ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 30, 2013

TAHADHARI YA MAGUFULI KWA WABUNIFU WA MAJENGO YATIMIA, GHOROFA LAPOROMOKA NA KUUA DAR

Siku chache baada ya Waziri wa Ujenzi Dr. John Magufuli kuwaonya na kuwatahadharisha wabunifu majengo na wakadiriaji wa ujenzi nchini kuwa makini na waangalifu katika kazi yao na kuacha tabia ya kutanguliza rushwa, maafa makubwa yametokea jijini Dar es salaam baada ya jengo la Ghorofa 16 lililokuwa likiendelea ujenzi kuporomoka na kuwafunika watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 60.

Tukio hilo lilitokea jana ijumaa majira ya asubuhi jirani na msikiti wa Shia katika eneo la makutano ya barabara ya Morogoro na mtaa wa Indira Ghandi.

Imefahamika kuwa jengo hilo linamilikiwa na mfanyabiashara mmoja wa jijini Dar es salaam Bw. ladha khimji kwa ubia na shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Aidha, harakati zaidi za uokoaji zilikuwa zikiendelea kufanywa na vikosi vya uokoaji.

Rais Jakaya kikwete alifika katika eneo latukio hilo majira ya saa 7:00 mchana hiyo jana akifuatana na mkewe Bi. Salma kikwete na kabla yake viongozi kadhaa wa serikali na makamanda wa polisi katika Kanda Maalum ya Dar es salaam walikuwa wameshafika kusaidia shughuli za uokoaji, miongoni mwao akiwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam aid Meck Sadick.

Baadhi ya mashuhuda walieleza kuwa mabaki ya jengo hilo yalionyesha kuwa mchanga ulikuwa mwingi mno kulinganisha na saruji, hali inayodhaniwa kuwa ni moja ya sababu za kuporomoka kwa jengo hilo lililogharimu mamilioni ya pesa.

Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi aliiagiza Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji wa Majenzi (AQRB) kufanya kazi kwa uadilifu na kuzingatia sheria kwa kutanguliza uzalendo na kuepuka kufanya kazi kwa misingi ya rushwa.

Akifungua kikao cha siku mbili cha bodi hiyo majuzi katika ukumbi wa Chuo cha Benki kuu ya Tanzania Tawi la Mwanza, Dr. Magufuli aliwaeleza wataalamu na wajumbe wa kikao hicho kwamba wanayo dhamana kubwa ya kutekeleza majukumu ya taaluma yao kwa kuzingatia maadili, sheria, wajibu na kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Dr. Magufuli alisema kwamba kuporomoka kwa baadhi ya magorofa katika sehemu mbalimbali hapa nchini ni ushahidi tosha kuwa ujenzi wa majengo unakiuka utaratibu na alisisitiza wataalamu hao kuwa makini katika  utendaji wa kazi zao.

Aidha magufuli ameitaka AQRB kuwachukulia hatua za kinidhamu na kisheria wataalamu watakaohusika na usimamizi na ukadiriaji mbovu na majengo yatakayoporomoka muda mfupi baada ya kujengwa au kuwa chini ya kiwango.

Kwa upande mwingine waziri huyo amewataka wataalamu hao kupanua wigo wa majukumu yao nakuanza kukagua miradi ya barabara katika halmashauri za majiji, manispaa na wilaya na kutoa taarifa serikalini kwa lengo la kuhakikisha kuwa miradi hiyo ina thamani ya fedha kama ilivyokusudiwa.

TOTO 2 SIMBA 2

Kikosi cha Toto Africans kilichoshuka dimbani leo kuchuana na Simba kwenye dimba la CCM Kirumba mchezo uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Zaidi sikiliza taarifa ya Sports Xtra kwa kubofya play.
Ni mchuano...


Mtafutano...


Mbinu za ziada zimetumika...


Kocha wa Simba 


Kocha wa Toto

Mashabiki wa Simba.


Mashabiki wa Toto.

Ulinzi mwanzo mwisho.

Friday, March 29, 2013

MCHEZO BAINA YA TOTO NA SIMBA MASHABIKI WAPANIANA

Shabiki wa Toto Africans na uchokozi wake.

Hapa kunamchanganyiko wa mashabiki wa Simba utawajua (nyekundu imehusishwa kwenye jezi zao) na shabiki wa Toto utamwona (jezi nyeusi na rangi fulani hivi...) Majibu jumamosi hii.

