ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 16, 2013

JIJI LA MWANZA KUSAINI UPYA HATI YA URAFIKI NA JIJI LA HUSBERG


 Ujumbe wa watu watano ukiongozwa na Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula hivi karibuni ulifanya ziara katika jiji rafiki na Mwanza la Augsburg nchini Ujerumani.

Ziara hiyo ilikuwa na mafanikio makubwa baada ya jiji hilo rafiki na jiji la Mwanza kusaidia vifaa vya utendaji kazi pamoja na mitambo ya kuboresha miundombinu kwa ajili ya shughuli za usafi wa jiji la Mwanza.
Katika ziara hiyo jiji hilo la Augsburg ambalo ndani ya kipindi cha mwezi wa April litakwenda kuadhimisha miaka yake 50 tangu lilipotunukiwa hadhi ya kuwa jiji, liliweza kuahidi ujumbe wa jiji la Mwanza, kuendeleza mahusiano kwa kusaini upya hati ya urafiki wa majiji siku ya kilele cha maadhimisho hayo mwezi April 2013.

Pamoja na kusaini hati mpya jiji hilo rafiki liliweza kutoa msaada kwa jiji la Mwanza wa magari mawili ya kisasa ya uzoaji taka pamoja na kompyuta 500,  kwa ajili ya kuboresha maktaba ya jiji na shule za Sekondari za jiji la Mwanza.

Jiji la Husberg limeahidi kugharamikia safari ya wajumbe watakao kwenda kuhudhuria sherehe hizo za kutimiza miaka 50,  ikiwemo shughuli ya kusaini mkataba mpya wa Urafiki, lakini pia jiji hilo litaendelea kusaidia jiji la Mwanza linalokuwa kwa kasi kimaendeleo ili kuboresha sekta mbalimbali za Afya, Miundombinu, Teknolojia,  Elimu  na Mawasiliano.

Wengine walikuwemo kwenye ziara hiyo ni pamoja na Mkurugenzi wa jiji la Mwanza Bw. Wilson Kabwe, Afisa Uhusiano wa jiji la Mwanza Bw. Joseph Mlinzi pamoja na Mweka hazina wa jiji la Mwanza Bw. Paulo Ntinika na Afisa mmoja wa Kitengo cha Tampere.

MICHEZO MWANZA YAPATA MWARUBAINI



Mkuu wa Mkoa wa mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo akisikiliza kwa makini Michango ya Wajumbe wa Kamati ya Michezo Mkoa walipokutana kujadili maendeleo.

Meneja wa TRA Mkoa wa Mwanza (kushoto) pamoja na Bw. Kizito Bahati Afisa Michezo wilaya ya Ilemela aliyemwakilisha Mkurugenzi wa wilaya hiyo wakiwa kwenye kikao hicho kilichofanyika ukumbi wa mikutano ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Mwenyekiti wa Chama cha soka mkoa wa Mwanza MZFA Bw. Jackson Songora ambaye ni mmoja kati ya wajumbe wa kamati hiyo akichangia hoja iliyowasilishwa mezani. 

Wajumbe wakitafakari kwa makini huku wakiainisha kwenye karatasi zao maoni yao namna ya kuinua michezo mkoa wa Mwanza.

 · Zachangwa Mil. 6 Papo kwa Papo

Na. Atley Kuni -Afisa Habari Mkoa wa Mwanza.

Kamati ya Michezo Iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,  imeazimia kuhakikisha inainua suala zima la Michezo katika Mkoa huo.
Wakitoa mawazo katika kikao kilicho itishwa na Mkuu wa Mkoa huo  walisema tatizo kubwa ambalo lipo katika Masuala ya Michezo ni pamoja na nidhamu ndogo ya michango kwa Viongozi wanao chaguliwa,

Walisema kukwama kwa michezo katika Mkoa nia tatizo la watu wanaochaguliwa kutokuwa na dhamira ya dhati katika kuendeleza michezo Mkoani hapa.

Akizungumza katika Kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo amesema, "kwakweli tufike mahali tumalize tatizo hili lakukwamisha suala la michezo katika Mkoa huu". Alisema haipendezi watu kugeuza uongozi kama sehemu ya Miradi yao badala yake tufanye kazi ambayo itakuwa na maslahi kwa wanamwanza wote.

