ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 29, 2012

TASWA YAFANYA MKUTANO MKUU NA WANACHAMAWAKE BAGAMOYO MKOANI PWANI.


Baadhi ya wanachama wa TASWA wakiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete. 

Katibu Mkuu wa TASWA Amir Muhando akizungumza katika mkutano Mkuu leo 

Baadhi ya wanachama wa TASWA wakiburudika katika hotel kubwa mjini bagamoyo ya Kiromo view Hotel jana usiku kutoka kushoto ni Somoe Ng'itu, Hadija Khalili' Zena Chande na Angela Msangi

Shafii Dauda akiwa na dada Asha Muhaji. 

Mmiliki wa blog ya Bongo Staz Mahmud Zubeir kulia akizungumza na Wiliam Chiwango na Salim Said Salim

Mjumbe wa mkutano huo, Rajabu Mhamila 'Super D' akijitambulisha kwa mgeni rasmi

 
Ni wanachama wa TASWA wakisikiliza mada mbalimbali.

Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto  akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete walipokutana katika mkutano mkuu wa Taswa

 

Mmoja wa waandishi wa habari Egbert Mkoko akitoa salamu kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa TASWA. 


Katibu Mkuu wa TASWA Amir Muhando akitoa neno la shuklani kwa wajumbe waliohuzulia mkutano wakati wa kufunga mkutano huo.

Mwanachama wa Taswa Saleh Ally akichangia mada wakati wa mkutano huo.

 
Kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' kushoto  akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys, Ridhiwan Kikwete pamoja na mweka hazini wa TASWA Sultani Sekilo walipokutana katika mkutano mkuu wa Taswa

 Picha na www.burudan.blogspot.com

PATO LA MKOA WA MWANZA LAKUWA KUTOKANA NA SHUGHULI ZA UZALISHAJI KUSHAMIRI.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akiwasilisha Muhutasari wa Taarifa ya Utekelezaji mbele ya waandishi wa habari shughuli iliyofanyika leo kwenye ukumbi wa mikutano Ofisi ya mkuu wa mkoa.

Pato la Mkoa wa Mwanza limekuwa likiongezeka mwaka hadi mwaka kulingana na ongezeko la uzalishaji katika sekta mbalimbali.

Hayo yamebainishwa leo na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo wakati akiwasilishwa muhutasari wa taarifa ya kuhusu utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya disemba 2005 hadi mwezi juni 2012 mbele ya waandishi wa habari ambapo amesema kuwa kulingana na Takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu, wastani wa pato la mwananchi kwa mwaka limepanda hadi kufikia 924,536 kutoka 421,379.

Kwa wastani wananchi wa Mkoa wa Mwanza, wamevuka kiwango cha umaskini uliokithiri kwa watu wanaishi chini ya dola moja kwa siku.

 Pia mkoa wa Mwanza umetajwa kuwa mchangiaji mkubwa wa pato la Taifa ambapo kwa mwaka 2011 Mkoa ulichangia asilimia 9  ukiwa ni Mkoa wa pili ukitanguliwa na Mkoa wa Dar es Salaam uliochangia asilimia 16.6.
UTEKELEZAJI
 Jumla ya mashamba darasa 2,115 yalianzishwa na kuendelezwa Mkoani Mwanza ili kuwafikishia wakulima vijijini maarifa yanayohusu kanuni za kilimo bora.  
Moja ya shamba darasa la Pamba lililoko kijiji cha Solwe, Wilaya ya Kwimba, hali hii imefikiwa mara baada ya wakulima wa eneo hili kupewa maarifa ya jinsi ya kubotesha uzalishaji.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akiwasilisha Muhutasari wa Taarifa ya Utekelezaji mbele ya waandishi wa habari shughuli iliyofanyika leo kwenye ukumbi wa mikutano Ofisi ya mkuu wa mkoa.

MAPINDUZI YA UVUVI: (Ibara ya 41)
           Maelekezo ya Ilani:
Kuweka ulinzi madhubuti dhidi ya wavuvi haramu ikiwa ni pamoja na kukamata vyombo vyao vya uvuvi na kuwatoza fidia kwa mujibu wa sheria.

Uzalishaji:
Jumla ya shilingi billioni 250.2 zimeingia katika uchumi wa wananchi wa Mwanza.
Shilingi bilioni 3.6 zimelipwa kama sehemu ya kodi kwa serikali.