Kocha wa Simba akiwanoa wachezaji wake kwa mazoezi ya mwisho mwisho dimbani CCM Kirumba ambapo kesho (jumamosi) timu hizo zitashuka dimbani kumenyana.

Wachezaji wa Simba mazoezini dimba la CCM Kirumba Mwanza.

PAMBANO lililokuwa likisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa kanda ya ziwa kati ya timu hasimu Toto Afrika ya jijini Mwanza na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Vodacom Simba linatarajiwa kupigwa kesho jumamosi katika uwanja wa CCM Kirumba huku mashabiki wa kila timu wakijinasibu kushinda.

Simba SC ambao walipoteza mechi yao iliyopita mjini Bukoba baada ya kuchapwa bao 1-0 na timu ya Kagera Sugar wanaingia katika uwanja wa CCM Kirumba kesho huku wakiwa na kumbukumbu ya kuchapwa na Toto katika mechi ya kwanza katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kwa bao 1-0.

Kujua kilichojiri Sikiliza Taarifa ifuatayo:-

Hii ni big mechi, nyasi hizi zitawaka moto.

Katibu wa Chama Cha soka mkoa wa Mwanza Nasibu Mabrouk amevitaja viingilio  katika mchezo huo kuwa Jukwaa kuu ni shilingi 10,000/=, na shilingi 3,000/= mzunguko.
Kocha mkuu wa Simba akitoa maelezo kwa Ngasa kwenye mazoezi dimbani CCM Kirumba.

Zoezi la kutawala eneo la 18.
Mmoja kati ya makocha wa Simba Jamhuri Kiwelu akizungumza na waandishi wa habari.



"Tuacheni tutete wawili tu!"

Mashabiki wa Simba walimzonga kocha msaidizi Julio wakitaka kujua nini hatma ya timu yao mara baada ya kuonekana kusuasua katika ligi ikiwa nipamoja na kichapo mkoani Kagera. Hata hivyo julio alionekana kujibu kwa ufundi maswali yao. 

STORY...


MWANDISHI: NEEMA JOSEPH

Ukweli utabaki palepale  kwamba afya bora ni muhimu  kwa binadamu kuliko kitu  kingine chochote hapa duniani. Siku zote binadamu anapo ishi duniani kila kukicha anategemea  awe mzima ndipo atakapoendelea na  shuguli zake kwa sababu mtu hawezi kupanga mipango ya kesho kama mwilini  kwake  kuna maradhi.

Ilikuwa ni jioni   ambapo nilipiga  kambi  katika nyumba ya  Cosmas   Bonifance, mzee  ambaye   anaishi  na wake wawili  na kwa  wakati  huo alikuwa  kwa bi  mkubwa  akiwa  ameenda  kiumtembelea na kumpelekea matumzi .

hapo  ndipo  mzee  huyo alipoanza mazungumzo name kwa kuniambia  ushiriki wake  kikamilifu  katika  huduma  ya  ushiriki wa  uzazi  wa afya   kwa  familia  yake  yenye  wake wawili, kwa ujumla  mzee Cosmas amekiri   kushiriki  kikamilifu  kwenye  huduma ya  uzazi wa afya  baada  ya  kupata  elimu  na kuhudhuria  semina  mbalimbali tofauti  na hapo  awali.
Kwa sasa  anakwenda  kliniki  na mkeo  na kushiriki  hatua  zote  za  tangu  mwenza wake  anapoanza  kuhudhuria  kliniki  hadi  anapojifungua  ikiwa na pamoja na kupima  vipimo  vinavyohitajika wakati mama  akiwa mjamzito.

“Kabla  ya  kupewa  elimu  ya ushiriki  wa huduma  ya uzazi   ya   afya    mke  wangu  hakuthubutu  kuniambia  juu  ya  ushiriki  wangu  wakati wa ujauzito wake  na hata  mila  na desturi za kabila  letu  la wasukuma  hazikuruhusu  mwanaume  kushirikishwa  kwenye  afya  ya  uzazi” alisema   bwana  Cosmas.

Kwa hivi  sasa bwana  Cosmas  anaishi na wake zake wawili   na amekuwa akishiriki vyema  katika huduma ya  afya  ya uzazi  kwa wote  licha ya mke wake  mkubwa   aliyemtaja  kwa jina la  luncy  Magesa kutokuwa na  mtoto  kutokana  na kila anaposhika  mimba, mimba uharibika lakini  yeye amekuwa mshiriki wa karibu  katika  kufahamu  chanzo cha  tatizo  hilo.