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza bwana Hamisi Maulid alisema tatizo lililopo ni Umbwe la uongozi usio zingati maadili ya uongozi hivyo Umefika wakati sasa kamati kama hii inayo undwa kusimamia kwa dhati na ikiwezekana viongozi wanaochaguliwa wawe ni wale tu wenye dhamira ya dhati katika kuinua Michezo katika Mkoa huu, akitolea mfano alisema huko yeye alipotoka waliunnda kamati kama hiyo na usimamizi wa fedha ukaimarishwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Hata hivyo kamati hiyo ilitoka na Maazimio Manane yakwenda kuyafanyia kazi, Maazimio yaliofikiwa ni pamoja, kila halmashauri ya Wilaya kuchangia, Mil.10, Uchaguzi wa vilabu ambao bado haujafanyika ufanyike ikiwezekana hata kwakulazimishwa, Kamati ya Michezo ya Mkoa kuwa Mhimili Mkuu wa kusimamia masuala ya michezo, kufungua akaunti kwaajili ya kuhifadhi pesa itakayokuwa inapatikana, kutunga sheria ndogondogo kwaajili kukusanya sehemu ya kodi ya leseni kwaajili yakuendeleza michezo mkoani humo, Aidha kila mjumbe wa kamati hiyo amehimizwa kuwa chachu ya mabadiliko yakuhakikisha suala la Michezo katika Mkoa huo linarejea kama enzi za zamani.

Katika hatua nyingine kamati hiyo Imewachagua Bibi Doroth Mwanyika kuwa Mwenyeki wa Kamati hiyo, huku bwana Peter Ngongoseke akichaguliwa kuwa Makamu wa Mwenyekiti, huku nafasi ya Mtunza fedha ikienda kwa bwana Peter Shewio ambaye ni mfanya kazi wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA.

Kabla ya kikao hicho kumalizika wajumbe hao walikusanya kiasi cha Tshs 6,000,000 kwaajili yakuanziasha mfuko huo na wadau wengine waka ahidi kuendelea kuchangia mfuko huo.

 Kamati ya Michezo ya Mkoa wa Mwanza inaundwa na Mkuu wa Mkoa Mwenyewe kama Mlezi, Bibi Dorothy Mwanyika Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Mwenyekiti, Peter Ngongoseke Makamu wa Mwenyekiti,  wajumbe ni Ernest Mangu, Christopher Gachuma,Altaf Hilani, Nuru Suleiman, Jeremiah Lusana wajumbe, wengine ni Leonard Kadashi Mjumbe, L. Japhet,Wilson Kabwe,Zuberi Mbyana Jackson Songora, Gisiruri Mwihechi, Baraka Ezekiel, Njile Lili, Samwel Nyala wote wajumbe, taarifa hiyo Imeongeza kuwa wajumbe wengine ni James William, Lameck Airo, Joseph Kahungwa, Lazaro Ngweleja, na Hamis Salehe wote wajumbe.

Kwa mujibu wa historia Mkoa wa Mwanza uliwahi kuwika katika Michezo katika vipindi tofauti kati ya miaka ya sabibi na Themanini, lakini pia Mwanza ndio Mkoa pekee wenye chuo kikubwa kabisa cha Michezo cha Malya.

Friday, February 15, 2013

IBF YACHUKUA NAFASI YA KATIKATI BARANI AFRIKA

Msimamazi mkuu wa mpambano huu ni Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi aliyesimama katikati pichani na mabondia Gogita Gorgiladze (kushoto) na Ilunga Makabu (kulia)


Mabondia wanaotaraji kupambana katika mapambano mawili ya IBF yanayofanyika katika majiji ya Johannesburg na Tunis, leo wamekamilisha kupima uzito kabla ya kuingia ulingoni.

Mapambano haya yaliyopewa jina la “Barabara ya kutoka Cape Town mpaka Cairo kwa IBF” kutokana na majiji haya kukaa moja kusini na lingine kaskazini mwa Afrika, yanafanyika wakati IBF ikijipambanua vyema katika bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi.
 