Utekelezaji:
Doria shirikishi dhidi ya wavuvi haramu zilifanyika zikihusisha vikosi vya doria vya Wilaya/Mkoa, jamii ya wavuvi (BMUs) na Polisi.   Watuhumiwa waliokamatwa ni 1,178, Zana haramu zilizo kamatwa ni Makokoro 5,971, Nyavu za Makila 37,980, Nyavu za dagaa (vyandarua) 992, Timba 9,317, kamba za kuvutia Makokoro mita 469,541, Samaki wachanga waliokamatwa ni Sangara wachanga kilo 220,021, sato wachanga kilo 59,596.
Zana haramu zilizokamatwa ziliharibiwa, Samaki wachanga kugawiwa kwenye vituo vinavyolea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, Taasisi za Serikali, kwa idhini ya Mahakama. Aidha, Watuhumiwa wote 1,178  walifikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Moja ya boti za kisasa kwa ajili ya kudhibiti uvuvi haramu, Wilayani Sengerema.
Upatikanaji wa samaki unapungua siku hadi siku hii imetokana na sababu zifuatazo:-
(a)   Uvuvi wa kutumia zana haramu kama vile makokoro, timba, Katuli, na nyavu za macho madogo.
(b)   Kufanyika kwa uvuvi kwenye maeneo ya mazalia ya samaki.
(c)   Kuendelea kupungua kwa kina na maji ya ziwa  Victoria kunakosababisha kuathirika kwa mazalia na makulio ya samaki.

Sensa ya uvuvi iliyofanyika mwezi Agosti, 2010 ilionyesha kwamba matumizi ya zana haramu yamepungua kwa kiasi kikubwa, kwa mfano matumizi ya nyavu za makila (gill nets) zenye macho madogo madogo yalikuwa yamepungua kwa asilimia arobaini na tano (45%).
Mkoa unaendelea kutoa elimu juu ya uvuvi endelevu, hivyo jamii inaombwa kushirikiana na Serikali katika kutokomeza uvuvi haramu.

Maelekezo ya Ilani:
Kuimarisha miundombinu ya uvuvi kwa kujenga mialo, masoko ya kisasa, vituo vya kutotolea vifaranga vya samaki na maabara.

Utekelezaji:
Ukarabati wa mialo tisa umefanyika katika Mkoa kwa mchanganuo ufuatao, Magu 2, Jiji la Mwanza 3, Sengerema 3,  na Ukerewe 1. Na ujenzi wa mialo 2, vituo 2 vya kupokelea samaki, Majengo ya Ofisi 2, Mabanda 2 ya kupokelea samaki yenye meza, Toshari za chuma 2, umefanyika kwa wilaya za  Magu (Kigangama)  na Sengerema (Kahunda), 

UNIQUE MODEL 2012

Mwanamitindo bora wa mwaka 2012 Catherine Masumbiga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Unique Model Photogenic Elizabeth Pertty (kushoto) na Unique Model Talent Vestina Charles mara baada ya kutangazwa kwa mshindi.
Mwanamitindo wa mwaka 2012 Catherine Masumbiga (katikati) amepatikana jana usiku kwenye shindano lililofanyika kwenye Klabu ya New Maisha jijini Dar es Salaam akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa pili Cesilia Michael (kushoto) na mshindi watatu Amina Ayubu.




Washiriki waliongia tano bora.
Washiriki waliongia tano bora.
Majaji wa shindano hilo kutoka kushoto ni Gymkhana Hilal kutoka Paka Wear , Asia Idarous na Martine Kadinda.
Unique Model Talent of the year 2012 Vestina Charles akionyesha uwezowake wa kucheza jukwaani.
Wakitumbuiza mashabiki mapema kabla ya kuingia kuonyesha mavazi ya aina mbalimbali.
Washiriki 12 wa shindano hilo wakiwa wamejipanga tayari kusubiri kutangazwa mshindi.

MASIHI ANGEKUWA MTANZANIA ANGEKUWA NA UJUMBE GANI?

