ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 27, 2012

MAJUNGU NA MAKUNDI YATAPOTEA NDANI YA CCM TUKIHESHIMU NA KUKIFUATA UTARATIBU ASEMA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA MWANZA, ANTHONY DIALLO


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Anthony Diallo akizungumza kwenye kikao cha Uchaguzi Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Mwanza.
Ni Leo katika kikao cha Uchaguzi cha Halmashauri Kuu ya Mkoa kumchagua Katibu wa siasa na Uenezi, Katibu wa Fedha na Uchumi, pamoja na wajumbe watano wa Kamati ya siasa ya MKOA.






WATEJA WA AIRTEL SASA KULIPIA KODI KWA AIRTEL MONEY

Mwakilishi wa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania bw Saleh Mshoro na  Mkurugenzi wa Biashara za Mashirika wa Airtel  bi Irene Madeje Mlola na Kaimu Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi bwn Allan Kiula kwa pamoja wakionyesha kipeperushi  wakati wa uzinduzi wa Huduma itakayowawezesha wateja wa Airtel kulipa kodi ya mapato na Majengo kwa kupitia Huduma ya Airtel Money. Uzinduzi huu ulifanyika leo katika makao makuu ya Airtel Morocco.

Press Release 

Wateja wa Airtel sasa kulipia Kodi kwa Airtel Money

*Kulipia kodi ya mapato na majengo 

*Airtel na TRA kuwezesha ukusanyaji na Ongezeko la pato 


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayotoa huduma za mawasiliano yenye gharama nafuu zaidi na mtandao wenye wigo mpana leo imezindua mwendelezo wa huduma za Airtel kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwawezesha wateja wake nchi nzima kulipia Kodi kupitia huduma ya Airtel Money. Hii imekuja wakati huduma za pesa kutumia simu zimekuwa zikibadilisha huduma za kibiashara na kuongeza ufanisi.

Kwa kupitia huduma ya Airtel money na ushirika na Mamlaka ya Mapato Tanzania Airtel wateja wa makampuni hayo wataweza kulipia kodi ya mapato na majengo kupitia Airtel Money.

Akiongea wakati wa uzinduzi uliofanyika makao makuu ya kampuni ya Airtel, Mkurugenzi wa Biashara za Mashirika bi Irene Madeje Mlola alisema” Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuleta ufanisi na mapinduzi katika sekta ya mawasiliano nchini. Leo tuna furaha kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwezesha wateja wake kulipa kodi kwa kupitia huduma ya Airtel Money.  Airtel money ni huduma iliyotengezwa kukithi mahitaji ya wateja wetu na hii ni hatua nyingine muhimu kwa Airtel kutumia miundo mbinu tuliyonayo na TRA katika kuhakikisha wanaboresha huduma zao. Sasa walipaji wa kodi wadogo na wakubwa wanalipia kodi zao kwa urahisi wakiwa katika biashara zao na nyumbani”

“Mpaka sasa takribani nusu ya wateja wa Airtel wamejiunga na kutumia huduma ya Airtel money, huduma iliyo rahisi, iliyojitosheleza, salama na nyenye kutoa nafasi kufanya miamala mbalimbali ikiwemo malipo ya bidhaa mbalimbali. Kwa kupitia huduma ya Airtel money inayotoa huduma nyingi zaidi ya kutuma pesa tumeona maisha ya watanzania wengi yakibadilika kila siku na biashara zao kuwa na ufanisi zaidi aliongeza Madeje.”

Kwa upande wake Kamishina Msaidizi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania bw Rished Bade alisema” Tunayofuraha kuzindua huduma yenye kutumia mfumo wa teknolojia ya malipo ya uhakika na salama kwa wateja wetu nchi nzima.

