ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 22, 2013

TAMPERE WAKABIDHI GARI LA ZIMAMOTO KWA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA.

Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akihutubia wananchi na wageni waliofika katika viwanja vya Ghand Hall,  kushuhudia makabidhiano ya msaada wa gari la Zimamoto yaliyofanywa na jiji rafiki la Tampere toka nchini Finland kwa kukabidhi msaada huo kwa jiji la Mwanza.
Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula (kushoto) akikata utepe kwa kushirikiana na Bi. Kaisn Anttoncn ambaye ni Director Chair of PST wa jiji la Tampere.
Bi. Kaisn Anttoncn ambaye ni Director Chair of PST wa jiji la Tampere naye akikata kipande cha utepe kwaajili ya kumbukumbu huku akishuhudiwa na Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula.
Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akikagua ubora wa gari hilo toka katika uskani huku akiwa na Bi. Kaisn Anttoncn ambaye ni Director Chair of PST wa jiji la Tampere. Thamani ya gari hili ni zaidi ya shilingi millioni 500 za Tanzania.
Mstahihi Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akimkabidhi funguo Kaimu kamanda wa kikosi cha Zimamoto mkoa wa Mwanza Christon Mamyologa mara baada ya kupokea msaada huo toka jiji rafiki la Tampere toka nchini Finland.
 Kaimu kamanda wa kikosi cha Zimamoto mkoa wa Mwanza Christon Mamyologa akionyesha ufunguo wa gari hilo sambamba na kadi yake mara baada ya makabidhiano.
Sasa ni wakati wa majaribio...
Wafanyakazi wa zimamoto wakikimbilia eneo la tukio...!!
Stop..!! amri toka kwa kiongozi.
Zimamoto kikazi zaidi...!!
Picha ya pamoja ya wadau ofisi ya Halmashauri ya jiji la Mwanza pamoja na jiji rafiki la Tampere.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.