Jesus Christ Superstar … Carl Anderson as Judas in the 1973 film version. Photograph: Ronald Grant Archive


Anna Mghwira
Kwa takiribani miaka 2000 sasa Waumini wa dini ya Kikristo huadhimisha sikukuu hii ya Krismas ulimwenguni kote. Krismas ni tafsiri fupi ya siku ya kuzaliwa Kristo. Kristo mwenyewe hakuwa Mkristo kwa maana kuwa jina Kristo lilipatikana kwa ujio na mauti yake. Yeye alikua Myahudi wa dini ya Kiyahudi.

Tarehe hasa ya kuzaliwa Kristo haifahamiki ijapo majira yanafahamika na yanatofautiana kati ya desturi mbalimbali za Kikristo. Kwa mfano nchi za magharibi ndizo zinazoadhimisha tarehe 25 Decemba kama siku ya kukumbuka kuzaliwa kwa Kristo Yesu. Desturi ya magharibi inafuata tarehe iliyoandikwa mwaka wa 336 baada ya kuzaliwa Kristo.

Desturi zingine za Kikristo huadhimisha siku hii na kuipa maana tofauti, kwa mfano desturi ya Kiothodox huweka mkazo zaidi katika majira ya kuzaliwa Kristo (epiphany) kuliko siku yenyewe ya kuzaliwa. Hawa pia huhesabu mwaka wao mpya tofauti na mwaka wa kalenda tunaotumia unaotokana na desturi za magharibi. Wao huadhimisha siku za majira ya mwaka mpya mwezi wa nne wa kila mwaka.

Aidha kuna tafsiri mbalimbali juu ya ujio na utambulisho wa Kristo. Kwa jinsi ya desturi za Kiyahudi, alikozaliwa Yesu na ambalo ndilo taifa lake la asili, Kristo yaani Masihi bado hajaja kwa maana kwao masihi ni mfalme wa aina ya kidunia.

Yaani ataonekana kwa macho kama mfalme na si kama alama ya imani. Na si kama mwana wa Mungu kama imani ya Kikristo inavyoelekeza. Baadhi ya Wayahudi pia hawamtambui Yesu kama masihi mpaka leo. Kwa hiyo Kristo wa imani na Kristo wa matendo wanaweza kuwa viumbe viwili tofauti.

Kwa jinsi hii maana ya Krismas inatofautina katika misingi hii. Na kwa sababu hii tafisiri mbalimbali za maana ya Kristo huelekezwa katika maana ya ujio wa Kristo zaidi kuliko katika hali ya kimwili ya kuwa mwana wa Yusufu na Maria.

Kwa hiyo Wakristo huadhimisha siku hii kama ishara ya ujio wa mkombozi wa kiimani zaidi. Maana ya ukombozi wenyewe nayo hutofautiana, wengine wakimtazama Yesu kama Mungu aliyefanyika mwanadamu, wengine wakimtazama kifalsafa na kumpa maana kubwa ya mafunzo ya uadilifu ambayo wakristo wanapaswa kufuata.

Katika mkazo wa mafundisho, kuna mambo mengi yanayohusishwa na ujio wa Kristo ulimwenguni. Tafsiri nyingi zimetawaliwa na desturi za magharibi ambazo kwa kweli hazina uasili na ujio wa Kristo, lakini kama ilivyo katika masuala mengine ya jamii, jamii za awali za magharibi zinaonekana katika historia ya binadamu kuwa na mwamko wa kuchukua mambo na kuyafanyia kazi kwa haraka kuliko jamii zingine na kwa hiyo zinamiliki tafisri za mambo mengi hata yale yasiyokuwa na asili yao.

Kwa hili hatuwezi kuzilaumu jamii hizi au watu binafsi kwa juhudi zao. Tunaweza badala yake kutoa changamoto kwa jamii zingine ulimwenguni na hasa za Afrika ambazo zimekuwa nyuma sana katika kuweka mambo yake katika historia ya ulimwengu na hata kwa mambo yake yenyewe.

Kwa sababu hii tafisri kuu ya kile kinachoitwa Ukristo kwa sehemu kubwa ni desturi ya magharibi na tafsiri yao juu ya dini hii. Ni kwa sehemu inafanana na Uislamu pia ambao una destri kuu ya Kiarabu. Kwa hiyo kwa mfano vita kuu ya maneno na ya silaha kati ya Waarabu na Wazungu ina msingi katika dini zao.