Kusini mwa Afrika, leo imeshughudia mabaondia mawili wanaopambania ubingwa wa dunia kwa vijana walio chini ya miaka 25 wakipima uzito mbele ya mashirika mbalimbali ya habari ya ndani na nje ya Afrika ya Kusini.
 
Illunga Makabu kutoka Jamhuri ay Watu wa Kongo (DRC) alipima uzito kumkabili Gogota Gorgiladze wa Georgia. Upimaji huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa ulio katika hotel ya nyota tano ya Emperors Palace iliyoko katika jiji la Johannesburg!
 
Rodney Berman mtu anayeheshimika kwa kuwa promota wa kwanza kuandaa pambano la IBF la dunia katika bara la Afrika mwaka 1990, ndiye anayepromoti pambano hili!
 
Tayari wadau na mashabiki wa ngumi kutoka katika nchi mbalimbali za Afrika zikiwamo Namibia, Zambia, Msumbiji, Zimbabwe na Tanzania wameshawasili nchini Afrika ya Kusini tayari kuangalia mpambano huo. Wengine walibaki Afrika ya Kusini wakati wa mashindano ya kombe la Afrika yaliyomalizika wiki iliyopita.
 
 
Kaskazini mwa Afrika,
Bondia ambaye ameshajizolea sifa kemkem Ayoub Nefzi wa Tunisia anayeishi nchini Belgium atapigana na bondia Ishmael Tetteh kutoka nchi ya Ghana kugombea ubingwa wa Afrika, Ghuba ya Uajemi  na Mashariki ya Kati (IBF AMEPG) katika uzito wa Light Middle.
 
Mpambano huo uliopewa jina la “Uzuri wa Jasmine” kutokana na jina hilo kutumika katika mapinduzi yaliyomwondoa Rais wa zamani wa Tunisia Ben Ali unafanyika wakati Ayoub Nefzi akijiandaa kugombea mkanda wa juu wa IBF wa mabara mwezi wa tatu nchini Belgium.
 
Mabondia wote wawili wanatagemea kuonyesha moto mkali katika mpambano ambao tayari mashabiki wa ngumi kutoka katika nchi za Nigeria, Ghana, Libya, Misri, Algeria tayari wameshawasili nchini Tunisia kuangalia mpambano huo!
 
Tunisia inasifika kama nchi iliyowahi kutoa viongozi wengi wa mchezo wa ngumi katika bara la Afrika.
 
 
Imetolewa na:
 
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

SHUHUDIA MING'ARO YA PICHA ZA VALLENTINE VILLA PARK

Mmoja kati ya waimbaji wa kundi la Jahazi Morden Taarab akiwa juu ya stage la Villa Park kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa Usiku wa Mwambao sambamba na kusherehekea sikukuu ya wapendanao duniani.


Mwanadada aliyependeza usiku huo alizawadiwa mizawadi toka kinywaji cha Reds.


Flowerz mwingine huyu alizawadiwa full seti ya Reds huku kushoto kabisa Mc Magoma akimeneji vinavyojiri.


Best couples  zilizo shine nazo zilitoka na mizawadi kibao toka Reds.


You cant c' Me


Hivi ndivy Papaa alitokelezea na mkewe katika usiku wa wapendanao Villa Park Mwanza.


Kwa kunyakuwa nafasi ya tatu Papaa alipata zawadi toka home Shoping Centre. 


Hawa ni washindi wa pili kwa Couples zilizopendeza nao walipata zawadi ya kulala Hotel JB Belamounte. 


Mc Magoma akitambulisha washindi nafasi ya kwanza kwa Couple zilizotokelezea usiku wa Vallentine Villa Park.


Washindi wa kwanza niiiiiiii........


Mwaaaaaa....!!!!! Hawa ndiyo washindi wa kwanza, nao walijipatia tiketi kwenda na kurudi dar kwa siku wanayotaka toka Precision Air.

Ni Mc Magoma (kushoto) na Dj John Lyatou (kulia) na nyuma yao Jahazi Morden Taarab. 

