ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 9, 2013

TOTO YAAMBULIA SARE NYUMBANI.

Toto Africans Football Club.
Jahazi la timu ya Toto Africans ya jijini Mwanza limezidi kutoboka na kuwapa presha wakazi wa jiji la miamba kuhofia kukosa timu ya uwakilishi ligi kuu Tanzania bara kwa msimu ujao, mara baada ya matokea ya sare ya bila kufungana na timu ya Coastal Union katika mchezo uliochezwa leo ndani ya dimba la CCM Kirumba Mwanza.

Licha ya Coastal kuichachafya ngome ya Toto kwenye kipindi cha kwanza lakini hadi dakika 45 za kipindi hicho zinamalizika ubao ulisomeka 0-0.

Dakika 20 za mwisho kwa kipindi cha pili Toto walijaribu kubadilisha mchezo na kuwapa matumaini watizamaji wake wachache waliohudhuria mchezo huo kuwapa sapoti kwa kuumiliki mpira  na kulisakama lango la Coastal Union, lakini mashambulizi yao hayakuwa na manufaa yoyote kwa timu hiyo ambayo tangu kuanza kwa ungwe hii ya lala salama, tofauti na mchezo wa leo haikufanikiwa hata kuambulia pointi moja.

Ni ndani ya dakika hizo timu hiyo ilipaswa kujilaumu kwa kushindwa kuondoka kifua mbele.
Hatimaye hadi mwisho wa mchezo timu zote zilitoka uwanjani zikiwa na sare ya bila kufungana.

Friday, February 8, 2013

SHEREHE MAALUM YA WAPENDANAYO KWA AJILI YAKO NA MPENZI WAKO.


Mikono Media tunakukaribisha wewe na mpenzi wako ujumuike nasi Alhamis ijayo, tarehe 14 Mwezi huu, kusherehekea siku Maalum ya Wapendanao (Valentine's Day) kwenye ukumbi wa JB Belmont Hotel. Pata chakula cha usiku, muziki murua wa Live Band na mandhari nzuri kabisa kwa ajili yako wewe na mpenzi wako, bila kusahau ugeni maalum kutoka kwa Bw. Chris Mauki atakayetuelimisha zaidi kuhusu kujenga mahusiano imara ya kimapenzi. Kiingilio ni Tsh 100,000/= kwa mtu na mpenzi wake (couple) kuanzia saa 12 jioni.
Fanya booking mapema, piga simu namba 0717 109362.
Wahi sasa nafasi ni chache!

MASHAUZ CLASSIC YAENDELEA KUTAMBA KATIKA ANGA

Mwimbaji wa bendi ya Mashauzi Classic, Rukia Jumaa kulia akiimba wakati wa onesho lao lililofanyika katika bushati ya Magomeni Dar es salaam jana kushoto ni Mpiga gita la Solo wa bendi hiyo Jumanne Ulaya
 
Mwimbaji wa bendi ya Mashauz Classc, Rukia Jumaa akiimba wakati wa onesho la bendi hiyo.

Mwimbaji wa bendi ya Mashauz Classic, Hashimu Said 'Mzee wa Majanga' akiimba kwa isia wakati wa onesho la bendi hiyo lililofanyika katika bustani ya Magomeni Dar es salaam jana nyimbo anayoimba ni tukio la kweli lililomtokea na kumfanya atunge nyimbo inayokwenda kwa jina la 'Mimi Mwanaume Bonge la Bwana' baada ya kuchomewa moto kila kitu cha ndani pamoja na nguo zake zote na mke wake wa ndoa.


Thursday, February 7, 2013

LICHA YA SHESHE LA MOTO MV. VICTORIA YAFANYA SAFARI USIKU HUU

Mv Victoria ikijitayarisha kwaajiri ya kufanya safari yake usiku wa leo kuelekea mjini Bukoba mkoani Kagera mara baada ya kukaguliwa kufuatia kunusurika kuteketea mchana wa keo kupitia sakata la wachomeleaji walio sababisha moto uliozuka eneo la kuhifadhi mizigo.
Zaidi kujikumbusha sikiliza ripoti iliyofanyika ndani ya 'GUMZO' la Jahazi Clouds Fm, 
Kwa ku Bofya Play.

Mv. Victoria ikipakia gari usiku huu hatimaye kuanza safari yake usiku huu.


Nao wasafiri walipanda kama ada licha ya baadhi yao kuonekana kuwa na wasiwasi na wengine kuahirisha kabisa safari.


Ndani ya meli abiria wakitathimini mazingira.