Tukio la septemba 11 la mwaka 2001 lilihitimisha kwa sehemu ugomvi mkali kati ya desturi hizi mbili na mpaka sasa vita vya mashariki ya kati vinajengwa katika msingi wa imani na mali – mafuta kwa upande wa Waarabu na matumizi ya mafuta kwa upande wa Wazungu.

Desturi hizi mbili zinawagusa na kuwaathiri Waafrika kwa namna ambayo si rahisi kujitoa katika makucha ya mabwana hawa wawili: Mzungu na Mwarabu. Kwa hiyo kama kuna ukombozi Mwafrika anahitaji ni kujitoa katika makucha ya hawa kwanza, hata katika tafisri za kiimani.

Kisha kuangalia alikotoka na anakotaka kwenda na atakavyokwenda. Bila ya hivyo ukombozi wa Kikristo unaweza kubaki kuwa ukombozi wa kujua mila na desturi za watu wengine na imani zao, na kamwe usimkomboe Mwafrika. Hili ni kweli ikizingatiwa kuwa ukoloni ulikuja na Ukristo na utumwa ulikuja na Uislam! Tunahitaji kutafakari na kuchukua hatua mapema!

Nitoe mfano wa desturi ya Wakristo kusali wakifumba macho. Utani unakuja kuwa kwa kufundishwa kufumba macho Mwafrika alifumbia macho mambo ya msingi kama rasilimali zake na wakati angali amefunba macho, mzungu akachukua kisha akamtawala!

Kuna ukweli kuwa mila na desturi za Kiafrika hazikuwa na utamaduni wa kufumba macho wakati wa kusali. Makabila yetu mbalimbali huendesha ibada za kimila nuruni, katika mwanga ambapo kila mtu anamwona mwenzake. Aidha dini za asili kadhaa huamini na kuapa kwa jua na mwezi, kwa hiyo kufumba macho hakupo!

Nimewahi kushuhudia mwinjilisti mmoja ambaye alifungua macho wakati wa sala akakuta paka anataka kuchukua samaki waliokuwa wametengwa mezani na bila kujali imani yake na ya kuwa yeye ni kiongozi wa dini, alipoona paka ananyemelea samaki alipiga kelele “ paka anachukua samaki” kwa lugha ya kimila aliyotumia alisema”nyau ahora somba nye”!

Yaani paka anachukua samaki wakati wengine wamefunga macho wakisalia chakula!. Tukio hili lilinifanya nitafakari sana kama kweli imani hii inatokana na kufunga macho ama inatakiwa itokane na kufunga rohoni zaidi ili mtu astahimili kuyafumbia macho mambo ya dunia hii yanayopotosha!

Huu ni upande mmoja wa shilingi, upande wa pili ni kuwa wakoloni Wakristo walipofika na kufundisha kufumba macho ya akili wakati wao wakifumbua na kutumbua, ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo na leo ni vigumu sana kuwatoa katika fahamu zetu, katika mipango ya kujiendeleza na kujikwamua na udhalimu waliouanzisha.

Sheria zetu na umahiri wake msingi wake si zetu kwa kweli, ni mambo ya kuiga na kuigiza! Mwafrika hana desturi ya kumweka mkosaji kizimbani, kumhoji maswali akiwa ametengwa na jamii aliyoikosea. Mwafrika wa asili alitumia njia za matambiko kubaini wakosaji, kisha kuwarejesha ama kuwatenga kwa kuwapeleka mbali na makazi asili ili hayamkini wajifunze na kurejea tabia ya utu.

 Tunahitaji kubadilika! Tunahitaji kufanya kazi ya ziada kujua asili yetu na kuirejesha! Wakati mwingine nimefikiri kuwa pengine turudishe utumwa tena wa jinsi yetu ili hatimae tujikomboe.

Mtihani mkubwa wa imani upo hapo: katika kuyaona mambo mabaya yanayofanywa duniani na yenye mvuto machoni kama vile yanafaa lakini kumbe ndiyo yanayotuangamiza.

Kuzaliwa kwa Kristo ni wito kwa Wakristo kuleta amani, upendo na nuru katika ulimwengu. Ni tafsiri nzuri hata kama haitokani na desturi ambayo ningeitaka. Kwa makala hii niwatakie wasomaji wetu Siku kuu njema na niwape mtihani kufikiri kama masihi angetoka afrika angefananaje na ujumbe wake ungekuwa nini??