Uzinduzi wa leo ni udihirisho wa juhudi za Mamlaka katika kuongeza uboreshaji katika huduma za malipo ya kodi na ukusanyaji wa mapato.Tunategemea kwa kupitia huduma ya Airtel Money kutawezesha ulipaji wa kodi kwa wakati na kuwahamasisha watanzania wengi zaidi kulipia kodi zao za mapato na majengo. TUnategemea kuona ongezeko kubwa la wafanya biashara wadogo na wakati ambao leo hii wanalipia malipo ya kodi kwa kupitia maofisi na vituo mbalimbali vya kodi nchi nzima. 

Akiongelea kuhusu njia ya kulipia kodi hizo kwa njia ya simu Meneja Uendeshaji Airtel Money Asupya Naligingwa alieleza”Kulipia kodi ya majengo au mapato mteja wa Airtel atatakiwa kupiga namba  *150*60#*  kisha

   1. Atachagua Lugha
   2. Atachagu malipo ya bili 
   3. Lipa Bili
   4. Atachagu “JIna la fumbo” *MAJENGO” 
   5. Ingiza kiasi cha fedha unachotaka kulipia
   6. Ingiza neno la siri
   7. Ingiza namba ya akaunti ya Mamlaka ya Mapato (TRA) kisha bonyeza OK
   na utapokea meseji(SMS)itakayothibitisha malipo yako ”

Huduma ya Airtel Money service inayopatikana kwa kupiga  *150*60# inawawezesha
wateja kulipia huduma mbalimbali zikiwepo kama vile za kulipia bili za maji na umeme,bidhaa na huduma mbalimbali kama vile  bima,kununua muda wa maongezi, miamala ya huduma za kibenkiikiwemo kuweka na kupokea kutoa na vile vile kulipia huduma nyingine nyingi.

Airtel Money ni huduma inayopatikana masaa 24, siku 7 za wiki kutoka katika simu na ni salama ya uhakika na rahisi kutumia. Kinachohitajika ni kitambulisho na usajili wa simu yako ili kuweza kupata huduma hii katika maduka na mawakala wote waliopo nchi nzima. 

*Mwisho

MATUMLA - MKENYA NDANI YA MTWARA HAPATOSHI

Bondia Rashid Matumla akipima uzito tayari kumkabili Mkenya.

Patrik Amot wa Kenya akipima uzito tayari kumkabili Matumla.

Maofisa wa TPBO wakitafakari masuala mbalimbali baada ya zoezi la upimaji afya kwa mabondia kufanyika mjini Mtwara.
Bondia Rashid Matumla wa Tanzania na Patrik Amot wa Kenya wanategemea kupanda ulingoni kesho katika ukumbi wa Makonde mkoani Mtwara.

Mabondia wote wamepima na kuwa na afya njema na wote kuwa katika uzani sawa wa kilo 73 kila mmoja.zoezi zima la upimaji liloendeshwa na katibu mkuu wa TPBO ibrahim kamwe na dr madono lilienda vema.

Pia kutakuwa na mapambano ya utangulii kati ya  bakari mohamed wa mtwara na abdala mohamed wa dsm katika pambano la ubingwa kg57

Pia kutakuwa na mapambano mengine mengi ya utangulizi kati ya mabondia toka Black Mamba ya Mtwara na mabondia toka Dar es salaam. kama Haruna Mnyalukolo atacheza na Ashraf Abdalah, Issa Matumla (mtoto wa Rashid Matumla) atacheza na Hamis Mtupeni,Hamis Ali Mkupa wa Mtwara atacheza na Ide Mnali katika pambano la raundi nane.

Friday, October 26, 2012

EID AL ADHA

Ni kwa ndugu zangu waislamu wote akiwemo kaka yangu wa dhati Adam G. Sengo.

Thursday, October 25, 2012

BREKING NEWS: POLISI WAWANASA WAUAJI WA KAMANDA BARLOW MWANZA

Manumba akitaja majina ya wahusika pembeni kushoto ni IGP Mwema.

Majina ya watu watano  wanaotuhumiwa kuhusika moja kwa moja na kifo cha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Leberatus Barlow yametajwa rasmi leo jijini Mwanza.