Saa 3 na dakika 10 meli ya Mv. Victoria inaondoka Mwanza.... kuelekea Bukoba mkoani Kagera.
Blogu hii yawatakia safari njema abiria wote.

JK AZINDUA VITAMBULISHO VYA TAIFA LEO

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akibonyesha kitufe kuashiaria kuzindua rasmi mfumo wa usajili na utambuzi wa watu na utoaji wa vitambulisho vya taifa uliofnyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.Watatu kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bwana Mwaimu na kulia nia Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bwan Said Meck Sadik.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akibonyesha kitufe kuashiaria kuzindua rasmi mfumo wa usajili na utambuzi wa watu na utoaji wa vitambulisho vya taifa uliofnyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.Watatu kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bwana Mwaimu na kulia nia Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bwan Said Meck Sadik.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kitambukisho cha Taifa katika hafla ilkiyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi akimkabidhi mke wa Rais Mama Salma Kikwete kitambulisho chake cha Taifa katika viwanja vya Karimjee leo huku Rais Kikwete akishuhudia.Kushot o Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Bwana Mwaimu
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kitambulisho chake cha taifa katika viwanja vya Karimjee leo.

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume kitambulisho chake cha taifa katika viwanja vya Karimjee leo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa kitambulkisho cha taifa katika viwanja vya Karimjee leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad kitambilisho cha Taifa katika viwanja vya Karimjee leo wakati wa hafla ya Uzinduzi wa mfumo wa usajili na utambuzi wa watu.
Rais Kikwete akimkabidhi Kada wa CCM Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kitambulisho cha taifa.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Dkt. Alex Malasusa kiongozi wa kanisa la KKKT kitambulisho cha taifa.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Shekhe Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Alhaj Elihad kitambulkisho cha taifa.
 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  akimkabidhi Mwenyekiti wa CUF Professa Ibrahim Lipumba kitambukisho cha taifa.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt.Ramadhani Dau kitambulisho cha taifa leo katika viwanja vya Karimjee.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifurahi na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Bw.William Erio mara baada ya kupokea Kitambulisho cha Taifa

Baadhi ya wageni walioudhuria sherehe za uzinduzi wa Vitambulisho vya Taifa kutoka kushoto ni Kaimu Mhariri Mtendaji wa TSN Bw.Gabriel Nderumaki,Mkurugenzi Mkuu wa NSSF DKt.Ramadhani Dau,Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Bw.William Erio na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw.Emanuel Humba .Picha  na Freddy Maro  wa Ikulu.

BREAKING NEWS: MELI YA MV VICTORIA YANUSURIKA KUTEKETEA KWA MOTO.

MELI ya Mv Victoria inayomilikiwa na Kampuni ya huduma za Meli nchini (MSC) imenusurika kuteketea kwa moto uliozuka wakati mafundi wa kampuni hiyo wakichomelea eneo la shimo la kuhifadhia mizigo la mojawapo ya maeneo kwenye Meli hiyo.

Moto huo uliozuka katika meli hiyo ulizua tafrani kwa wakazi wa jiji la Mwanza na kufurika katika eneo la maegesho ya Meli za Kampuni ya MSC yaliyopo katika bandari ya Mwanza kaskazini majira ya saa 8 na dakika kadhaa na kusababisha msongamano mkubwa katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa taarifa zilizo naswa toka kwa wafanyakazi wa Meli hiyo ambao hawakutoa ushirikiano kuzungumza na waandishi wa habari, zilizonaswa wakati wakilaumiana zimeleeza kuwa mafundi wa kampuni hiyo walikuwa wakichomelea katika moja ya vyumba vya chini vya Meli hiyo ndipo cheche za moto zilipopenya na kuangukia katika sehemu ya pili ya kuhifadhia mizigo na kuanza kuwaka.

Sehemu hiyo ya mizigo kulikuwa kumehifadhiwa shehena ya magodoro pamoja na mito ya makochi tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenda mjini Bukoba Mkoani Kagera leo usiku.

Ni hali halisi ndani ya Sehemu hiyo ya mizigo kulikuwa kumehifadhiwa magodoro pamoja na mito ya makochi tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenda mjini Bukoba Mkoani Kagera leo usiku.

Maafisa wa kikosi hicho walijitosa kuhakikisha moto huo hausambai katika maeneo mengine ya Meli ya Mv Victoria ambapo walifanikiwa kuuzima huku ukiwa tayari umeteketeza magodoro yote pamoja na mito ya makochi iliyokuwa katika chumba cha kuhifadhia mizigo.

Hii ndiyo sehemu iliyokuwa na mafundi wa kampuni hiyo walikuwa wakichomelea ndipo cheche za moto zikapenya na kuangukia katika sehemu ya pili ya kuhifadhia mizigo na kuzua motomkubwa.

