ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 14, 2013

SASA UNAWEZA KUEPUKA MATUMIZI MAKUBWA YA MKAA NA KUNI.

Mchuuzi na wateja wake akiuza jiko la kisasa linalotumia vipande vitatu tu vya kuni ndogo, unawasha kisha moto ukiwaka unavitoa nawe unaendelea na mapishi au uchemshaji maji. kwa ndani kwenye kuta za jiko kuna pumba za mchele au pamba ambazo huwekwa na kushindiliwa vyema zikiacha tundu katikati ambalo husaidia kupitisha moto kwaajili ya mapishi.
Majiko haya yaliyofumwa na mwandishi wa g.sengo blog PETER FABIAN yakiuzwa katika lango kuu la hospitali ya wilaya mkoani Geita yamepata wateja wengi sana kutokana na ufanisi wake na kuwapunguzia gharama za matumizi ya fedha kupitia ununuaji wa mkaa na matumizi ya kuni nyingi. 
Mjasiliamali huyu pia anauza taa zinazo tumia solar yeneye uwezo wa kuwasha taa nne ambazo utazifunga kwenye vyumba tofauti majumbani kwa matumizi ya kutoa mwanga wa kutosha kwa muda wa saa 48. 
Ni solar na taa zake zisizokula umeme mwingi zilizotengenezwa kwa teknolojia ya kisasa kuzalisha mwanga wa kutosha penye giza.
Ni bidhaa zinazozalishwa toka mkoani Arusha na sasa zimevamia kanda ya ziwa kuwaokoa wananchi na kipato chao sambamba na kulinda mazingira kwa kuepuka matumizi makubwa ya ukataji miti kuwa kuni na uzalishaji mkaa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.