 Kabla ya hapo DCI Manumba alitoa taarifa juu ya uchunguzi uliofanyika na kikosi chake na kupelekea kunaswa wahusika hao... Msikilize kwa kubofya hapo juu kwenye play.

Akitaja majina hayo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania IGP Said Mwema, MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba,  amesema kuwa simu iliyoporwa ya mwanamama ambaye alikuwa akisindikizwa nyumbani na marehemu ndiyo imesaidia kukamilisha upelelezi huo hatimaye wahusika kukamatwa...

Majina ya wahusika hao kuwa ni Muganyizi Michael Peter (36) ambaye inatajwa kuwa ndiye aliyemuua Barlow, Chacha Waitare Mwita (50), Magige Mwita Marwa (48),  Buganzi Edward Kusuta pamoja na Bhoke Marwa Mwita (42) ambao wote wamekatwa katika jiji la Dar es Saalm.

Damu ya aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza Barlow
Alisema Kikosi kazi cha upelelezi kilichokuwa chini yake  Manumba kilijigawa kwenye makundi matatu moja ni lile la Ukamataji, Mahojiano na lingine la interejensia huku wakitumia njia ya sanyansi kwa kufuatia mitandao ya simu.

Kukamatwa kwa watuhumiwa hao wa dar na wale wa Mwanza kunafanya jumla yao kuwa 10 na bado jeshi linasaka wengine.  Lakini hakuna sababu iliyotokana na mauaji hayo ambayo imeelezwa mpaka sasa na jeshi hilo.

Wengine watano wanaoshikiliwa kwa usalama ni pamoja na Doroth Alicia Lymo (42) kabila mchaga mwalimu wa shule ya msingi Nyamagana  mkazi wa Kitangili Minazi mitatu Mwanza ambaye alikuwa na marehemu siku ya tukio akisindikizwa,  Felix Felician Minde (50) kabila mhaya  mfanyabiashara mkazi wa Lumala na  Fumo Felician Minde (46) kabila mhaya mfanyabiashara mkazi wa kona ya Bwiru.

Wengine katika orodha hiyo ni  Bahati Agustino Lazaro kabila Muha Mfanyabiashara mkazi wa Nyakabungo na Amos Weibe Magoto (Bonge) ambaye ndiye aliyekutwa na simu ya mwalimu Doroth


Liberatus Barlow aliuawa Oktoba 13 mwaka huu, saa 8 usiku kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika eneo la Minazi mitatu huko Kitangiri wakati alipopita kumsindikiza Mwalimu Dorothy Moses nyumbani kwake kutoka katika kikao cha harusi kilichofanyika Mtaa wa Rufiji. moja  


Msikilize kwa kubofya hapa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania IGP Said Mwema akizungumzia juu ya source ya mauaji..
Baadhi ya Polisi wakifuatilia kinachojiri ndani ya ukumbi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza jioni ya leo.



MSAADA JAMANI....


A.aleykum kaka,

Mimi  Rahma T. Ali, mwananfunzi wa International Medical and Technological University (IMTU), naomba unisaidie kuweka tangazo langu katika blog yako.

Nimepoteza wallet  yangu maeneo ya Muhimbili hospitali. Wallet hiyo ilikuwa na fedha kidogo (15,000 Tsh) na “documents” zangu muhimu zifuatazo. 1. ATM cards mbili (2 ) za NBC,  2. Kitambulisho cha Bima ya afya (NHIF), 3. Kitambulisho cha ukaazi cha Zanzibar  4. Kitambulisho cha uwanafunzi cha IMTU na 5 Picha aina ya passpot size mbili (2).

Hivyo basi kwa heshima kubwa, naomba mtu yoyote atakae iona/okota wallet yenye vitu hivyo au baadhi ya vitu hivyo awasiliane nami kwa  +255659891110 au aviwasilishe idara ya masikio, pua na koo "Department of ENT" hapo muhimbili hospitali.

