ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 18, 2013

ECOBANK YAFUNGULIWA RASMI TAWI LAKE JIJINI MWANZA

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo akikata pazia la jiwe la msingi kuashiria ufunguzi rasmi wa Ecobank Tawi la Mwanza katika shughuli iliyofanyika jana jioni kwenye jengo la benki hiyo lililopo barabara ya Karuta likitizamana na stesheni ya reli jijini Mwanza.

Hili ndilo jiwe la msingi.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo akisoma kwa umakini maelezo ya jiwe la msingi la ufunguzi aliloweka kwa tawi jipya la Ecobank litakalo hudumia wakazi wa pande zote Kanda ya ziwa pamoja na wageni waingiao na kutoka mkoani hapa.

Injinia Ndikiloakisalimiana na Afisa Masoko wa Ecobank mkoa wa Mwanza Manfred Kayala kabla ya kuingia ndani ya benki hiyo kukagua shughuli mbalimbali tawini hapo.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Ndikilo akisaini kitabu cha wageni kwenye tawi jipya la Ecobank Mkoa wa Mwanza huku akishuhudiwa na mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga (kulia) ambapo ndipo tawi hilo lilipo.

Ndani ya Ecobank tawi jipya jijini Mwanza. 

Mara baada ya uzinduzi huo hafla fupi ilifuata ndani ya hotel JB Belmont Mwanza ikihudhuriwa na viongozi wa serikali, wafanyabiashara, wajasiliamali wadogo kwa wakubwa hali kadhalika wandishi wa habari.

Mkurugenzi wa Ecobank Tanzania Enock Osei Safo anaimani kuwa benki yake italeta mapinduzi makubwa katika sekta za biashara ndogo kwa kubwa sambamba na kuimarisha soko la zao tegemeo la samaki. 

Injinia Ndikilo amesema kuwa kutokana na Benki hiyo kufungua tawi lake Mkoani Mwanza itawasaidia wafanyabiashara na wajasiliamali kupata huduma kwa ubora wa kiushindani hasa ikizingatiwa Mwanza ni kitovu cha nchi za Maziwa makuu na Jiji la pili kwa shughuli za kibiashara kubwa na linalokuwa kwa kasi zaidi nchini kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali ikiwemo za kibenki. 

Safu ya wafanyakazi wa Ecobank tawi la Mwanza.

Safu ya wafanyakazi wa Ecobank tawi la Mwanza.

Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nyamagana Raphael Shilatu, mkuu wa wilaya ya Magu Jaqueline Rianna, mkuu wa wilaya ya Sengerema na mkuu wa wilaya ya Ilemela Amina Masenza

Meneja wa TRA mkoa wa Mwanza idara ya mapato Mr. Shawiwa (katikati) akiwa na mkewe pamoja na mmoja wa wafanyabiashara maarufu ambaye ni mmiliki wa MSETI Investiment.

Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Maji Taka mkoa wa Mwanza (WAUWASA) Antony Sanga, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga Patrick Kalangwa pamoja na mmoja wa wadau muhimu wa Ecobank. 

Wakuu mbalimbali.

Meza hii ya wadau iliongozwa na Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Ernest Mangu (aliyeketi wa kwanza kulia).

Ni wafanyakazi wa Ecobank wakiwa na zawadi kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, kutoka kushoto ni Ziada Lymo na Anachurine Mushi

Philomena Jacob ambaye ni meneja wa Ecobank tawi la Mwanza (kushoto) akimkabidhi zawadi mkuu wa mkoa wa Mwanza injinia Ndikilo kama kumbukumbu ya ufunguzi wa tawi la benki hiyo.

Kwa mujibu wa Bi. Philomena picha iliyochorwa ya farasi huyu akimbiaye ni mfano wa taswira ya Ecobank katika kuyafukuzia mafanikio kwa wananchi hivyo wategemee kasi katika ukuzwaji kiuchumi kupitia Ecobank.

Naye Mkurugenzi wa Ecobank Mr.Enock alipata fursa ya kumtunukia zawadi mkuu wa mkoa wa Mwanza kwenye hafla hiyo.

Wadau walipata fursa ya kupata chakula cha pamoja na kuabadilishana mawazo.

Wadau namba moja.

'Tuko sawa, karibu ufaidi huduma zetu'

Ecobank Mwanza Crew.

Wafanyakazi wa Ecobank na wakuu wa idara mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na safu ya meza kuu kutoka kulia ni Mkuu wa wilaya Nyamagana Baraka Konisaga, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo, Mkurugenzi wa Ecobank Enock Osei Safo, Mstahiki meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula na Meneja wa tawi Ecobank Mwanza Bi. Philomena Jacob.

Meneja wa tawi Ecobank Mwanza Bi. Philomena Jacob akizungumza na waandishi wa habari.

Mjengo wa Ecobank tawi la Mwanza.
"Ecobank, pamoja na huduma za kibenki pia ina kampeni yake ya Ecobank Inakuwezesha inayonuia kuwawezesha watanzania kutambua nafasi mabalimbali za kiuchumi kwa kutoa ujuzi, maarifa na elimu  ili kupiga hatua zaidi katika kuzishika zile nafasi na kuboresha maisha ya wananchi. Nawaomba wananchi kutambua nafasi hizi na kuzipokea kila zinapotokea kwani tutafaidi sana kwa kupata maarifa kutokana na uzoefu wa benki hii katika nchi mbalimbali Afrika na kujifunza kutokana na changamoto za nchi nyingine ili kutusaidia sisi kuepuka matatizo madogo madogo katika mada yetu ya maendeleo". alisema Injinia Ndikilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.