Mmoja wa wasanii mahiri wa Mashairi,Mrisho Mpoto akifafanua jambo kuhusiana na mambo mbalimbali katika suala zima la wasanii kujipa nafasi ya Fursa mbalimbali zinazojitokeza mbele yao na namna ya kuzifanyia kazi na kuziboresha zaidi.

Mhe Zitto Kabwe akiwasili kwenye semina hiyo mapema leo,ambaye pia alikuwa ni mmoja wa wasemaji wa semina hiyo.


Pichani ni washiriki wa semina hiyo kutoka sehemu mbalimbali mjini Dodoma leo.

Baadhi ya washiriki wakifuatilia jambo kwenye semena iliyokuwa ikiendelea mapem leo kwenye hoteli ya African Dreamz,nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Mtangazaji wa Clouds FM,Loveness Love a.k.a Diva akijitambulisha kwenye semina hiyo

Mtangazaji wa Clouds FM,Shaffih Dauda akijitambulisha kwenye semina hiyo.


Wadau wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye semina hiyo iliyoibua changamoto nyingi.

Kutoka Clouds FM,Millard Ayo,Dina Marios pamoja na Zamarad wakifuatilia jambo

Mtangazaji wa Clouds FM,Arnold Kayanda Diva akijitambulisha mbele ya washiriki waliofika kwenye semina hiyo.

Baadhi ya wasanii wakiwa ndani ya semina hiyo katika harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi zao,ambapo matembezi ya hisani yamepangwa kufanyika kesho na Waziri Mkuu Mh.Pinda anatarajiwa kuyapokea matembezi hayo.

Msanii Afande Sele na Msanii mwenzake wakiwa ndani ya semina hiyo wakifuatilia yaliyokuwa yakizungumzwa.

Mtangazaji wa Kipindi cha jahazi,Mussa Hussein akijitambulisha.

Mtangazaji wa Clouds FM,B Dozen akijitambulisha

Mbwiga Mbwiguke nae kama kawa akijitambulisha kwa washiriki wa semina hiyo.

Zamarad Mketena akijitambulisha pia.

Said Falla akichangia hoja.


Suzzy Bartazar akijitambulisha.

MASHINDANO YA UMISSETA WILAYA YA ILEMELA YAZINDULIWA RASMI

Aritaf Mansoor aka Dogo ambaye ndiye mgeni rasmi wa Ufunguzi wa Mashindani ya UMISSETA wilaya ya Ilemela akisoma hotuba yake ya uzinduzi wa michuano hiyo jana katika viwanja vya shule ya sekondari Bwiru jijini Mwanza.

Jumuiko lililofika viwanja vya shule za Sekondari Bwiru (wavulana na wasichana) kushuhudia uzinduzi.
 Mashindano ya UMISSETA ngazi ya wilaya yameanza rasmi jana katika viwanja vya shule za sekondari Bwiru (Wavulana na Wasichana).

Mashindano hayo ni hatua ya nusu fainali na fainali katika ngazi ya wilaya kwani ngazi ya awali yalifanyika na kuunda timu ya kanda.

Wilaya ya Ilemela ina jumla ya kanda 4 zinazoshiriki ambazo ni Bwiru, Buswelu, Buhongwa na Pasiansi.

Michezo inayoshindanishwa ni soka, kikapu, mikono, riadha, wavu, table tenis kwa wavulana na wasichana, bao kwa wavulana na netiboli kwa wasichana.
Juma Kasandiko Afisa Elimu ya manispaa akizungumza na wadau wa michezo katika ufunguzi wa Michuano ya UMISSETA wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

Mdau wa Michezo mkoa wa Mwanza ambaye vilevile ni Mkurugenzi wa TSC Mutani Yangwe, alichangia mipira minne ili kuboresha michuano ya UMISSETA Wilaya ya Ilemela.

Kikao cha kupanga mikakati ya mafanikio kwa michezo kwa ujumla.

BATA MBELE YA BATA NA BATA NYUMA YA BATA

Ni katika stage la Villa Park Mc Zembwela akitambulisha msafara wa shughuli nzima ya Redds Miss Nyamagana itakayofanyika leo Jumamosi (11 May 2013) ndani ya ukumbi wa JB Belmonte jijini Mwanza.

Moja kati ya warembo 18 wa Miss Nyamagana akijitambulisha kwenye stage ya Villa Park jijini Mwanza.

The parade ya warembo hao.

Lilipigwa sebene nao hawakujivunga kulainisha nyonga.

Another location.

Mwanadada Recho tayari kesha tua jijini Mwanza kusababisha na kung'arisha kona ya burudani hii leo kwenye kinyang'anyiro cha Redds Miss Nyamagana 2013 ndani ya Hotel JB Belmont Mwanza.

Kisha msafara wa warembo ulielekea Club Fusion iliyopo katikati ya jiji la Mwanza.

Party Pipoooooooo wakishow love na kamera ya G. Sengo Blog.

Bata mbele ya bata.....!!!!

Dj Victor wa Club Fusion.

Naye Dj wa Clouds Tv in the house....Siwamjua?
Oiiii...Mzukaa.

This is how we do.

Zembwela na engo ya kutambulisha warembo ambao leo ndiyo leo mmoja wao ataibuliwa na kuvikwa taji la Miss Nyamagana 2013.

Ulingoni ndani ya club Fusion Recho akipenyeza upepo wake kwa shabiki wake.

Azontoooo!!!

Ni mwendo kusomeka tu!!
Brothers.

"Uskose leo (jumamosi) Miss Nyamagana ukumbi wa JB Belmont"  Hapa ni Mwandaaji wa Redds Miss Nyamagana 2013 kupitia Stoppers Entertainment Muhksin Mambo (kushoto) akiwa na meneja wa Villa Park Mwanza Meneja Ramma (kulia)

SUPER D AFYATUA DVD TATU MPYA ZA MAFUNZO YA MASUMBWI

 
Kocha huyo wa kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini,Rajabu Mhamila ‘Super D’ ametoa DVD mpya 3 kwa ajili ya mafunzo ya mchezo wa ngumi ndani yake kukiwa na clips za mabondia  wanaofanya vizuri Tanzania kama Thomas Mashali vs Fransic Cheka na mambondia wengine mbalimbali

CD hizo zilizotengenezwa kwa umakini wa ali ya juu ambazo zitakuwa chachu kwa ajili ya kuvutia wapenzi na mashabiki mbalimbali kujua mchezo wa masumbi wakiwa wanangalia live mana DVD hizo zina maelekezo ya sheria mbalimbali ambazo zinatumika katika masumbwi

DVD hizo kwa sasa zinapatikana katika makutano ya barabara ya Uhuru na Msimbazi au unaweza kuzipata jengo la Azam lililopo mtaa wa Msimbazi karibu na kituo cha Polisi Post Gelezani kwingine ni GYM ya Amana iliyopo Ilala au unaweza kuwasiliana na kocha kwa simu 0713406938 ili uweze kupata dvd hizo kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo

Mbali ya kupatikana katika maeneo hayo pia katika mchezo mbalimbali ya masumbwi kutakuwa na CD na DVD za mafunzo wa mchezo huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.
 
Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo katika CD na DVD hizo ni ya Kalama Nyilawila ,Japhert Kaseba,Rashidi Matumla, Hassani Matumla,Thomas Mashali Dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na Francis  Miyeyusho,Japhert Kaseba na Maneno Oswald, Said Mundi na King Class Mawe. 
 
 mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika Mpambano  ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D .