Hapa kila mmoja aliondoka na zawadi katika usiku wa wapendanao Villa Park  ukiambatana na uzinduzi wa Usiku wa Mwambao mara baada ya ukarabati mkubwa kufanyika


Hivi ndivyo rangi za hapa zilivyo someka toka dansing floo..


Guitalist.....


Ze eria...at Villa.


Live toka stejini.
We...

Mwanza nzima ilihamia hapa.

Thursday, February 14, 2013

WEZI WATATU WA ATM WAKAMATWA MWANZA

JESHI la Polisi mkoani Mwanza kwa kusaidiana na maofisa wa Benki ya NMB imewatia mbaroni watu watatu ambao wanadaiwa kuiba kiasi cha Sh700 milioni kwa nyakati tofauti.


 Watuhumiwa hao wamenaswa baada ya kuwekewa mtego na maofisa wa benki na polisi kwenye saa 6.00 usiku wa Februari 10, mwaka huu na mtuhumiwa mmoja alibambwa akichukua fedha katika ATM ya NMB kwenye Tawi la PPF Plaza Mwanza.

Baada ya kunaswa kwa mtuhumiwa huyo, alisaidia kuwaelekeza polisi walipo wenzake, ambao walikutwa katika hoteli moja jijini Mwanza wakiwa wamejipumzisha.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mwanza, Christopher Fuime alisema pia walikamata vifaa mbalimbali ambavyo walikuwa wakitumia kwa ajili ya kufanyia uhalifu huo.

Vifaa walivyokamatwa navyo
Vifaa vilivyokamatwa navyo ni kadi za bandia 194 za kuchukulia fedha katika ATM za Benki ya NMB, ambapo kati yake kadi 95 zilikuwa na namba 0225152975 zinazotumia namba ya akaunti ya 2258103695 zenye jina na picha ya mtu anayedaiwa kuwa ni mtumiaji mwenye jina la Molely L. P. Kadi nyingine 99 zilikuwa na namba 0506056317 za akaunti namba 5068000322 zikitumia jina moja la Mnuo Z. E na picha moja.
Mbali na kadi hizo pia waliweza kunasa kadi 36 za Benki za DTB, ambazo kati yake kadi 18 zilikuwa na jina moja la Kelvin G. Gratias na namba 20497883, kadi 12 zikitumia jina la John J. Paul zenye akaunti namba 2049783 huku kadi sita zikitumia jina moja la Joseph Donald akaunti namba 2049783.

Kadi nyingine tatu zenye maandishi ya Download List na nyingine ikiwa ni kadi ya Visa ya Benki ya KCB yenye namba 4183546040003827 zikitumia jina la Elikana Zacharia. Kadi nyingine zilikuwa ni tupu zisizo na maandishi wala nembo ya benki yoyote na nyingine zikiwa ni Soviet Royalty, kadi ya raia ya Urusi ikiwa na namba 000724.

Pia walikutwa na kadi ya Benki ya Amerikani yenye namba 549012345678 zilizokuwa zikitumia jina la Richard Croswell.

Walikamatwa pia wakiwa na vifaa mbalimbali vya kielektroniki ikiwamo kamera za siri tatu za kienyeji ambazo zimetengenezwa kwa kufungwa betri za simu ya mkononi na pia walikamatwa na kifaa cha kutengenezea kadi bandia (Magnetic Card reader), mikebe mitatu ya rangi za kupulizia kamera za usalama katika ATM ili wasionekane wakati wa wizi wao, ‘printer’ pamoja na kifaa cha kuchomea vifaa vya umeme.

Wizi ulivyofanyika
Wahalifu hufika katika mashine za kutolea fedha ambapo hatua ya kwanza ni kuzima kamera za usalama za eneo husika kwa kuzipulizia rangi maalumu ili kuzitia ukungu hivyo kuharibu mwonekano wake na kuruhusu wao kuingia eneo hilo bila ya kuonekana na kufanya wizi wao.
Mara baada ya kuziharibu kamera za usalama, walikuwa wakianza kwa kuweka kamera zao za siri ili kunasa namba za siri za kufungulia akaunti ambazo huzisoma katika ‘kompyuta’ na kuzinakili katika daftari lao maalumu na kisha kuchukua kadi zao bandia na kuchukua fedha.