Juhudi zikiendelea kwa maafisa wa kikosi hicho kuhakikisha moto huo hausambai katika maeneo mengine ya Meli ya Mv Victoria.

Maafisa wa kikosi hicho hapa wamefanikiwa kuzama chini ghalani melini humo kunyunyiza maji zaidi kuhakikisha moto huo hausambai katika maeneo mengine ya Meli ya Mv Victoria.

Maafisa wa kikosi hicho hapa wamefanikiwa kuzama chini ghalani melini humo kunyunyiza maji zaidi kuhakikisha moto huo hausambai katika maeneo mengine ya Meli ya Mv Victoria.

Hata hivyo moto huo uliodumu kwa saa kadhaa ulifanikiwa kuzimwa ndipo juhudi za kuyatoa magodoro na mito yote ya makochi yaliyokuwemo ndani ya hifadhi ya mizigo ili kuhakiki uharibifu pamoja na kufanya tathimini kwa mali zilizo haribika.
Kwa umakini zaidi kuhakiki moto huo.
Wafanyakazi wa MSC wakitumia mashine maalumu ya kushushia mizigo ya kampuni hiyo wakitoa mabaki ya vitu vilivyounguzwa na moto.
Mtoto huo kama ungefanikiwa kuiteketeza meli ya Mv Victoria ingekuwa hasara kubwa sana kwa shirika la Marine Service kukosa chombo cha usafiri majini bandari za miji ya Mwanza, Kemondo na Bukoba, kwani  meli hii ndiyo meli pekee iliyosalia kwa safari hizo.

Ikumnbukwe kuwa Mv. Serengeti kwa sasa haiko shughulini na Mv. Bukoba ndiyo hivyo tena ilizama mwaka 1996 na mamia ya ndugu zetu.

Juhudi za ushushaji mizigo iliyoungua zikiendelea.



Ndani ya masaa mawili moto huo ulikuwa umedhibitiwa na kikosi cha zima moto na uokoaji waliowasili katika eneo hilo muda mchache baada ya moto kuanza wakitumia gari lenye namba za ausajili STK 1965 Mali ya Halmashauri ya jiji la Mwanza.
Mmliki wa magodoro pamoja na mito ya makocho iliyoteketea kwa moto aliyejitambulisha kwa jina moja la Ogunya amesema kuwa amepoteza magodoro 180 pamoja na mito 80 katika tukio hilo.


Kwa upande wake afisa mfawidhi wa Mamlaka ya usimamizi wa usafiri wa majini na nchi kavu(SUMATRA) kanda ya ziwa Josephat Loisimaye amesema kuwa uzembe wa viongozi wa MSC ndio ambao ulisababisha kutokea kwa moto huo.

Amesema kuwa viongozi wa MSC walipashwa kuchukua tahadhari mapema kabla ya kuanza uchomeleaji katika sehemu ya Meli hiyo na kueleza kuwa wanasubiri ripori ili waweze kuchukua hatua zaidi.

Hata hivyo Loismaye amesema kuwa Meli ya Mv Victoia iko salama na itaendelea na safari zake kwenda Bukoba leo usiku kwa kuwa moto huo haukuweza kuathiri mfumo wa injini ya Meli na kukipongeza kikosi cha zimamoto kutokana na kufika mapema na kuzima moto huo vinginevyo Meli hiyo ingeliteketea kwa moto na kusababisha hasara kubwa.

AIRTEL YAZINDUA PROMOSHENI YA PATA MUDA WA MAONGEZI MARA MBILI KUPITIA AIRTEL MONEY


cid:image002.jpg@01CE0514.E1FF41D0
Airtel yazindua promosheni ya pata Muda wa maongezi mara mbili kupitia Airtel money
·         Wateja kupata salio mara mbili kila anapotuma pesa kupitia Airtel Money
·         Ni kwa wateja wa malipo ya awali nchi nzima
kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua promosheni mpaya ya Airtel Money ambapo wateja wakel watapata muda wa maongezi mara mbili ya gharama watakazotozwa kwa kutuma  pesa na kupata wateja muda wa maongezi kulingana na ada ya makato pale wanapotoa pesa  kwa kupita huduma ya  Airtel money.