Kama masihi huyu angezaliwa leo Tanzania angekuwa na sura na umbo gani?
Angewakilisha kundi gani? 
Angeongea lugha gani? 
Angekuwa na imani gani na angejishughulisha na nini?
Kristo alikuja ili wawe na uzima kisha wawe nao tele. Je tunao uzima huo? 
Yaani maisha bora ya kujitosheleza kusherehekea siku kuu hii na zingine zijazo na tunazoweza kuvumbua?
Mungu atubariki tunapokula na kunywa tusile kama wajinga wasio na imani bali kama werevu wenye hekima! Heri ya krismas kwenu Nyote!

Friday, December 28, 2012

WARSHA YA MAAFISA KUTOKA VITUO VYA MIPAKANI KUHUSU USIMAMIZI WA MAZAO/BIDHAA ZITOKANAZO NA BIOTEKNOLOJIA YA KISASA YAFANYIKA LEO JIJINI MWANZA

Naibu Katibu  Mkuu Ofisi ya makamu wa Rais Eng. Ngosi C.X Mwihava akitoa hotuba ya ufunguzi wa Warsha ya Maafisa kutoka Vituo vya mipakani kuhusu usimamizi wa Mazao / Bidhaa zitokanazo na Bioteknolojia ya kisasa inayofanyika leo La-Kairo Hotel Mwanza. 


Mwenyekiti wa Warsha hii Dkt. Julius Ningu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais akitoa maelezo kwa washiriki wa warsha ya Maafisa kutoka Vituo vya mipakani kuhusu usimamizi wa Mazao / Bidhaa zitokanazo na Bioteknolojia ya kisasa ambapo moja kati ya madhumuni ya warsha hiyo ni kukuza uelewa kwa maafisa wa mipakani (forodha/wakaguzi wa mazao/chakula na madawa) kuhusu usimamizi wa matumizi salama ya Biotekinolojia ya kisasa. 


Katika warsha hii washiriki wamepata fursa ya kukumbushwa majukumu yao muhimu kama yalivyoainishwa kwenye mfumo wa usimamizi wa mazingira dhidi ya athari zinazoweza kutokea kutokana na matumizi ya bioteknolojia ua kisasa hapa nchini. 


Vilevile Warsha hii pia ni fursa nzuri kwa washiriki kubadilishana uzoefu katika suala zima la usimamizi wa matumizi ya bioteknolojia ya kisasa hususani bidhaa au mazao ambayo yanaingizwa nchini kupitia katika mipaka yetu, bandari zetu na viwanja vya ndege.


Mtafiti wa Bioteknolojia nchini toka kituo cha Utafiti wa kilimo Mikocheni Dar es salaam Dr Emmarold E. Mneney akitoa darasa juu ya Kwanini Biotechnolojia ni muhimu kwa Tanzania. 


Washiriki takribani 30 kutoka katika wizara za kisekta na taasisi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na washiriki wa Wizara ya kilimo, Chakula na Ushirika Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC tawi la Mwanza, Mamlaka ya Chakula na Madawa TFDA tawi la mwanza, Taasisi ya Utafiti wa madawa ya Binadamu NIMR tawi la Mwanza wameshiriki Warsha hii.


Washiriki wengine ni Ofisi ya Forodha na zile za uthibiti wa mazao na mimea za mipaka ya Sirari, Mutukura, Kabanga na Ngara. 


Washiriki wengine ni Maafisa Afya wa mikoa ya kagera, mwanza, Shinyanga na Mara, washiriki wa kampuni za mbegu, mamlaka ya usimamizi wa mbegu (Tanzania Official Seed Certifying Institute -TOSCI) na bila kusahau wanahabari toka jijini Mwanza.

Naibu Katibu  Mkuu Ofisi ya makamu wa Rais Eng. Ngosi C.X Mwihava akizungumza na vyombo vya habari juu ya Warsha hiyo.. Msikilize kwa kubofya play.
Picha ya pamoja.

IBF YAMPONGEZA BINGWA MPYA WA AFRIKA, GHUBA YA UAJEMI NA MASHARIKI YA KATI



TAARIFA KW AVYOMBO VYA HABARI
TAREHE 27/12/2012

Shirilisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limepongeza bingwa mpya wa uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati, Mtanzania Francis Cheka.

