ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 8, 2013

MGAMBO ISAIDIE OPARESHENI KIMBUNGA-DC

Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Erasto Sima, akikagua kikosi cha mgambo wakati akifunga awamu ya kwanza ya mafunzo ya Mgambo katika Kijiji cha Ikungulyambeshi ‘A’ Kata ya Kilalo wilayani humo.
Kikosi kikipita kutoa heshima. 
"Heshimaaaa....Toaaa....!!"
kwa-kwa-kwa-kwaaa..!
Ukakamavu.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Erasto Sima, akihutubia wakati wa shughuli ya kuhitimisha awamu ya kwanza ya mafunzo ya Mgambo katika Kijiji cha Ikungulyambeshi ‘A’ Kata ya Kilalo wilayani humo.
Mshauri wa Mgambo wa wilaya hiyo Sajenti Ndasan Josephat akitoa nasaha zake.
"Ili muwe wakakamavu mwahitaji kuwa na afya na afya hujengwa kwa mazoezi" 
Picha ya pamoja.
Habari na Peter Fabian.
SERIKALI wilayani hapa, imewaagiza vijana waliohitimu mafunzo ya Mgambo wasaidie kukamata wahalifu mbalimbali, wakiwemo wahamiaji haramu waliokimbia opalesheni Kimbunga na kujificha wilayani humo.

Imewaonya baadhi ya wanasiasa wanaopinga mafunzo hayo na kuwaasa vijana hao wasitumie vibaya mafunzo waliyopata, yakiwemo ya siraha, kwa kujihusisha na vitendo vya ujambazi, ujangiri, uuzaji na utumiaji wa madawa ya kulevya, vinginevyo watakiona cha mtema kuni.

Wito huo ulitolena na Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Erasto Sima, juzi katika Kijiji cha Ikungulyambeshi ‘A’ Kata ya Kilalo wilayani humo, wakati akifunga awamu ya kwanza ya mafunzo ya Mgambo Katani humo.

Sima alisema kwamba, baadhi ya watu wakiwemo wana siasa walijaribu kukwamisha mafunzo hayo kwa kuwashawishi vijana wasishiriki lakini wananchi na viongozi wanaojali maslahi ya umma, walisimama kidete na kushirikiana na wakufunzi wa JWTZ, hatimaye mafunzo hayo yakafanyika kwa ufanisi.

“Baadhi waliona mafunzo haya ni jambo la kisiasa wakati sivyo, maafunzo haya ni kwa ajili ya ulinzi na usalama wa nchi yetu hivyo mliopata mafunzo, msaidie opaleshen Kimbunga kwa kufichua wahamiaji haramu waliokimbilia kujificha huku.” Alisema Mkuu huyo.

Alieleza kuwa ni wajibu wao kulisaidia taifa kupambana na uhalifu mbalimbali ukiwemo dawa za kulevya, rushwa, majambazi, majangiri ambayo yanaisumbua nchi yetu na kujitolea katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa taifa.

“Jeshi la Mgambo limeanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 147, kifungu (1) na (2) kwa kuwa vijana ndiyo tegemeo la taifa, msikub ali kushawishiwa kukataa mafunzo ya mgambo, wanaowakataza ni maadui wa ndani wasioitakia mema Tanzania, ole wao watakao bainika.” Alionya Sima.

Mshauri wa Mgambo wa wilaya hiyo Sajenti Ndasan Josephat akiwapongeza vijana hao na wakufunzi wa JWTZ, alieleza kwamba, anayo furaha kubwa kupata walinzi 138 waliohitimu mafunzo ya ukakamavu, ujanja wa porini, mbinu za kivita na siraha ndogondogo kwa manufaa ya umaa.

Awali katika risara yao iliyosomwa na Hosea Peter, Mgambo hao walisema kwamba walioandikishwa katika mafunzo hayo walikuwa vijana 540 lakini waliohitimu ni 138 ( wanawake wakiwa sita) kutokana na wengine kukimbia mafunzo hayo kwa kushawishiwa na baadhi ya watu.

Vijana hao waliiomba serikali iwape kipaumbele katika nafasi mbalimbali za ulinzi zinazopatikana na kuahidi kufanya kazi za kujitolea kulinda usalama wa wananchi na mali zao pia kupambana na kila aina ya uhaifu katika maeneo yao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.