ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 4, 2013

MEYA WA JIJI AONGOZA WASHIRIKI WA REDS MISS NYAMAGANA KUFANYA USAFI JIJINI MWANZA

Ni sehemu tu ya nyuso za warembo wanaowania taji la unyange wa Miss Nyamagana 2013 walioshirikiana na Mstahiki Meya  wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (CCM) kufanya usafi wa mazingira katika Mtaa wa Rufiji Wilayani Nyamagana Jijini hapa

MSTAHKI Meya  wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula akizoa taka katika zoezi la usafi aliloshirikiana na washiriki wa kinyang’anyiro Reds Miss Nyamagana mwaka 2013. 

Warembo wakifanya usafi wa kina kwenye matundu madogo ya maji katika barabara ya mtaa wa Rufiji jijini Mwanza. 


Mtangazaji wa Star Tv na kiss Fm Yvonna (kushoto) akishirikiana na warembo washiriki wa kinyang’anyiro Reds Miss Nyamagana mwaka 2013 kufanya usafi wa mazingira katika Mtaa wa Rufiji Wilayani Nyamagana Jijini hapa

Usafi haukuishia barabarani tu bali pia ulizigusa hata kaya zilizopo pembezoni mwa barabara hiyo kama mfano safi wa kuigwa katika utunzaji mazingira.

Barabara iling'aa kwani takataka zote iwe makopo, mchanga au hata karatasi ndogo kama vocha havikusalimika kubakia barabarani.

Usafi kwa pamoja ukiendelea.

Wenye maduka nao walipata somo.

Usafi makini

Mratibu wa shindano la Reds Miss Nyamagana Mc. Stopper wa Stopper Entertainment (katikati) pia mkono wake ulitumika.

Wakikusanya taka ni diwani wa kata husika (kulia) pamoja na meya, Yvonna aliyeshika toroli  na mrembo akizoa taka. 

Kona hdi kona hapa ilikuwa kona kuelekea soko la jumapili.

Mmoja wa warembo wa kuelekea kinyang'anyiro cha Miss nyamagana akizibua matundu madogo ya maji barabara ya Rufiji.

Usafi hadi miferejini.

"Msiache taka" says Mtahiki Meya Mabula kwa warembo.


MSTAHKI Meya  wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (CCM) ameongoza washiriki wa kinyang’anyiro Reds Miss Nyamagana mwaka 2013 kufanya usafi wa mazingira katika Mtaa wa Rufiji Wilayani Nyamagana Jijini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika mataa wa Rufiji ambako usfi ulikuwa ukifanyika Mstahiki Meya Mabula alisema kwamba usafi uliofanywa na warembo hao ni sehemu ya huduma ya usafi kwa jamii  inayowazunguka.

Alisema kuwa usafi wa mazingira katika jiji la Mwanza ni mpango endelevu ambapo hivi karibuni Halmashauri ya jiji inataraji kuzindua wiki ya usafi itakayowashirikisha wananchi na wadau mbalimbali ili kuendelea kudumisha ushindi wa Tuzo ya usafi na mazingira inayoshikiliwa kwa mara ya saba sasa mfululizo.

Meya alisema kwamba Wiki ya usafi na mazingira imepangwa kuzinduliwa rasimi Mei 15 mwaka huu itakayokuwa na mkakati mpya ulioboreshwa kutokana na changamoto zilizopo na zilizoonekana kupitia shughuli za usafi wa kila siku ambapo watendaji wake wamezibaini

“Warembo hawa kufanya usafi leo ni kuongeza chachu kwa wananchi kuona kwamba jukumu la usafi ni la kila mtu, kwani jamii imekuwa na imani potofu kuwa wafanyao usafi ni watu wa hali ya chini, hivyo kwa hatua hii iliyochukuliwa na warembo hawa itakuwa mfano tosha kwa jamii kubadilika”

Mstahiki Mabula pia aliipongeza Kamati ya Miss Nyamagana kupitia Kampuni ya Stopper Entertainment inayoanda mshinano hilo na kutoa wito kwa waandaaji wengine kuiga mfano huo na kuzingatia changamoto na kulenga changamoto ya usafi ili Jiji la Mwanza liendelee kutetea sifa na Tuzo ya usafi kwa kipindi kingine.

