ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 14, 2013

PAMBA YASHINDA 1-0 DHIDI YA TOTO LIGI DARAJA LA KWANZA

Pamba Sport Club.

Toto Africans.

PAMBA YASHINDA 1-0 DHIDI YA TOTO LIGI DARAJA LA KWANZA

NA. ALBERT G. SENGO: MWANZA

Timu ya soka ya Pamba ya jijini Mwanza imeanza vyema safari yake kuelekea ligi kuu mara baada ya kuifunga Toto Africans bao 1-0 katika mchezo wa kwanza wa kundi C, Ligi daraja la kwanza Tanzania Bara uliochezwa dimba la CCM Kirumba.

Pamba ilipata bao hilo la ushindi katika dakika ya 5 tu kipindi cha kwanza mfungaji akiwa ni Paschal Liponda mara baada ya kupokea mpira wa krosi ya winga machachari Mathius Wandiba.

Dakika 90 zinamalizika zikishuhudia Pamba wakitoka kidedea na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Toto.
- Athuman Bilali ambaye ni Kocha wa Toto Africans anazungumza na Sports Xtra juu ya kichapo kwa timu yake.


- Naye Kocha wa Timu ya Pamba Kazimoto Muzo alikuwa na haya ya kusema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.