Katika barua yake aliyomtumia Francis Cheka ya tarehe 28/12/2012 Mwenyekiti wa kamati ya Ubingwa wa IBF/USBA Lindsey Tucker alisema "Tunachukua fursa hii kukutakia maisha na mafanikio mazuri kama bingwa wa IBF na kumhimiza kuishi kama bingwa". Cheka atatakiwa kutetea taji lake katika kipindi cha miezi sita kufikia mwezi wa 6 mwakani dhidi ya mpinzani ambaye ana rekodi ya mapambano yasiyopungua 15 na mengi awe ameyashinda hususan mapambano mawili ya mwisho.

Aidha IBF inampongeza bondia Chiotcha Chimwemwe kutoka Malawi kwa ushupavu wake na ushindani mzuri katika pambano hilo lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid katika jiji la Arusha tarehe 26 Desemba, 2012.


Imetolewa na:
Onesmo A.M. Ngowi
Rais
IBF/USBA Afrka, Ghuba ya Uajemi an Mashariki ya Kati



CHIOTCHA AONJA MACHUNGU YA CHEKA

Bondia kutoka Jamhuri ya watu wa Malawi Chiotcha Chimwemwe alionja machungu ya Mtanzania Francis Cheka katika mpambano wao uliopewa jina na “Vita vya Ziwa Nyasa” tarehe 26 Desemba 2012 siku ya Boxing Day jijini Arusha.

Ulikuwa ni mpambano wa mwaka ambao bondia Francis Cheka nusura aupoteze katika raundi ya pili wakati konde zito la kushoto la kapteni Usu kutoka katika jeshi la jamhuri ya watu wa Malawi, Chiotcha lilipompeleka chini na kuinuka kwa msaaada wa kamba za ulingo.
Francis Cheka.

Konde hilo zito lilifungua mpasuko mkubwa katika paji la Cheka na hivyo kuleta wasiwasi kwa mashabiki zaidi ya elfu 10 waliofurika katika uwanja wa Sheikh Amri Abed kumshughudia Cheka akipambana kiume kwelikweli.

Raundi ya kwanza mpaka ya nne Chiotcha alikuwa anamiliki mpambano huo na makonde mazito ya mkono wake wa kushoto kwani anatumia staili ya South Paw inayomlazimu kutanguliza mbele mguu wa kulia.

Ni katika raundi ya sita ambako Cheka aliweza kubadilisha mwelekeo wa mpambano kwa kuanza kumwadhibu Chiotcha na makonde mazito ya kombinasheni yaliyomfanya Mmalawi huyo kumkumbatia bila mafanikio Mtanzania huyo asiyepigika.

Cheka aliwanyanyua mashabiki waliojaa uwanjani wakiongozwa na Mstahiki Meya wa jiji la Arusha, Mh. Gaudence Lyimo alipompiga bila huruma Chiotcha na kumlazimu refarii wa kimataifa wa mpambano huo Nemes Kavishe wa Tanzania kumwonya kutomshika Cheka kama vile anapigana mieleka.,

Juhudi za Chiotcha kujisalimisha kwa kumkumbatia Cheka hazikuzaa matunda kwani aliendelea kupewa mkong’oto na mwana huyo wa Kitanzania aliyejizolea sifa kemkem kwa kuwapiga wapinzani wake.

Mashabiki wengi walinyanyuka katika viti vyao katika raundi ya 12 ya lala salama wakati Cheka alipodhihirisha kweli ni bondia asiyepigika kwa kumpiga makonde mazito kichwani Chiotcha na kumfanya apepesuke kila mara.

Katika mchezo huo ulioandaliwa na kampuni ya Green Hills (T) Investment ya jijini Dar-Es-Salaam inayomilikiwa na bingwa wa zamani wa taifa Andrew George, mabondia wa mapambano ya utanguliizi walikuwa wa ngumi za ridhaa kutoka katika jiji la Arusha.

Mpambano huo ulisimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi akisaidiwa na Kamishna wa TPBC kutoka Jiji la Arusha bw. Roman Chuwa.

Refarii alikuwa Nemes Kavishe kutoka Tanzania wakati majaji walikuwa: Daudi Chikwanje kutoka Malawi, Boniface Wambura kutoka Tanzania na Galous Ligongo kutoka Tanzania.


Imetolewa na

Uongozi, TPBC