 Sheria ya masuala ya uzazi na ushiriki wa   mwanaume  inasisitiza   mwanaume  kushiriki katika    huduma  ya  afya  ya   uzazi  kikamlifu  lakini wanaume  wengi   hawaijui  sheria  hiyo  hali  inayosababisha  ugumu wa kuwaomba waajiri wao  ruksa  ya  kumsindikiza  mke/wake  kliniki  na   baadhi yao wanaoijua wansingizia  kuwa wananyimwa  ruksa  na waajiri wao kuwasindikiza wake zao.

Lengo  la  tano  la millennia  linasisitiza  kupunguza  vifo  vya  kinamama wajawazito  kwa  robo  tatu  ya   vifo  kati ya mwaka 1990  hadi  2015  sanjali  na  lengo  la  sita  la kukinga  maambukizi  ya virusi  vya  ukimwi, malaria  na magonjwa  mengineyo.
Sera  ya  afya   ya Tanzania  ya  mwaka 2003  iliyosainiwa na waziri wa afya  wakati  hulo Anna  Magreth  Abdallah  moja  ya  lengo  lake kati  ya  malengo  tisa  ni kupunguza  maradhi  kwa  wakina mama wajawazito  na watoto  na kuongeza  umri wa kuishi.

Takwimu za  shirika la chakula duniani (FAO) zinaonyesha kuwa  wanawake huzalisha asilimia 60 na 80 ya chakula chote katika nchi zinazoendelea.wanawake  wanatoa mchango mkubwa  kama wazalishaji wakuu wa chakula katika ngazi za familia hatua ambayo imeanza kutambuliwa na kudhaminiwa na vikao mbalimbali kitaifa na kimataifa.

Serikali kushirikiana na vyama visivyo vya kiserikali(NGOS) imefanya kazi  ya kuondoa vipengele vinavyo bagua sheria zinazotumika ambazo hazitoi haki  na uhuru wa wanawake ,Aidha, serikali imepitisha sheria kadha katika kutoa upendeleo  kwa mwanamke mfano”sexual offences special provision Act of 1998, land law Act of 1999, na village land Act1999.

Sheria ya kwanza itawalinda  wanawake, wasichana na watoto kutokana na kunyanyaswa  kijinsia na  kutendewa  matendo mabaya .katika maeneo mbali mbali, mathalani mkoa wa Arusha, familia nyingi uimara wake umewezeshwa  na wanawake, ambao  ndio walezi  na wenye kutafuta kipato kwaajili ya kutunza familia.

Ushiriki  wa  wanaume katika swala zima la  afya ya uzazi mkoa  wa  mwanza umeongezeka kwa  asilimia 24 kwa mwaka  2011 haya yamebainishwa na katibu mkuu wa  mkoa  hospitali ya seketure mwanza Bw,  Danni  temba.

Mara nyingi  wanawake  wamekuwa wahanga wa  tabia , mila,  na  desturi  zenye  athari  katika  afya  ya  uzazi  kama ukeketaji  kwa  wanawake, kudhalilishwa  kingono ,   unyanyasaji wa kijinsia, ukahaba,  kulazimishwa   kuolewa   a u  kuoa  mapema  na  utumiaji  wa  madawa  ya  kulevya.

Wanaume  waache  kuwanyanyapaa   wenza    wao,   ubepari,   mila,  na  desturi walizo nazo waziiache, afya ya mama mjamzito ni muhimu kuliko kitu kingine chochote  duniani, hinyo  wanaume wadhubutu   kwani     nia,  uwezo  na  nguvu  wanazo.