Naye mmoja wa wa warembo wanaoshiriki shindano hilo Rose Peter akiwawakilisha wenzake alisema kwamba kufanya usafi mbele ya jamii imawaongezea kujiamini na kwao wameona thamani na umuhimu wa wao kushiriki mashindano kama hayo kwani jamii katika barabara mbalimbali na maeneo waliyokuwa wakifanya usafi imelipokea zoezi hilokwa taswira chanya iliyoamsha ari kwa jamii kushiriki kila siku kutunza mazingira. 

Picha ya pamoja na Mstahiki Meya.

PROF. LIPUMBA AONGOZA MIKUTANO YA NDANI MJADALA KWA MAENDELEO YA WOTE MWANZA.


Mwenyekiti wa chama cha CUF Ibrahimu Lipumba akiwasilisha mada mbalimbali kwa wadau wapatao130 kutoka makundi mbalimbali ya jamii taasisi za kiserikal, viongozi wa dini, mashirika na vyama vya siasa waliohudhuria mkutano huo.

Mkutano huu umekuja ukiwa na maudhui ya kuimarisha mfumo wa demokrasia ndani ya vyama vya siasa na kukuza mijadala baina ya vyma, wapiga kura na taasisi mbalimbali za kijamii.

Mada zilizowasilishwa na kujadiliwa ni pamoja na :
1.Sekta ya madini na maendeleo ya wananchi wa mikoa ya ukanda wa ziwa na mchangowake katika madnelao ya taifa.

2Changamoto zinazowakabili wakulima wadogo wadogo katika sekta ya kilimo cha pamba, mazao ya chakula na sekta yaufugaji katika mkoa wa Mwanza.

3. Matatizo yanayoikabili sekta ya uvuvi na matumizi sahihi ya ziwa Victoria kwa maendeleo ya wananchi wamikoa ya kanda ya ziwa.

4.Rasilimali ya maendeleo ya watu elimu ya awali, msingi na sekondari pamoja na huduma za Afya. 

Washiriki wakifuatilia kwa makini mada ziwasilishwazo.

Washiriki eneo jingine kusanyikoni.

Umakini kwa washiriki huku wakitafakari mada.

pia washiriki walipewa fursa kuwasilisha michango yao kuishauri serikali nini kifanyike ili kuboresha huduma mbalimbali na utendaji kazi kwa jamii.

Mwenyekiti wa chama cha CUF Ibrahimu Lipumba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kujibu maswali na kuelezea ujumbe wa mkutano huo.

Engo nyingine.

Mkutano huu umefanyika ndani ya ukumbi wa JB Belmount jijini Mwanza.

BIG DAY FOR IBF, GHAHA, NIGERIA AND AFRICA



IBF/AFRICA – SATURDAY 04 MAY, 2013 – DAR ES SALAAM, TANZANIA Ghanaian fighting machine and BEIJING 2008 Olympiad Issa Samir becomes the first ever Ghanaian “IBF Youth Champion of the World” after stopping the Georgianhandsomely true man Robison Omsarashvili 1 minute 29 seconds in round 3 at the Accra National Sports Stadium last night.

Cheered on by thousands of Ghanaians who thronged the stadium from all walks of life, Samir lured the handsomely Georgian to his much anticipated “killer punches”. He peppered him with his telling jabs while dancing like a butter fly (Muhammad Ali’s style) as thousands of Ghanaians in attendance including several ministers and Nigerian Ambassador to Ghana cheered him throughout the rumble.

Every punch that BEIJING 2008 Olympiad Samir threw was calculated to do damage to the handsomely Georgian and it became obvious that his team had the perfect game plan.  Charming the Georgian with his telling jabs so as to lure him to his WEB, Samir’sfighting speed and power was awesome in that Robison could hardly see his punches coming.

As the Ghanaians kept counting when he was administering his lethal punches tearing the handsomely GeorgianSamir’s huge right drove straight to Robison’s jaw and sent him crashing on the canvas with the sound of the falling tree! It was all over even before referee May Mensah Akakpo of Ghana started counting!

