ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 19, 2013

CRDB WAPANDA MITI 1000 HOSPITALI YA RUFAA BUGANDO

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo (wa pili kutoka  kushoto) akishiriki zoezi la kupanda miti katika hospitali ya Rufaa Bugando ambapo Benki ya CRDB imehisani shughuli hiyo ya upandaji miti 1000 kwaajili ya kutunza mazingira ya hospitali hiyo, wengine katika picha kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Bugando Dr. Charles Majinge, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Dr. Charles Kimei na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akipanda mti kuhifadhi mazingira ya Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza, zoezi lililohisaniwa na Benki ya CRDB.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Dr. Charles Kimei na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga wakipanda miti kuhifadhi mazingira ya Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza, Benki hiyo imeweka mikakati ya kuitunza miti hiyo mpaka itakapokuwa.
Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Bugando Dr. Charles Majinge (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo huku wadau wa CRDB na wahudumu wa hospitali hiyo wakifurahia zoezi hilo.
Ni wakati wa umwagiliaji sasa.
Wadau wa Benki ya CRDB nao walishiriki zoezi hilo kuhakikisha miti 1000 inapandwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza.
Zoezi la upandaji miti lilikuwa kubwa kwani miti 1000 siyo mchezo.. kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza, Mkuu wa Mkoa Injinia Ndikilo na Mkurugenzi wa CRDB Charles Kimei.
Wadau wa CRDB wakipanda miti na maua kuhakikisha BMC panakuwa mahali safi kimazingira.
Pamoja na upandaji miti, pia Mkuu wa Mkoa Injinia Evarist Ndikilo aliongoza zoezi la upakaji rangi jengo la Hospitali ya Bugando ambapo benki ya CRDB inahisani mpango huo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Charles Kimei. 
Kamanda wa Polisi Ernest Mangu akishiriki upakaji rangi jengo la Hospitali ya Rufaa Bugando anayefuata ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza.
Burudani toka Bujora Dance.
Ngoma Boys.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Charles Kimei akiwapongeza wafanyakazi wa CRDB Mwanza kwa kusimamia shughuli nzima kwa ufanisi.
Kamati.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.