ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 14, 2013

SALHA ISRAEL ATEMBELEA KAMBI YA TANZANIA TOP MODEL 2013


 Mrembo Salha Israel atembelea kambi ya washiriki wa sindano la Tanzania Top model iliopo katika hoteli ya Jb Belmont iliyopo maeneo ya posta kwa lengo la kuwapa mbinu mbalimbali za kufanya vizuri jukwaani kwani shindano hilo lina upinzani mkali kwa washiriki wenyewe kwa wenyewe.

  Salha alitoa mbinu mbalimbali za kujiamini kwa mwanamitindo awapo jukwaani pamoja na mbinu za kujibu maswali kiusahihi kwa wanahabari ambapo imezoeleka kwa washiriki wengi hushindwa kujibu maswali kiusahihi kitu ambacho hupunguza ari ya shindano.
Washiriki wakimsikiliza kwa makini Salha Israel wakati akiongea nao.
Salha israel mrembo alieng'ara miaka ya 2011 katika mashindano ya urembo nchini,akiongea na washiriki wa Tanzania Top Model 2013 namna ya kujiamini wakiwa katika jukwaa na kujibu maswali endapo watakabiliana na vyombo vya habari.
 Fainali za mashindano haya zitafanyika desemba 7,pia washiriki watapigiwa kura na wananchi ambapo namba maalumu itaolewa hivi punde kumpigia mshiriki umpendae ili kumuongezea alama amabazo zitamwezesha mshiriki wako ashinde.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.