ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 12, 2013

SOMA KILIO CHA MACHOZI YA DAMU CHA BAADHI YA WANASAUTI MWANZA WAKILIA KUSALITIWA

By kijungu jiko View Post

Malisa Godlisten Rais wa Serikali ya WanafunziSAUTSO Chuo kikuu cha St Augustine umetudharirisha mpaka tunaona aibu sasa na vuguvugu la CHADEMA, tena tuliingia kwa mbwembwe kali kuwa tutakuwa wakombozi wa watu, waliotuchagua kwa kura nyingi richa ya kuwepo nguvu kubwa ya viongozi waliotangulia hasa Rais Bwana Cosmas Mataba na Anna Mushi, Spika wa Bunge Bw Maro Pius, na aliyekuwa Waziri mkuu Bw Leonard Mafuru, tukamchagua kijana huyu aliedaiwa machachari akitokea Baraza la vijana la CHADEMA yani BAVICHA kwa kishindo cha zaidi ya asilimia 75% licha ya hira za Mataba na Tume yake ya Uchaguzi, tukashinda uchaguzi kwa mbwembwe kabisa tukimtupilia mbali mgombea aliefadhiriwa kwa gharama kubwa na CCM Bwana Antony na Mgombea mwenza Bibie Alice, tuliingia huku wanafunzi wakiwa na matumaini makubwa ya kuona mabadiriko kufuatia manung’uniko ya serikari ilio tangulia ya Bwana Mataba, Maro na Mafuru kutuhumiwa kwa ufisadi, ubadhirifu Ngono na matumizi mabaya ya ofisi na kupeana madaraka ya SAUTSO (Maro na Mataba wanadaiwa kuongoza serikali hiyo ya 2011/2012 kwa ubia wa makubaliano maalum…. Source kinasa sauti cha siri kilichomrekodi Bwana Maro kwa siri na vijana wa CHADEMA nyumbani kwake Nganza). Tuliingia tukiwalaumu wenzetu waliotutangulia lakini kwa mtazamo wa haraka hakika wao na sisi wana unafuu mkubwa wa kukumbukwa, hakuna kilichofanyika wala kubadilika, Ahadi zote tulizo ahidi mpaka wakati huu tunapoelekea kufanya uchaguzi tena hakuna dalili kuwa tutafanya chochote,

Tumeshindwa kabisa kutekeleza ahadi zifuatazo:-
1. Tuliahidi kujenga kutuo cha polisi katika jamii hii ya watu zaidi ya 26,000 ili kupambana na vitendo vya ubakaji wa dada zetu katika maeneo tofauti ya vuinga vya chuo hiki tumeshindwa.
2. Tuliahidi kuhamia kwenye ofisi mpya za SAUTSO ili kuongeza ufanisi wa shughuri zetu mpaka sasa hivi haifahamiki mradi huo umeishia wapi.
3. Tuliahidi kupambana na matatizo ya mikopo kwa wanafunzi lakini hakika hivi sasa tuna matatizo makubwa katika idara ya mikopo kuliko hata wakati wa Mataba, mikopo inachelewa, majina yanachanganyika, na mpaka hivi sasa kuna watu hawajaona mkopo since waje mwezi September.
4. Tuliahidi kuanzisha utaratibu wa kutunza kumbukumbu za kudumu lakini hilo limeshindikana.
5. Tuliahidi kurekebisha miundo mbinu ambayo sio rafiki kwa wenzetu wenye changamoto ya viungo sijui tumeishia wapi.
6. Bunge limekuwa genge la malumbano, migawanyiko, makundi ya urais ujao, na mijadara ya miradi isiyotekelezeka,
7. Umeme madarasani bado na viongeza sauti bado ni kero.
8. Unyanyasaji wa kimapenzi umekithiri hasa kwa viongozi wa kike pale SAUTSO.
9. Kuna serikali ya siri ya Bw Tungaraza ndani ya serikali ya Bw Malisa,
10. Migawanyiko iliyotokana na maslahi binafsi na uroho wa fedha umezidi.
11. Ubadhirifu wa pesa umeongezeka na pesa zinaishia kwenye mikono ya mabosi wachache wa SAUTSO.
12. Bwana Malisa mwenyewe anaongoza kwa matumizi mabaya ya fedha za wanafunzi, amesafiri zaidi kwa Ndege hata zaidi ya Bwana Mataba na Serikali yake, hakai ofisini, hatekelezi majukumu ya SAUTSO kwa wakati, wanafuzi wanalaumu kuwa muda mwingi pamefungwa, na wasaidizi wake wana kauri mbaya hasa idara ya mikopo, Malisa yuko busy facebook mara sijui naenda Lunch, nimepoteza simu, mara sijui najiandaa kupanda ndege, mara sijui natoka wapi naenda wapi je hiyo ndio spirit ya wana BAVICHA.
13. Tuliahidi Basi la SAUTSO mradi umeishia hewani bila maelezo.
14. Funga kazi ni kitendo cha aibu cha maandalizi ya michezo ya Vyuo vya SAUT kule Morogoro hali ilikuwa ni ya aibu, michezo mibovu, hakukuwa na motisha, zawadi hovyo, ugomvi, mazingira magumu, nilibahatika kupata taarifa kuhusu michezo ya aina hiyo ambayo ilifanyika Mtwara wakati wa Bw Mataba, yani ni mara Elfu kumi Tamasha la Mtwara, kulikuwa na msisimko, watu wengi, zawadi nzuri, malazi safi, chakula kingi, matibabu, michezo mingi, na Ratiba ya kueleweka, yani kilichofanyika Morogoro hakikuwa tofauti na Kombe la mbuzi kwenye shule Fulani za kata.
15. Chini ya Uongozi wa Malisa na wenzake Umoja wa vyuo vya SAUT Umekuwa na picha mbaya, pesa zilitafunwa, watu wakapigana, zawadi zikaibiwa, makombe yakachanganyikana, mgeni rasmi kwa aibu kubwa akapigwa na maganda ya ndizi, mayai viza na kondomu zilizotumika ebu pata picha hali ingekuwa nihiyo kule Mtwara ambapo mgeni rasmi alikuwa ni VC KITIMA mwenyewe na wakuu wengine wa SAUT Tanzania nzima.

Aliyetuponza mpaka hapa ni mambo ni mengi ila TUNGARAZA ametuponza pia kwa kujaribu kuingilia kwa siri kila jambo, Vijana wa BAVICHA tuliohusika katika harakati za kukuweka madarakani tumeishiwa na imani kabisa tunahitaji mabadiriko ya vijana wajao katika nafasi hizi tulijitoa kwa moyo na maisha yetu mpaka hata kufikia hatua ya kuweka masomo yetu hatarini kwa kupambana na viongozi waliotangulia Bw Mataba na wenzie kufanikisha hili ila tumekatishwa tamaa.

TUMECHOKA NEXT TIME BAVICHA TUNATAKA MABADIRIKO TUNAIDHARIRISHA CHADEMA KWAKWELI

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.