"NKABAAAA..HILI HAPA PAMBANO LA PASAKA"


COSMAS KIBUGA KUPANDA ULINGONI JUMAPILI

Bondia mwenye makeke mengi na asiyekubali kushindwa ulingoni na huwa tayari kupigana kavukavu Cosmas kibuga anategemea  anategemea kupanda ulingoni jumapili hii ya tarehe 31katika ukumbi wa Texas hall – Manzese, kuzipiga na bondia mkongwe Sweet kalulu katika pambano la kirafiki lakusherehekea  Pasaka. Akilizungumzia pambano hilo Miraji msusa ambae ni muandaaji wa mchezo huo alisema “burudani yetu ni kuangalia ngumi na kushangilia na najua ngumi nzuri zipo katika hawa mabondia wasio na majina na wenye upinzani mkali ,nikaonelea lazima katika sikukuu hii ya pasaka tusiiache ipite hivihivi bila kupata starehe yetu, kusubiri mpaka tarehe 7 april kwenye pambano kubwa la pale ccm mwinjuma-mwanayamala  ni mbali, Nikaafikiana na cosmas kibuga na sweet kalulu ambao ni wapinzani mitaani wamalizie kiu yao hiyo jumapili juu ya ulingo katika pambano la round sita.
Mabondia hao pamoja na wa utangulizi wanategemea kupima  kesho jumamosi saa nne asubui hapohapo katika ukumbi wa Texas hall-manzese

Thursday, March 28, 2013

LOWASSA MGENI RASMI JUMAPILI HII KATIKA PASAKA GOSPEL FESTIVAL JIJINI MWANZA

Waziri Mkuu Mstaafu ambaye ni Mbunge wa Monduli Mh. Edward Lowassa akiwa na Meneja wa COSU Entertainment Albert G. Sengo. 
Waziri Mkuu Mstaafu ambaye ni Mbunge wa jimbo la Monduli Mh. Edward Lowassa amethibitisha kuwa mgeni rasmi kwenye tamasha kubwa la muziki wa Injili lijulikanalo kama Pasaka Gospel Festival litakalo fanyika pasaka hii tarehe 31 march 2013, na kujumuisha waimbaji mbalimbali kutoka mikoa tofauti hapa nchini ikiwa ni pamoja na kwaya zaidi ya 15 za jijini Mwanza.
Mkurugenzi wa COSU Entertainment Phabian Fanuel (kushoto) akifafanua jambo ndani ya studio za Afya Radio kuhusu tamasha la Pasaka Gospel Festival litakalofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza tarehe 31/march 2013 ambapo mgeni rasmi anatazamiwa kuwa Waziri  Mkuu Mstaafu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli Mh. Edward Lowassa.  Kulia ni mtangazaji wa Xtra Vaganza Mr. Credit.

Si wageni hao tu bali atakuwepo pia Meya wa jiji la Mwanza Mh. Stanslaus Mabula na wengine wengi waalikwa, hivyo wakazi wa Mwanza watashuhudia burudani ililoandaliwa kwa ubunifu wa hali ya juu ikishirikisha waimbaji wakubwa kama Enock Jonas (ZUNGUKA), na Neema Mwaipopo (RAHA JIPE MWENYEWE).

Wengine ni Nesta Sanga (JIANDAENI), Danni Safari, John Shahban, Jeska Julius, Isaya Msangi (SHETANI IMEKULA KWAKO), Danny Sanga kutoka Iringa, Tumaini Mbembela  kutoka Mbeya na mkoa wa Arusha utawakilishwa na Neema Munisi.

Kwaya za mkoa wa Mwanza ni nyingi za kutosha Anglican Vijana kwaya, EAGT City Centre kiufupi kwa zote zitaweka kambi kwenye shughuli yetu ya Uzinduzi Pasaka hii.

Jumatatu ya pasaka tutakuwa Geita uwanja wa CCM Katoro
Kiingilio kwa maeneo yote kitakuwa ni shilingi. 2000/= tu
Hivyo tunawakaribisha wote kwenye uzinduzi huo.

Mkurugenzi wa COSU Entertainment Phabian Fanuel amesema kuwa hii imekuwa ni bahati ya kipekee kuweza kuweza kufikia hatua hii na ugeni huo mzito kwani maandalizi yote yamekwisha kamilika kwa asilimia 97 jambo la kumshukuru Mungu.


Kulia ni mtangazaji wa Xtra Vaganza Mr. Credit na kushoto anaonekana Dj. Sande.
Njooni tuzunguke kwani wema wa Mungu umetuzunguka. 


Ili ufanikiwe tizama na sikiliza wimbo huu 'UFANIKIWE'

KUPITIA JAHAZI SALAMU ZA MKUU WA MKOA WA MWANZA INJINIA NDIKILO ZASIKIKA

Sikiliza hapa salamu za mkuu wa mkoa wa Mwanza.

