ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 20, 2013

UHAMIAJI MKOA WA MWANZA YANASA WATATU.


IDARA ya Uhamiaji Mkoani Mwanza imeendelea kuwanasa Wahamiaji haramu wanaoingia nchini kwa njia za panya baada ya hivi karibuni kuwakamata vijana watatu raia wa Burundi.

Akizungumza ofisini kwake leo Naibu Kamishina Msaidizi na Kaimu Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza Bi. Anamaria Yondani alisema kwamba hii inatokana na Idara hiyo kuendelea kupokea taarifa kutoka kwa wananchi na kuzifanyia kazi, huku pia uhamiaji ikiendelea kutekeleza mradi wa Shirika la Kimataifa ambalo linahusika na shughuli za Kiuhamiaji (OIM) kupitia mradi wa Capacity Buiding in Migration Management (CBMM-II)

Bi Yondani aliwataja vijana hao waliokamatwa kuwa ni Akizmana Adamu (15), Gerlad Michael (17) na Boaz Ernest (15) wote wakazi wa Ruingi  raia wa nchi yaBurundi walioingia nchini kwa njia za Panya kupitia Mkoani Kigoma kabla ya kunaswa Mkoani Mwanza wakiwa kwenye harakati za kutafuta kazi ili kuwasaidia kuishi nchini kinyume cha taratibu na sheria za nchi.

Kaimu Mkuu huyo wa Uhamiaji Mkoa  alisema tatizo la wahamiaji haramu limekuwa ni Janga la Kitaifa na Mkoa wa Mwanza ni Kitovu cha Mawasiliano, Biashara ,Elimu na Usafiri kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Nchi za Maziwa Makuu na wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akitoa taarifa ya Mkutano wa Kamati ya  National Immigration Inter-regional Steering Committee (NIISC) uliofanyika Mjini Sumbawanga Mkoani Rukwa Machi 11 hadi 12 mwaka kwa lengo la kuendeleza mradi wa CBMM-II, kuongeza Mikoa wanachama wa NIISC na Namna ya kushirikiana na IOM katika kuendeleza mradi wa huo ambayo yalijadiliwa katika mkutano huo.

“Mradi huu wa NIISC awali ulianzisha na Mikoa ya Mwanza, Mara, Kagera na Kigoma mwaka 2012 na kasha kuongeza Mkoa wa Rukwaa hii ikumbukwe ipo katika Kanda ya Ziwa ambapo kuna vivutio  kadhaa vinavyosababisha wahamiaji haramu kuingia na kujipenyeza katika sekta za i Uvuvi, Kilimo, Ufugaji, Madini, Biashara, Elimu na Usafiri  hali ambayo Uhamiaji imekuwa ikizifanyia  doriawavutia ”alisema

Aidha katika mkutano huo  uliweza kuongeza wanachama wapya katika Kamati ya NIISC ambayo ni Mikoa ya Geita, Shinyanga ,Tabora na Katavi ili kuongeza ushirikiano katika kubadilishana taarifa na uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ndaji ya kila siku katika kupambana na wimbi kubwa la wahamiaji haramu.

“Tunatambua wahamiaji haramu bado wanaendelea kupitia  nchini mwetu kwa ajili ya kuelekea  nchini Afrika ya Kusini ambapo awali walikuwa wakipita Mpaka wa Sirali kutokea nchi ya Kenya kuingia Wilaya ya Tarime,Musoma kisha Mkoani Mwanza na kuelekea Mikoa ya Kati hadi Mkoani Mbeya kabula ya kuanza safari kuelekea nchi za kusini hadi Afrika Kusini ili kuwa lahisishia kwenda nchi za Ulaya”alisema.

Bi Yondani alisema kwamba baada ya kutekelezwa kwa mradi wa CBMM-II wahamiaji haramu  waliamua kubadili njia pengine kupita mawakala ambao ni raia wa Tanzani wanaowasaidia kuwaingiza kwa njia haramu na sasa kupitia Mikoa ya Kaskazini ya Kilimanjaro,Arusha,Manyara na Tanga na kuelekea mikoa ya Kati kwa ajili nya kuelekea Mkoani Mbeya na kuvuka kuelekea Malawi na Zambia.

“Lengo kuu la wahamiaji haramu ni kwenda Afrika Kusini ni kutafuta maisha bora na kuwa njia lahisi ya kwenda Mataifa ya Bara la Ulaya na Marekani huku wahamiaji wengi wanaoingia kinyume na utaratibu wa kisheria wengi ni kutoka nchi za Ethiopia,Eritrea na Somaliaambao wamekuwa wakinyanyaswa, kuteswa na kufariki wanapokuwa safarini kwenye maroli ya mizigo na watu wanaowasaidia”alisema

“Wanatumia njia za panya kusafiri kupita mipaka isiyo rasimi  na husaidiwa na mawakala  (Maajenti) wao ambao wengine ni watanzania wasio na uzalendo na wamekuwa wakiwapakiza katika maroli ya mizigo,magari ya makontena  na hata wengine kupitishwa kwenye Hifadhi za wanyama wakali na baadhi yao kupitia Ziwa Victoria kwa mitumbwi na kuvuka mito yenye wanyama wakali wakati wa usiku”alieleza

Bi.Yondani ametoa wito kwa wananchi kurejesha uzalendo wa Taifa na kushirikiana na maafisa uhamiaji na polisi kutoa taarifa kwa watu ambao wanawahisi kuwa siyo raia na watu ambao wameingia kwa njia za panya katika maeneo mbalimbali ya Mikoa yao na wanaotafuta kujipenyeza kufanya kazi ambazo zitawasaidia kuonekana kuwa ni raia wakati huu taifa linaelekea kutoa vitambulisho vya uraia .

“Wananchi sasa warudishe uzalendo wao na kuacha kuwasaidia wageni na wahamiaji haramu walioingia nchini kinyume cha taratibu na kuvunja sheria za nchi kwa kuwatolea taarifa kwa ofisi za uhamiaji na vituo vya jeshi la polisi kwa lengo la kupambana na janga hili la kitaifa la kupambanana wahamiaji haramu wanaoingia nchini kila siku kwa kusaidiwa na mawakala na kuhifadhiwa na watu wasiokuwa na uzalendo”alisisitiza

Amevipongeza vyombo vya habari kwa kushirikiana na Idara hiyo kutoa taarifa kwa wananchi ikiwemo Elimu kwa kueleza bayana athari za kuwa na wahamiaji haramu ambao wengi wao wamekuwa wakifanya uhalifu na kuwapora mali na kufanya mauaji kwa wananchi na sasa wananchi katika maeneo yao ya mitaa na kata kuwa kuwatolea watu ambao si raia ili kuwabaini kabla ya kutolewa vitambulisho vya uraia kitaifa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.