Akizungumza kuhusu promosheni hiyo, Meneja Uhusiano Jackson Mmbando alisema” Tumewawezesha wateja wetu kutumia huduma ya Airtel money na kufanya miamala mbalimbali ya pesa huku tukisogeza huduma za kifedha karibu na makazi na sehemu zao za  kazi , leo tunayofuraha kuwazawadia wateja  wetu waliojisajili nchini nzima muda wa maongezi mara mbili ya gharama watakazotozwa kutuma pesa kupitia Airtel money na pia tunawapa muda wa maongezi kulingana na ada watakayotozwa kutoa pesa pale watakapo toa pesa kupitia Airtel money. Bonus hii ya muda wa maongezi itatumika  kupiga simu Airtel kwenda Airtel siku nzima , kwa siku nzima hadi saa sita usiku.”

“Tunaendelea kuboresha huduma yetu ya Airtel money na kuendelea kutoa suluhisho la huduma za kifedha hasa katika maeneo yenye changamoto ya huduma za kibenki. kwa kupitia mtandao wetu mpana ulioenea zaidi tuna wawezesha watanzania nchni nzima hasa wa maeneo ya vijijini kupata huduma za fedha zilizo salama , nafuu na gharama nafuu kupitia Airtel Money.

Promosheni hii ya pata muda wa maongezi itaondoa Kampeni ya  bure,  na kuanzia sasa wateja wa Airtel watazawadia muda wa maongezi kila wanapotuma na kupokea pesa kupitia huduma ya Airtel Money”. Aliongeza Mmbando.

Airtel bado inaendelea kutoa huduma za mawasiliano za simu zenye ubora na gharama nafuu , kwa sasa wateja wa Airtel wa malipo ya Awali wanatuma ujumbe mfupi was ms kwa shilingi moja mara baada ya kutuma ujumbe mfupi wa kwanza kwa shilingi 125na kupiga simu kwa senti 10 mara baada ya dakika mbili za mwanzo.

ZAIDI YA MASIKIO YA WATANZANIA MILLIONI 40 NA WADAU WENGINE NCHI MBALIMBALI DUNIANI WAISUBIRI KWA HAMU AMLIFAYA YA LEO (ALHAMISI) KUSIKIA KAULI YA BABU, NINI HATMA YA KIKOMBE CHAKE.


Host wa kipindi cha Amplifaya akifanya mahojiano na Babu wa Loliondo Ambilikile, mpango mzima tutaupata leo (alhamisi) ambapo ile kiu ya maswali yote tuliyokuwa nayo inakwenda kupata tiba....ha-haaa ... tiba ya kikombe au...!!? Usiogope majibu ni leo, leo kuanzia saa moja usiku ndani ya Clouds fm.
Kwa sasa msikilize Babu wa Loliondo kwenye hiyo promo yake hapo chini.

MKURUGENZI WILAYA YA MAGU ABAINI MAPUNGUFU YA WATUMISHI IDARA YA FEDHA BARAZA LA MADIWANI LAMTAKA KUWACHUKULIA HATUA.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Magu Bi. Naomi Nnko (L) akitoa ufafanuzi juu ya masuala mbalimbali kikaoni.

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu limemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wake Naomi Nnko kuwachukulia hatua za kimaadili maafisa wake wa Idara ya Fedha wanaojihusisha na njama ya kuikosesha mapato Halmashauri hiyo kupitia vyanzo vyake vya mapato vilivyopo.

Hatua hiyo inafuatia kikao cha Baraza hilo kilichoketi jana Wilayani humo na baadhi ya Madiwani kuhoji chanzo cha mapato cha soko kuu la Mjini Magu kuingiza kiasi cha shilingi laki sita kwa miezi miwili badala ya kukusanya kiasi hicho kwa mwezi mmoja hali iliyobainika kuwepo mwanya wa kufujwa kwa fedha za mapato ya chanzo hicho na watumishi wa halmashauri idara ya fedha..



Diwani wa Kata ya Ngasamo Wilayani Busega Jejeje Manyama aliunga hoja ya iliyotolewa na Diwani Mwenzake Julias Ngongoseke wa Kata ya Lubugu (UDP) kutoa hoja ya kutaka kufahamu nini kimepelekea chanzo hicho kukusanya mapato madogo ili hali kilikuwa na wakala wa kukusanya mapato aliyekusanya kiasi cha shilingi 600,000/= kwa mwezi na sasa kushuka hadi shilingi 310,000/-kwa mwezi  jambo ambalo lilitakiwa kutolewa majibu na Mkurugenzi Nnko.