CLOUDS CREW YATEMBELEA STUDIO ZA ONE LOVE FX

Kutoka kushoto ni Mr. Hypa ambaye ni producer wa video ndani ya Studio za One Love FX, mtangazaji wa Passion Fm  Philbert Kabago, Sebastian Maganga ambaye ni Production Manager wa Clouds Fm, Dj Fetty, Joff Leah, producer wa audio na video ndani ya studio hizo TIDDY Hotter na Director Shahib, pindi Radio ya watu ilipo fanya ziara fupi kwenye studio hizo wilayani Ilemela jijini Mwanza.

Mara baada ya kuwasili kwenye himaya ya studi hizo, Clouds Crew ilitembezwa kila kitengo kujionea shughuli zinavyofanywa na wadau hawa waliowekeza kanda ya ziwa.

Producer wa audio na video ndani ya studio za One Love FX  TIDDY Hotter (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Clouds Crew pindi ilipofanya ziara kwenye himaya hiyo.

Production manager wa Clouds Fm Sebastian Maganga akifurahia jambo na wadau kwenye moja ya kazi zilizofanywa chini ya One Love FX  Studio Mwanza... elekeza jicho lako Clouds Tv kujionea sambamba na kuisikiliza 'redio ya watu' makubwa yaja mwanawane.

Hapa macho na masikio yote yalielekezwa kwa Director Shahib aliyekuwa akifafanua jambo.

Hypa na one mic.

Prizenta wa Sports Xtra Joff Leah na one mic.

Sasa ni wakati wa tathinini.....

Li-picha la pamoko.

MATAMASHA YA AIRTEL YATOSHA KUFANYIKA NCHI NZIMA


Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akiongea wakati akitangaza wa Airtel wa kufanya Matamasha ya Airtel Yatosha katika mikoa mbalimbali ya Tanzania yenye lengo lan kutoa burudani sambamba na kuelimisha Jamii na wateja  wake kuhusu huduma za Airtel ikiwemo kuitambulisha huduma mpya ya Airtel Yatosha. Kulia Meneja Mauzo Airtel  Kanda ya Pwani  Raphael Daudi

Kiongozi wa Tip Top connection Bwana Madee  moja ya kikundi kitakachotumbuiza katika Matamasha ya Airtel Yatosha akiongea wakati wa uzinduzi wa Matamasha hayo yaliyofanyika katika ofisi za Airtel morocco, Matamasha haya yatawashirikisha wasanii wengine wakiwemo Fid Q,   Juma Nature,   Ney wa Mitego  na Stamina.Kulia Meneja Mauzo Airtel  Kanda ya Pwani  Raphael Daudi

Matamasha ya Airtel Yatosha  kufanyika Nchi Nzima
·         Tamasha la kwanza litafanyika Morogoro siku ya Jumapili na Jumatatu
·         Zaidi ya mikoa 6 kupata burudani kutoka kwa Wasanii wa kizazi kipya nchini
Airtel Tanzania leo imetangaza mpango wake wa kufanya matamasha ya Airtel Yatosha yenye lengo la kutoa burudani na kuwaelimisha jamii na wateja wake  juu ya huduma mbalimbali zinazotolewa na Airtel ikiwemo huduma mpya Airtel Yatosha inayomuwezesha mteja kupiga simu kwenda mtandao wowote kwa gharama nafuu zaidi.
Akiongea wakati wa kutambulisha matamasha hayo, meneja uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando alisema “Airtel tumeamua kutoa burudani wakati wa msimu huu wa sikukuu ikiwa ni pamoja na kuitambulisha huduma yetu ya Airtel yatosha kwa watanzania,  tunaamini kwa kupitia matamasha yatakayofanyika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania wateja wetu na watanzania kwa ujumla watapata burudani na kupata nafasi ya kupata elimu juu ya huduma zetu Nyingi
“Safari yetu ya burudani za Airtel yatosha itaanza katika Mkoa wa Morogoro katika siku ya  Jumapili na Jumatatu ya Tarehe 31/3 na 01/04/2013,  Kuanzia Saa Tatu kamili Asubuhi mpaka saa Kumi na Mbili Jioni, pale katika viwanja vya Sabasaba.