In another epic rumble of the evening, Princess Helen Joseph of Nigeria became the Champion of the “IBF Intercontinental Featherweight Female Title” after humiliating the beautiful Mariana Gulyas from Hungary in the shortest fight in history.  As thousands of boxing fans (many from Nigerian community in Ghana and other who arrived by hired busses from Nigeria, including their Ambassadot to Ghana ) cheered her, Helen's brinkmanship of the game proved her rightful Princess role on the mantles of theIBF Intercontinental Featherweight division after stopping te beautful Hungarian 23 seconds in round one.          

AND! The man who is touted as the next Sugar Ray Leonard in the making Albert Mensah proved his prowess in boxing as a professional sport after beating his “arch-rival” and boatful Ben Odamettey. It was really drama as groups from each camp danced and beating their drums as the bout progressed on.

Mensah’s articulated style and strength became obvious as the rumble progressed to Odamattey’s anguish as if he wanted to teach“the Bad Boy on the Block” a lesson or two! The two made the stadium live with drums and dance from their camps but as it is always said in boxing, it was Albert Mensah who had the “last laugh” after becoming the “IBF Continental Africa Jr. Welterweight” champion by TKOed Odametey  in round 7. Years from now as they judge his performance, historians would begin at this stage when he assumed his mantles as the “IBF Continental Africa Jr. Welterweight” champion!

Thumb up to both GoldenMike Boxing Promotions Syndicate, Ghana and Nigeria for the excellent rumble. This put the Ghana way ahead of others in the continent as it consolidates its role as the “boxing powerhouse”.

Harrah to IBF as it continue its “top dog” position in boxing as a professional sport. Indeed, African professional boxing has “come of age”.

Friday, May 3, 2013

MAMONG'O KUKISANUKISHA ROCK BOTTOM LEO

Mtangazaji Philbert Kabago wa Passion Fm Mwanza akizungumza na wasanii wa kundi la Jambo Squard toka jijini Arusha wanaonekana katika picha inayofuata ambao wako jijini hapa na leo watapiga show ndani ya ukumbi wa Rock Bottom ulioko Gold Crest Hotel.
SIKILIZA MAHOJIANO HAPA KWA KUBOFYA PLAY
Mi wale wakali wa masongi kama Mamong'oo, Disco malapa na nyingi kali za mahadhi ya hip hop Masai, Pichani kutoka kushoto ni Odinal aka 'Dogo Kichaa' akiwa na Chaliii Mtoto wa Bibi aka Nigga Bombom Matatizo wakizungumza na wakazi wa Mwanza kupitia masafa ya Passion Fm ndani ya kipindi cha Michano Tyme leo hii wakitaraji kukisanukisha ndani ya Rock Bottom kwa kiingilio cha shilingi 10,000/= tu.


Kutoka kushoto ni Odinal aka 'Dogo Kichaa' akiwa na Chaliii Mtoto wa Bibi aka Nigga Bombom Matatizo wakizungumza na wakazi wa Mwanza kupitia masafa ya Passion Fm ndani ya kipindi cha Michano Tyme leo hii wakitaraji kukisanukisha ndani ya Rock Bottom kwa kiingilio cha shilingi 10,000/= tu.

MAMIA WAJITOKEZA SAFARI YA MWISHO KUMSINDIKIZA MWANASHERIA KITWALA

Mwili wa marehemu Elias Kitwala (wakili wa kujitegemea) ukiwa katika kanisa la AICT Bugarika wakati wa ibada ya kumwombea ambapo walioketi kulia ni Bi Joyce Masunga (katibu wa CCM Mkoa), Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nyamagana Raphael Shilatu wakiwana waombolezaji wengine wakiwemo viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali, mahakimu, mawakili na wafanyabiashara.

Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga akitoa salamu za rambirambi.

Mchungaji wa AICT Bugarika akitoa ushuhuda juu ya kazi njema za marehemu enzi za uhai wake kwa kulitumikia kanisa na  taifa lake.

Baadhi ya mawakili na waombolezaji wengine wakifuatilia mahubiri ya askofu wakati wa misa ya kuuga mwili wa marehemu Elias Kitwala.

Walioketi kutoka kulia ni Deogratius Rutha (katibu wa CCM wilaya ya Nyamagana), Bi Joyce Masunga (katibu wa CCM Mkoa), Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nyamagana Raphael Shilatu

Sehemu ya waombolezaji waliojitokeza leo katika misa ya kuuga mwili wa marehemu Kitwala.

