ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 19, 2013

DIRECTOR "JOHN KALLAGHE" ALIFANYA KWA TID, JAY DEE, MATONYA NA SASA KWA "AMA G"?

Director John Kalage.

Ama G.
Muandaaji wa video wa kampuni ya Kalla pics amejikuta akikataa au kuzungusha kukabidhi video mpya ya msanii AMA G ambaye alifanya poa kupitia video ya NENDA SALAMA siku za hivi karibuni, kichupa hicho kipya cha AMA G kilifanyika miezi kadhaa (5) iliyopita chini ya kampuni ya KALLAPICS na kutokana na sababu ambazo hadi sasa hazijafahamika kichupa hicho hakijatoka.

Wadau wengi wamekuwa wakihoji, kwa nini kila siku iwe Kallage? 

Msanii Ama G amesema kuwa hatopenda kulizungumzia kwa kina suala hilo kwani tayari amekwisha lifikisha mbele ya vyombo vya dola na kukabidhiwa RB, hivyo kinachofuata ni kumnasa director huyo na kumfikisha panapostahili ili aweze kurudisha gharama zote likiwemo suala la kupotezewa muda!

Ama G. amesema kuwa mara baada ya kushauriana na wadau wake siku si nyingi atauweka wazi mkasa mzima wa tukio na kipi kilichojiri.

Taarifa hii imewasilishwa na DJ Sauti.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.