Tutakuwa na wasanii mbalimbali wakiwemo Fid Q,   Juma Nature,   Ney wa Mitego  na    Tip Top Connection. Kiingilio ni BURE , tunapenda kukukualika wewe na washikaji zako wote kuhudhuria katika tamasha hili la kwanza kabisa pale morogoro na utape burudani kabambe. Njoo na Kitambulisho chako ili uunganishwe na ufurahie ofa nyingi toka Airtel” aliongeza Mmbando

Naye kiongozi wa Tip Top connection Bwana Madee  alisema” kama kawaida tumejipanga kuwapa wateja wa Airtel na watanzania burudani ya Ukweli katika mikoa mbalimbali ya Tanzania, tunaomba watanzania wajitokeze kwa wingi katika matamasha haya ya Airtel Yatosha. Mbali na sisi kutoa burudani itakuwa nafasi pia kwetu kuona vipaji mbalimbali vya mashabiki wetu ambao ndio wasanii nyota wa kesho hivyo tuwapa hamasa ya kujitokeza kwa wingi ili tuweze kuburudika pamoja.

Wasanii watakaoshiriki katika Matamasha maalumu ya Airtel yatosha watatumbuiza kwa vibao vyao mahiri kama vile Fid Q na kibao chake cha Sihitaji Marafiki na  Ney wa Mitego na kibao chake cha Nasema Nao huku Tip Top Connection wakiwakilisha na kibao chao cha Nani kamwaga pombe yangu
Airtel hivi karibuni imezindua huduma ya Airtel Yatosha inayomuwezesha  mtumiaji wa mtandao wa Airtel kupiga simu kwenda mitandao yote kwa gharama ya chini kabisa na hivyo kutokuwa na haja tena ya kubadilisha kadi ya simu pindi anapohitaji kuongea na mtu wa mtandao mwingine.  Mteja anajiunga kwenye huduma hii kwa kupiga *149*99# 



BIG RIGHT YAWEKA MIKAKATI YA UBINGWA


Big Right YAWEKA MIKAKATI YA UBINGWA

Kampuni  changa ya Bigright Promotion inaanzisha mkakati wa kuwapiganisha mabondia  kwa ajili ya kugombania mikanda au kutetea mikanda yao isipotee.
Ibrahim kamwe kiongozi wa kampuni hiyo alisema ” Tutaanzia kwa kuandaa ubingwa wa mapambano ya uzito mdogo kabisa yaani light fly weight,baadae tunawaandalia fly weight na super fly  ,bantam …. .. ..mpaka heavy weight.
Hiyo itawasaidia mabondia kupata mapambano ya mara kwa mara na kuwapatia kipato kidogo kwa ajira walioichagua inayoambatana na utambulishaji wa kimataifa kwa nchi yetu, kwani mchezo wa ngumi ni mchezo  mmojawapo unaoutangaza na kuipeperusha vema bendera ya nchi yetu kimataifa.
Bila ya watanzania wengi kulifahamu hilo, hivyo kukosa usaidizi mzuri toka serikalini na taasisi binafsi tofauti na baadhi ya nchi za wenzetu zinazopenda na kuithamini michezo, Nchi nyingi zinatangazika  kupitia michezo hadi sisi tunazifahamu na kuzitembelea  au kuwa na shauku ya kutaka kuzitembelea, wakati uwezo huo wa kufanya vizuri  tunao lakini hatusaidiwi kujinyanyua wala kuwa na sehemu ya kueleweka kwamba hii ni kwa ajili ya ngumi (ulingo wa kisasa na ukumbi wa uhakika), na wakati wadau wa mchezo huu tunanung`unika na kuhaha kutafuta wadhamini  nasi tujikwamue tokakatika hali tuliyonayo, kuna wengine wasio wastaarabu watataka kuchukua nafasi hii kufanya ubadhilifu dhidi ya wanaosaidia-hii sio njema  na inadumaza michezo.
Kwa mfano mashindano yaliyo andaliwa na bigright tarehe 7 april mwananyamala hayana udhamini wala ufadhili wowote hivyo yanaendeshwa katika hali ya ugumu ili vijana nao wapate kucheza kuliko kufanya mazoezi ya muda mrefu bila mashindano hivyo kuwasababisha baadhi ya mabondia kukata tamaa na kuacha ngumi au kijiingiza katika vitendo vya ukabaji jambo ambalo sio jema na laweza kuepukika kwa kuwaandalia mashindano kama haya.
Ili azma yetu ya kuyafanya michezo iendelee yatubidi tushirikiane kwa kushawishi wafadhili, wadhamini au wapenda mchezo wenye uwezo watuwezeshe japo kidogo walichonacho ili nasi tuongeze nguvu ya kupigania michezo isidorole,  mipango ikienda kama tulivyopanga tunategemea kila mwezi kuwashindanisha kugombania ubingwa na kila mwezi wa 12 kunakuwa na ligi ya mabingwa na kumzawadia mshindi  kitu ambacho atakuwa anakikumbuka katika maisha yake.
Hivyo  kwa alie tayari na mwenye mapenzi na maendeleo ya michezo tunaomba mchango wako uwe wa vifaa kama gloves, bandages, ballguard, headguard, gumshield, chakula ,nauli, ulingo na mengineyo mengi tu sijayaorodhesha,msitutenge na uwezo wetu mdogo tusaidiane
 
