ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 23, 2013

FREDERICK LAWSON KIBOKO YAKE SOWAH


Lile pambanolililokuwa linasubiriwana mashabiki wengi wa ngumi katika jiji la Accra nchini Ghana kati ya bondia kijana anayechipukia Frederick Lawson na mkongwe Isaac Sowah limemalizika muda wa sekunde ya 43 katika raundi ya tatu baada ya referii Shedrack Aquaye kuingilia kati kumwokoa Isaac Sowah asiendelee kupokea mkong’oto kutoka kwa kijana Frederick Lawson.

Wawili hao walikutana kwenye uwanja wa mpira wa Accra katika mpambano ambalo ulirushwa live na Super Sport pamoja na mitandao ya televisheni nyingi duniani. Mpambano mkubwa usiku wa leo ulimshughudia mbabe Joseph Agbeko wa Ghana akimshinda kwa taabu na kuchukua ubingwa wa dunia dhidi ya bondia kutoka nchini Columbia Luis Melendez.

Kwa sasa bondia Frederick Lawson anangojea mapambano mengine ya kuinua kipaji chake na anga ndiyyo tu itakuwa kilele chake katika juhudi zake za kuchanja mbuga kwenye ngumi!

Pambano la wawili hao lilisimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Africa, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi ambaye yuko katika jiji la Accra akitokea Windhoek, Namibia!

INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.