Nje ya kanisa ni sehemu ya waombolezaji waliojitokeza leo katika misa ya kuuga mwili wa marehemu Kitwala.

Wanachama wa CCM kata ya Pamba na wilaya ya Nyamagana wakiwa nje ya kanisa la AICT Bugarika wakisubiri kuuaga mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM kata ya Pamba marehemu Wakili Elias Kitwala.

Misa ikiendelea utulivu ukitawala ndani ya kanisa la AICT Bgarika jijini Mwanza.

Viongozi,kutoka kushoton ni Katibu mwenezi wa CCM Nyamagana..., Simon Ntambi ambaye ni katibu wa CCM kata ya Pamba, Ole Porokwa katibu wa CCM wilaya ya Ilemela, George Masha na Dkt. Magabe ambaye ni katibu mwenezi wilaya ya Ilemela wakitafakari nje ya kanisa la AICT Bugarika.

AIRTEL YATANGAZA MSHINDI WA MILLION 50 WA PROMOSHENI YA AMKA MILLIONEA


Mwandishi wa Clouds TV Austin Bayadi ( wakwanza kushoto) akibonyesha kitufe cha komputa wakati wa droo kubwa ya mwisho ya kumtafuta mshindi wa shilingi million 50 wa promosheni ya Amka millionea ambapo bwana Layakal Akbar Thawer mkazi wa Dar es salaam aliibuka mshindi wa promotion hiyo. Wakishuhudia ni meneja uhusiano wa Airtel  Jackson Mmbando(aliyekaa katikati) akifatiwa na mwakilishi wa bodi ya michezo ya Bahati Nasibu Emmanuel Ndaki akifatiwa na Afisa masoko wa Airtel  Khalila Mbowe


Meneja Uhusiano wa Airtel  Jackson Mmbando(katikati) na Afisa masoko wa Airtel  Khalila Mbowe kwa pamoja wakionyesha droo ya kumtafuta mshindi wa millioni 50 wa Amka millionea inavyotafuta mshindi wakati wa droo hiyo iliyofanyika katika makao makuu ya Airtel Moroco na kushuhudiwa na Waandishi wa habari, akishuhudia kulia ni mwakilishi wa bodi ya michezo ya Bahati Nasibu Emmanuel Ndaki


Meneja Uhusiano wa Airtel  Jackson Mmbando(aliyekaa katikati) akiongea na wandishi wa habari (hapo pichani) wakati wa droo kubwa ya mwisho ya kumtafuta mshindi wa shilingi million 50 wa promosheni ya Amka millionea ambapo bwana Layakal Akbar Thawer mkazi wa Dar es salaam aliibuka mshindi wa promosheni hiyo.  Kushoto ni mshindi wa million 15  wa promosheni ya Amka milionea bwana Juma Ibrahim Hiza mkazi wa Dar es Saalam na kulia ni  mshindi mwingine wa shilingi milioni 15 Bwana  Adnan Ayub Khan mfanyabiashara  Simiyu.



Airtel yatangaza mshindi wa million 50 wa promosheni ya Amka millionea
·         Zaidi ya washindi 1458 wazawadiwa pesa taslimu zenye thamaniya shilingi million 626 Hadi mwisho wa promosheni hii
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imechezesha droo ya mwisho ya promosheni ya Amka millionea na kumzawadia mshindi  wa droo hiyo kitita cha shilingi million 50.

Droo hiyo kubwa na ya mwisho ilifanyika katika makao makuu ya Airtel morocco na kushuhudia na waandishi wa habari ambapo mkazi wa Kariakoo Dar es Salaam  Bwana Layakal Akbar Thawer  mwenye umri wa 60  mafanyabiashara wa duka la rangi aliibuka kuwa mshindi wa millioni 50 na kutangazwa rasmi kuwa mshindi.

Akiongea wakati wa droo hiyo, Mkuu wa kitengo cha Masoko wa Airtel Levi Nyakundi alisema,  Mpaka sasa Airtel kwa kupitia promosheni ya Amka millionea imewazawadia watanzania na wateja wengi nchini. leo tunashuhudia bwana Akbar akiibuka kuwa mshindi wa pesa taslimu shilingi million 50 kupitia promosheni hii ya Amka millionea na Airtel. 