IBRAHIM ABBAS KAMWE
+255 713501991 ,+255 784501991 , +255 767501991

SIMBA YALEWA CHAKARI MIWA YA KAGERA.

"Simba sc imefungwa kihalali kabisa sidhani kam tutapata walau nafasi ya 4, kwani timu inacheza chini ya kiwango  hakuna sababu ya kutokuwepo Mwinyi,  Sunzu, Bobani, Nyoso na haya yote kayasabisha huyu kocha wetu wa sasa si lolote si chochote,  hongera Kagera Sugar" Asema Muddy Mtabora Rais wa klub ya  Channel Afrika (pichani akinunua t-shirt)
Hadi mwisho wa mchezo Kagera 1 Simba 0.



Wednesday, March 27, 2013

WEMA WA WEMA SEPETU HADI VIKATUNI VYAUNENA

Ni katuni (kibonzo) toka gazeti la HABARI LEO JUMATANO MARCH 27, 2013

Tuesday, March 26, 2013

BAADA YA KUIKUNG'UTA MOROCCO TANZANIA YANG'ARA KWENYE KURASA ZA MAGAZETI NCHINI ITALIA.



Mdau wangu toka Facebook anaandika
#Sports NEWS: MARCH 26: Baada ya TAIFA STARS kuwafunga MOROCCO juzi jumla ya magoli 3-1 leo hii imekuwa gumzo katika vyombo mbali mbali vya habari ikiwemo Magazeti ya hapa nchini ITALY. Na moja ya Gazeti lililotoa taarifa ya TAIFA STARS kufanya vizuri ni hili hapa chini na nimaarufu sana nchini ITALY kwa utoaji wa habari za Michezo. Gazeti hili linaitwa LA GAZZETTA DELLO SPORT. Tazama ushahidi wa picha ya wachezaji wa TANZANIA (TAIFA STARS) wakishangilia ushindi baada ya kutupia bao la 3. 

Kiukweli wamezungumza mengi sana na na mojawapo ya mambo waliozungumzia ni kukua kwa Socer letu la Tanzania kwa ushindi huu mkubwa tulioupata nyumbani na pia wameupongeza uwanja wetu kuwa niwakimataifa kwa uzuri wake pamoja na uwezo mkubwa wa kubeba watu zaidi ya Elfu 50. 
Big up  Tanzania tupe raha ili magazeti yazidi kutunadi #
CEO wa G Sengo Blog na Mbwana Samatta.

QUALIFICAZIONI AI MONDIALI 2014 - AFRICACLASSIFICHE E RISULTATI


GRUPPO C
COSTA D'AVORIO-GAMBIA 3-0 [49' rig. Wilfried, 59' Y.Tourè, 70' S.Kalou] - Tutto facile per gli 'elefanti', che liquidano con un secco tris la pratica Gambia. Apre le marcature un calcio di rigore di Wilfried a inizio secondo tempo, raddoppio del 'citizen' Yaya Tourè e terza rete di Salomon Kalou che mette in cassaforte la vittoria.

TANZANIA-MAROCCO 3-1 [46' Ulimwengu (T), 67' Samata (T), 80' Samata (T), 90' El Arabi (M)] - Vittoria a sorpresa per la Tanzania che, battendo il più quotato Marocco, si conferma al secondo posto del Gruppo C a -1 dalla Costa d'Avorio. Gara senza storia con Ulimwengu e doppio Samata che hanno chiuso in anticipo la pratica. Inutile nel finale il goal della bandiera di un Marocco in dieci segnato da El Arabi.