ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 2, 2013

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AZINDUA TAASISI YA UHASIBU TANZANIA TAWI LA MWANZA.

Naibu waziri wa Fedha  Mh. Saada Mkuya Salum akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Tawi la Mwanza na kufanya Taasisi kuwa na matawi matano nchini, huku akishuhudiwa na  Mwenyekiti wa MAB - Prof. Isaya Jairo (wa pili kulia) pamoja na mkurugenzi wa TIA Shah Hanzuruni, matawi mengine yapo mikoa ya Mtwara, Mbeya, Singida na Makao Makuu Dar es salaam. 

Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza ambaye alimwakilisha mkuu wa mkoa wa Mwanza, akimkaribisha mgeni rasmi  Naibu waziri wa Fedha  Mh. Saada Mkuya Salum, kuzindua tawi la Taasisi hiyo ya fedha mkoani Mwanza,  

Hii ni ngoma ya Bujora ambayo hucheza na nyoka na hapa wachezaji wake wakionyesha 'mautundu' katika uzinduzi wa Tawi la Taasisis ya Uhasibu Tanzania (TIA) jijini Mwanza, taasisi iliyopo chini ya Wizara ya Fedha. 

Ngoma ya kundi la Bujora toka kituo cha kuhifadhi kumbukumbu za watu wa kabila la wasukuma ambayo hucheza na nyoka na hapa wachezaji wake wakionyesha 'mautundu' zaidi katika uzinduzi wa Tawi la Taasisis ya Uhasibu Tanzania (TIA) jijini Mwanza, taasisi iliyopo chini ya Wizara ya Fedha.

 "Lekaga tobine Bamping"

Moja kati ya mashuhuda wa tukio, walimu wa taasisi ambao walichanganyika na wananchi.

Mwanza House of talent walifunika mbayaaa na igizo lao.

Naibu waziri wa Fedha  Mh. Saada Mkuya Salum akifanya ukaguzi kukagua majengo ya madarasa ya chuo cha Taasisi ya Uhasibu Tanzania tawi la Mwanza.

Moja kati ya madarasa ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania tawi la Mwanza yaliyopo Nyakato Buzuruga wilayani Ilemela.

Naibu waziri wa Fedha  Mh. Saada Mkuya Salum akifungua pazia la jiwe la msingi kuashiria uzinduzi rasmi  wa Kampasi ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania tawi la Mwanza shughuli iliyofanyika jana mkoani hapa.

Kama jiwe linavyosomeka .

Naibu waziri wa Fedha  Mh. Saada Mkuya Salum akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo. Msikilize kwa kubofya play..

Picha ya pamoja kwa Naibu waziri wa Fedha  Mh. Saada Mkuya Salum pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania tawi la Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.