Hii inathibitisha thamira yetu ya kutuoa huduma bora na bei nafuu huku tukiendelea kuwazawadia watanzania na wateja wetu kwa kupitia promosheni mbalimbali ikiwemo hii ya Amka millionea
Tunaahiidi kuendelea kuboresha huduma zetu na kuhakikisha tunawafikia watanzania wengi zaidi,  mpaka sasa kwa kupitia huduma ya Airtel yatosha wengi wamepata unafuu wa gharama za mawasiliano na kuwezeshwa kupiga simu kwenda mitandao yote nchini na kushuhudia kuwa kweli Airtel yatosha. 

Tunaamini kwa kuendelea kuongeza ubunifu katika huduma zetu na  kuwazawadia wateja wetu kwa kupitia promosheni mbalimbali pamoja na huduma bora zikiwemo za kibenki kupitia Airtel money na huduma ya internet ya kasi zaidi ya 3.75G wateja wataendelea kupata suluhusho la mawasiliano na za kimtandao zilizo bora , za uhakika na gharama nafuu aliongeza Nyakundi.

Akiongea kwa njia ya simu mshindi wa shilling million 50 bwana Layakal Akbar Thawer alisema “ mimi nimekuwa mteja wa Airtel kwa miaka 7 sasa na nafurahia huduma zao, napenda kuwambia watanzania washiriki promosheni hizi nao wananafasi ya kuibuka washindi. 

Promosheni ya  Amka milionea ilizinduliwa rasmi mwenzi December mwaka jana na kuongezewa muda wake mwenzi machi mwaka huu, mpaka sasa wateja zaidi ya1458 na pesa taslimu zenye thamani ya zaidi ya shilingi  million 626 zimezawadiwa kwa washindi walioibuka kutoka katika mikoa mbalimbali nchini.

Mshindi mwingine wa shilingi million 50 alipatikana na kuzawadia mwenzi watatu naye ni Mwalimu wa shule ya msingi na mkazi wa manyara kiteto bwana Grayson Safieli Kabora , huku washindi wa shilingi million 15 wakiwa ni pamoja na  Juma Ibrahim Hamza  umri wa miaka 30 na mkazi wa kawe  Dar es Saalam na Adrian Ayub khan umri wa miaka 25 mfanyabiashara Simiyu

AFLEWO KESHO KUFANYA TAMASHA KUBWA LA KUSIFU NA KUABUDU JIJINI DAR

Tamasha kubwa la kusifu na kuabudu linatarajia kufanyika leo katika ukumbi wa BCIC mbezi beach kuanzia saa 3 usiku hadi saa 12 alfajiri lenye lengo la kuliombea Taifa Amani, Upendo na uchumi. 

 Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mlezi wa Aflewo (Africa Let’s Worship) Askofu Fredy Kyara, alisema watanzania wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kwani hakuna kiingilio. Alisema kuwa, tamasha hilo
litashirikisha kwaya mbalimbali kutoka makanisa 32 ya madhehebu tofauti katika kusifu na kuabudu. 

 Askofu kyara alisema, tamasha hilo linafanyika kwa mara ya tatu tangia kuanzishwa hapa nchini mwaka 2011 na kuenea nchi zote za Afrika. “Tamasha hili limeboreshwa kwa kuongeza muiondombinu ya utendaji kazi, kwa kutanua wigo wa ushirikishwaji wa makanisa mengi,” alisema Kyara. 

 Aidha matasha mengine ya Aflewo, yanatarajia kufanyika nchi nzima kwa kufanyika kila mkoa, kwa mwaka huu litaanza kufanyika katika mikoa ya Mwanza, Moshi na Zanzibar na hatimaye Afrika yote.

MAZOEZI YA REDS MISS KIBAHA YAPAMBA MOTO


Mkufunzi wa Warembo wa Redd's Miss Kibaha Rehema Uzuwiya akizungumza na warembo hawo wakati wa mazoezi yao yanayo endelea katika ukumbi wa Vijana Kinondoni 


Warembo wa Redd's miss kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao


Warembo watakao wania taji la Redd's Miss Kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika ukumbi wa vijana Kinondoni Dar es salaam picha na www.burudan.blogspot.com