ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 19, 2013

MAAJABU: PAMOJA NA KUPATA MZINGA WA KUTISHA WAKUTWA WAKIWA HAI

Mwananamke mmoja pamoja na dereva wamenusurika kifo kufuatia tukio la ajali mbaya ya kutisha mara baada ya kugonga nyuma ya roli lililokuwa likiendeshwa mbele yao.

Dereva pamoja na mwanamke huyo ambao walikuwa wakisafiria gari ndogo huku wakiwa katika mwendo wa kasi bila kuzingatia distance ya gari na gari wakiwa katika mji wa Guizhou nchini China walijikuta gari lao likibamiza nyuma ya roli lililokuwa mbele yao, mara baada ya roli hilo kupunguza mwendo.
Mwanamke huyo ambaye wakati wa tukio alikutwa amezirai, amelowa damu chepechepe huku akiwa hajavaa mkanda safarini wakati wa ajali alichomoka toka kwenye kiti chake na kichwa chake kubamiza kwenye kioo na kukivaa kama blauzi hali iliyomwonyesha kama kipande cha kichwa cha sanamu kilicho pachikwa kwenye kioo cha ajali ya gari.
Zima moto (waokoaji) waliwahi eneo la tukio na kutoa msaada, hatua ya kwanza ikiwa ni kwa uangalifu walianza kumchomoa dreva ambaye alikuwa katika upande rahisi kutoka kisha kwa mwendo wa kasi yenye umakini na uangalifu wa hali ya juu walianza kuvitoa vioo vilivyokuwa vimemzonga shingoni abiria huyo mwanamke ili wapate kumtoa kiurahisi bila madhara.

Kwa mujibu wa madaktari wa hospitali waliyolazwa jamaa hao ambapo wanapata matibabu taarifa zinasema kuwa hali zao zinaendelea kuimarika siku baada ya siku tofauti na hali waliyokuwa nayo siku ya Jumatano wiki hii walipopata ajali.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.