Wizi huo wa kuchukua fedha waliufanya nyakati za usiku saa sita hadi saa tisa usiku wakati ule wa kutegea kamera zao ulifanyika muda ambao huwa na wateja wengi hasa siku za mapumziko. 

TOTO YALAZIMISHWA SARE NYUMBANI.

Goli la kwanza la Toto Africans.
Toto ndiyo walianza kufungua pazia la magoli kwenye dakika ya 52 kipindi cha pili mfungaji akiwa Mohamed Jingo kufuatia timu yake kuzawadiwa penati mara baada ya mchezaji mmoja wa Polisi Morogoro kuunawa kwenye eneo la hatari.

Dakika tatu baadaye Polisi Morogoro walisawazisha kupitia mpira wa faulo iliyopigwa na kuwababatiza mabeki wa timu ya Toto hatimaye ukamkuta kwenye nafasi nzuri mfungaji Keneth Masumbuko kuweza kuzifumania nyavu.

Toto walitulia na kuweza kujipatia bao la pili kwenye dakika ya 60 baada ya krosi safi ya Emma Swita kukifikia kichwa cha mfungaji James Magafu aliyeutupia mpira engo ya kushoto mwa lango la Polisi Morogoro.

Uzembe wa  kipa wa Toto Africans Erick Ngwengwe aliyeponyokwa na mpira aliokuwa na uwezo wa kuudaka wa shuti la Niko Kabipe uliigharimu timu hiyo kutoa mwanya kwa Polisi kupata bao la pili la kusawazisha kwenye dakika ya 65 ya mchezo.

Hadi mwisho wa mchezo ndani ya dimba la CCM Kirumba  Toto 2 Polisi Moro 2.
 Kocha wa timu ya Polisi Morogoro Richard Adolf akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mchezo.. Kumsikiliza bofya play.
 Mashabiki walivamia benchi la wachezaji wa timu ya Toto baada ya kumalizika kwa mchezo kati yake na Polisi  Moro na hapa kiwalaumu wachezaji kucheza chini ya kiwango na kutoka sare kwenye mchezo huo... kusikiliza bofya play.
 Hapa lilitoka 'buku' tu'''' mwanawane...
Kepteni wa timu ya Toto Africans Hamisi Msafiri akipokea fedha zilizochangwa kwa style ya papo kwa hapo na wadau wa soka kutoka kwa Mwandishi wa habari Philbert Kabago,  baada ya wachezaji hao kudai kuwa wako taabani katika kambi yao likiwemo suala la kutolipwa mishahara na posho za michezo mbalimbali kwa zaidi ya miezi minne sasa kiasi cha kuwaathiri mikakati yao ya kupata matokeo mazuri.

Wednesday, February 13, 2013

BAADA YA MIAKA 13 YA HUDUMA SAMONA YAENDELEA KUTAKATISHA WAKAZI WA KANDA YA ZIWA.

Mtangazaji wa Passion Fm Philbert Kabago (kulia) akimkabidhi zawadi ya Epron Dickson Msenda aka Dizzo Man mkazi wa Luchelele, mara baada ya kushinda kupitia maswali yaliyokuwa yakiulizwa redioni ndani ya kipindi cha Michano Time kuhusu bidhaa za Samona. 

Mtangazaji wa Passion Fm Philbert Kabago (kulia) akimkabidhi zawadi ya T-shirt  Mr. Cleva Man ambaye ni fundi ujenzi kutoka Mayanja Camp Mkudi mwanza anayetumia mafuta ya Samona kulainisha ngozi na mikono yake mara baada ya kazi.

Hii ni promosheni ya bidhaa za Samona zinazosambazwa na Lakairo Investiment Co. LTD iliyofanyika viwanja vya mnada  wa Kiloleli Mwanza.

Wanafunzi nao ni sehemu ya jamii watumiaji wa mafuta na sabuni ya Samona nao wamefurika eneo hili kushuhudia promosheni hii.