Akijibu hoja hiyo Mkurugenzi huyo alikiri kwa wajumbe wa baraza hilo kuwepo mapungufu ya kiutendaji katika Idara hiyo ya fedha na kuomba apewe muda wa kufanyia marekebisho ikiwemo kufatilia kwa ukaribu mapato ya vyanzo mbalimbali ili kuondoa mwaswali mengi kutoka kwa waheshimiwa madiwani ambao wameonekana kukelwa na majibu ya kila yasiyojitosheleza.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Boneventura Kiswaga (CCM) ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Uchumi na Fedha alisema kwamba kamati yake imeshitushwa na taarifa hizo za kukusanywa mapato kidogo ikiwemo kumuondosha wakala aliyekuwa anakusanya mapato ya soko hilo Samson Merthusela (Mtu binafisi) ambaye hata hivyo hakuwa na mkataba wowote wa Halmashauri hiyo bali kwa makubaliano.

Kiswaga aliwaeleza wajumbe wa baraza hilo kwamba Idara hiyo ya fedha inaonekana kufanya mambo kienyeji sana na kutofuata taratibu na kanuni zilizopo za Halmashauri hiyo ikiwemo ya mikataba inayoingia na Makampuni na Mashirika mbailimbali kutofuatwa kwa mujibu wa sheria zilizopo.

“Nakuagiza Mkurugezi,pamoja na kukiri udhaifu yaliyopo kwenye Idara hiyo ya fedha sasa kuwa makini na anza kufatilia kwa ukaribu na kuhakikisha mikataba iliyopo ya halmashauri inaheshimiwa na kufuatwa na wanaingia kisha kushindwa kuitekeleza basi taratibu za kisheria zichukuliwe ikiwemo kushikilia dhamana aliyoiweka wakati wa kuingia mikataba hiyo na halmashauri”alisema

Mwenyekiti huyo alimtaka Mkurugenzi Mtendaji kupitia upya vyanzo vya mapato vilivyopo na kuangalia upya uwezekano wa kuviboresha vya na kupeleka mapendekezo kwenye kikao cha baraza kitakachofuata ili madiwani waitambue kabla ya kuipitia na kulidhia kuiboresha jambo ambalo litaiwezesha halmashauri hiyo kukusanya mapato mengi zaidi ili kufikia malengo ya kutoa huduma kwa wananchi wake.

Hatua hiyo imeonyesha kuwepo baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo wasio waaminifu katika Idara ya fedha ,udhandisi wa barabara na majengo,kilimo,ardhi na maendeleo ya makazi, ugavi na manunuzi kutokana na hoja za mara kwa mara za madiwani kushutumu kuwepo uzembe na miradi mingi kujengwa  chini ya viwango kila vikao vya baraza vinapofanyika hali ambayo Mwenyekiti Kiswaga ameonya na kumtaka Mkurugenzi Nnko kuwachukulia hatua watumishi na Wazabuni na kuzuia dhamana zao ikiwemo kuwaondosha watakaoshindwa kufuata taratibu kwa kuzigatia sheria  za kazi na mikataba.



Mkurugenzi Nnko alisema kwa wajumbe wa kikao hicho kwamba tayari hatua za kuwafukuza kazi zimeisha tekelezwa na kuwataja waliofukuzwa kuwa ni Winfrida Sanga,Josephat Kajilo,Mathias Bulashila,Bertha Sahani,Emmanuel Mashimba,John Shilunga,Reuben Selestine na John Chululuka huku Samson Aron (Afisa Mtendaji wa kijiji) akihukumiwa kwenda jela miezi 9 kwa kosa la kuiba na kuuza chakula hicho baada ya kufunguliwa kesi na kufikishwa Mahakama ya Wilaya hiyo.

Nnko aliwataja watumishi wengine wa Halmashauri waliochukuliwa hatua ni pamoja na Lutundula Mabimbi aliyekuwa Afisa Kilimo na Mifugo wa Wilaya hiyo aliyefukuzwa kazi mwezi uliopita kwa kukiuka taratibu za kazi kufatia taarifa ya tume iliyoundwa kuchunguza tuhuma za kugawa Power Trel 6 na Pikipiki 6 zikiwa na mapungufu ya vifaa kubainika huku  aliyekuwa Afisa Ugavi na Manunuzi Mbrose Monyiaichi akishushwa cheo baada ya kubainika kuhusika na mapugufu hayo.




Aidha kikao hicho kilipokea taarifa ya kufukuzwa  kazi kwa watendaji wa vijiji vinane Wilayani humo waliobainika kufuja fedha za chakula cha msaada kilichotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu kisha kusambazwa na halmashauri kwa wananchi wa maeneo yao yaliyokumbwa na tatizo la ukame na kusababisha kuwepo njaa kwa baadhi ya wananchi hao na kutakiwa kununua kwa bei ya chini.


Hatimaye kikao hicho kiliahirishwa mpaka tarehe tajwa....