ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 1, 2013

BONDIA ALBERT MENSAH KUWA NA WAKATI MGUMI ULINGONI TAREHE 30, MACHI


FOR IMMEDIATE RELEASE – Friday, March 1st, 2013 -Dar-Es-Salaam, TANZANIA- Bondia wa IBF aliye na kiwango cha namba 11 duniani katika uzito Jr. Welter, Albert Mensah wa Ghana atakuwa kwenye wakati mgumu atakapombana na bondia mkongwe ulingoni na asiye na huruma na ngumi zake Mghana Ben Odamettey katika mpambano wao wa kugombea mkanda wa “IBF Africa uzito wa jr. Welter”.
Pambano hili linalowafanya Waghana wengi kuwa na roho juu juu kuhusu ni nani haswa mbabe kati ya wawili hao litafanyika jijini Accra, Ghana tarehe 30 Machi 2013 na linaandaliwa na kampuni kubwa ya kupromoti ngumi ya “GoldenMike Boxing Promotions Syndicate” inayomilikiwa na bwana Michael Tetteh andHenry Many-Spain.
Albert Mensah (kulia) akifanya anachokipenda sana  “Kuwaadhibu wapinzani wake”

Huu ni wakati ambao Waghana wengi kutoka kila kona ya nchi waliokuwa wanaungojea na wawili hao hawajaacha kugeuza hata jiwe moja kwa namna wanavyojifua kwa mazoezi yao ya mpambano huu!

Albert Mensah, ni bondia mtulivu na anayetumia akili nyingi ulingoni ambaye mabondia wengi waliokutana naye wanakiri kuwa huwezi kujua anachokifikiri ukingoni na hata ni ngumi gani atairusha kwako na wakati gani. Ni bondia aliyepewa nafasi kubwa sana ya kuchukua umaarufu wa bondia bingwa wa zamani wa dunia wa Ghana Profesa Azumah Nelson.
Naye bondia mwenye madaha na majivuno mengi Ben Odamettey, huu ni wakati wa ukweli umewadia kwani atatakiwa kuwahakikishia wapenzi wake kuwa hana wasiwasi na mpambano huu na kwamba yuko tayari kukumbana na adui wake mkubwa ambaye ni “Hasira”
Wakati ambao Waghana wa kila umri na rika zote waliokuwa wanaungojea na hawatangoja zaidi ya tarehe 30 Machi, 2013.
ISSUED BY:
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. Please let me knοw if you're looking for a writer for your blog. You have some really good posts and I believe I would be a good asset. If you ever want to take some of the load off, I'd love
    tο wгite somе aгticlеs for your
    blog іn exchange for a link back tο mine.

    Pleаse shoοt me an e-mail if interеsted.
    Thank you!

    My wеb blog - mrbean73.blog.com
    My webpage: Iphone 5 Case Otterbox

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.