Kujitosa kulikuwepo na hapa bidada akijituma jukwaani kuonyesha maufundi katika kucheza muziki wa Ragga....



Wananchi waliojitokeza kushuhudia promosheni eneo la Kiloleli .

Ni wakati wa zawadi kwa aliyeonyesha maufundi...na hapa alikuwa akipewa  zawadi moja baada ya nyingine.

MKUTANO WA TATU WA WADAU WA NSSF WAANZA RASMI LEO JIJINI ARUSHA

Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Gaudencia Kabaka akizungumza na kuzindua wimbo maalum wa NSSF uliotungwa na Wasanii hapa nchini wajiitao All Stars,mbele ya wadau waliohudhuria mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.Kauli mbiu ya mkutano huo kwa mwaka huu ni Sekta ya hifadhi ya Jamii Tanzania,Njia panda-Nini kifanyike.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau akifafanua jambo kwa umakini  mbele ya  Wadau zaidi ya 1000 kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya Tanzania, kwenye mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) unaondelea hivi sasa kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha,ambapo kauli mbiu yake kwa mwaka huu ni Sekta ya hifadhi ya Jamii Tanzania,Njia panda-Nini kifanyike..
  
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crenscentius Magori akifafanua jambo mapema leo asubuhi wakati mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,ukiendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Meneja wa kanda na anaeshughulikia Idara mbalimbali za serikali kutoka NSSF,Rehema Chuma akifafanua namna ya uendeshaji wa shirika hilo kwa  wadau waliohudhuria mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe akichangia moja ya mada zilizokuwa sikitolewa kwenye mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Wakili Harold Sungusia akichangia moja ya mada zilizokuwa sikitolewa kwenye mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Mmoja wa wajumbe wa NSSF,Peter Sumbi aliyekuwa akifanya kazi shirika la Wildlife Fund akitoa ushuhuda wake,namna alivyopata ajali na kufanikiwa kupata fao lake la ajali kazini kutoka kwa shirika la NSSF na hatimaye kufaidi matunda kupitia mfuko huo.
Pichani ni Mwenyekiti wa wasataafu wa TAZARA,Injinia Mwl.Sango akitoa ushuhuda wake kuhusiana na namna shirika la NSSF lilivyowasaidia wastaafu wa shirika la TAZARA,kupitia mfuko wa pensheni na fao la kujitoa.

Sehemu ya Meza kuu ya mkutano huo.

Sehemu ya Wabunge waliopo kwenye mkutano huo.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Mifuko ya Jamii nchini wakiwa kwenye mkutano huo.

Baadhi ya watendaji wakuu wa NSSF wakiwa mkutanoni.

Meneja Mahusiano wa PPF,Lulu Mengele na  Meneja Mahusiano wa SSRA,Sarah Kibonde wakifuatilia yanayojiri ndani ya mkutano huo unaoendelea hivi sasa.
Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini (CHADEMA),Mh Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu akiwa sambamba na Mbunge wa Arumeru Mashariki,Mh Joshua Nasari (CHADEMA) na Wadau wengine wakifuatilia yanayojiri hivi sana kwenye mkutano wa NSSF.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali wakifuatilia yanayojiri ndani ya mkutano wa NSS unaoendelea hivi sana ndani ya ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Mbunge wa jimbo la Ludewa,Mkoani  Njombe,Mh. Deo Filikunjombe (CCM) akiwa na baadhi ya Wabunge Wenzake wanaohudhuria mkutano huo wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijiri ndani ya mkutano huo ambao umewakutanisha wadau zaidi ya 1000 kutoka sehemu mbalimbali jijini Arusha.
Mwenyekiti wa kikao cha awamu ya kwanza cha Mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Bwa.Daudi Msangi akitoa utaratibu kwa Wanachama na wadau mbalimbali waliohudhuria mkutano huo unaoendelea ,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha,kulia kwake ni  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau akizungumza jambo na  Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crenscentius Magori mapema leo asubuhi kabla ya kuanza kwa mkutano wa shirika hilo.
Wadau.

Wadau.

Mkutano ukiendelea.
  

Picha zote na Othman Michuzi