ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 6, 2013

LIGI DARAJA LA 3 NGAZI YA MKOA WA MWANZA LIVER SIDE WAONA MWEZI

Ratiba ya ligi soka daraja la tatu ngazi ya mkoa wa Mwanza inayoendelea kwenye uwanja wa Nyamagana.
Ndani ya uwanja wa Nyamagana jijini mwanza katika ligi soka daraja la 3 ngazi ya mkoa inayoendelea, mchezo baina ya Lake Worious na Liver side uliochezwa tarehe 4/04/2013, ulimalizika kwa River Side kuibuka kidedea kwa mara ya kwanza kwenye ligi hiyo kwa kuifunga Lake Worious ya Ukerewe bao 1-0, mfungaji akiwa ni Frank Kulwa kwenye ungwe ya lalasalama.
Mmoja kati ya washambuliaji wa Liver side akiukokotoa mpira toka pembe moja ya uwanja wa Nyamagana katika mchuano wa soka ligi daraja la tatungazi ya mkoa.
Kwa matokeo hayo kwa mara ya kwanza Liver side imeambulia pointi na kuwa na pointi 3, huku timu ya Lake Worious ikibakia na pointi zake 7 ilizozivuna hadi sasa.
Msahambuliaji wa Liver side Frank Kulwa akiinyanyasa ngome ya Lake Worious.

"Ngoma katikati ya miguu huku kila timuikijitahidi kwa ufundi kuona ni jinsi gani inapata ushindi"

"Ni hatari langoni mwa Lake Worious lakini anajitokeza pale beki wa timu hiyo na kuiondosha hatari..."

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.