Natanguliza shukrani zangu za dhati

Mimi Rahma, T. Ali

ZIJUWE PASSWORD 25 ZILIZOTOMIKA SANA 2012


Miaka ya sasa suala la kuingiliwa mawasiliano binafsi kwenye mitandao limekuwa likiwaathiri wengi, kiasi kwamba wengi wamejikuta kazi zao za kiofisi zikiingiliwa, siri zao binafsi zikivuja mitaani au pengine kupoteza kabisa akaunti zao za email, na mitandao mingine kutokana na hackers kuzinasa password zao kisha wakazibadili nao watumiaji wakajikuta hawawezi kusaini in kama awali.


YAFUATAYO NI MANENO 25 YALIYOTUMIKA KAMA PASSWORD NA WATU WENGI KWA MWAKA 2012 KWA MUJIBU WA WADADISI WA YAHOO.


1. password
2, 123456
3. 12345678
4. abc123
5. qwerty
6. monkey
7. 
letmein
8. dragon
9. 111111
10. baseball
11. iloveyou
12. trustno1
13. 1234567
14. sunshine
15. master
16. 123123
17. welcome
18. shadow
19. ashley
20. football
21. jesus
22. michael
23. ninja    
24. mustang
25. password1 
Je wataka kuwa na Password isiyofojika? 
Hapa kuna vidokezo:
- Tumia herufi ya kwanza kwa kila neno la shairi au mstari kutoka katika wimbo. Kwa Mfano, "Hey, I just met you... And this is crazy... But here's my number... So call me maybe" herufi za mwanzo ni "hijmyaticbhmnscmm."  Of course, itakupasa kuimba kichwani kila mara unapotaka ku-log in.
- Changanya maneno mawili, mfano "hungrydog" au "choppywater." Na ili kuweka usalama zaidi, tenganisha maneno hayo kwa kuweka alama au namba au kiwakilishi chochote kwenye keyboard ya komputa yako. Hivyo badala ya kuandika "hungrydog," tumia "hungry$d0g."  Ni mifano tu mengine fanya ubunifu ila kumbuka kuweka kumbukumbu kichwani mwako.

HII NDIYO HALI HALISI KWA BARABARA ZA NDANI KILIMAHEWA

Wakati mkandarasi aliyepewa tenda na halmashauri ya jiji la Mwanza akiendelea na ujenzi wa daraja la Big Bite Kilimahewa na ukarabati wa njia mbadala kwaajili ya kuunganisha eneo hilo na barabara ya kuelekea Nyasaka na maeneo mengine ukiendelea...hali ni tete kwa barabara  nyingi zilizo ndani ya mji huo.

Mifereji ipitishayo maji yatiririkayo ni midogo na mingi imeziba hivyo maji yanakatiza katikati ya barabara na kuharibu miundo mbinu.

Katika maeneo mengine maji yamatengeneza madimbwi makubwa katikati ya barabara.

Ni kama hakuna barabara vile....

Barabara zinapogeuka kuwa.... 

Wenye nyumba zao maeneo haya na kuta za nyumba zao....

Mbele ya shule ya chekechea...

Yahitaji mahesabu wakati wa kuvuta hatua...

Mbele ya mjengo

Mbele ya maduka.... kwenye barabara hizi zenye kilio cha miaka nenda rudi..

Wednesday, October 24, 2012

AIRTEL YAWAZAWADIA 500% BONUS YA MUDA WA MAONGEZI KWA WATEJA WAKE.


Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania Sam Elangalloor akiongea  na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa promosheni ya “Jipatie Mara 5” inayowawezesha wateja wa Airtel kupata mara tano ya  wastani wa kiwango cha pesa watakayotumia kila siku  . Uzinduzi huo umefanyika leo katika ofisi za makao makuu ya Airtel morocco. Kushoto ni Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Beatrice Singano Mallya na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko Cheikh Saar.

Waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania Sam Elangalloor akiongea  wakati wa uzinduzi wa promosheni ya “Jipatie Mara 5” inayowawezesha wateja wa Airtel kupata mara tano ya wastani wa kiwango cha pesa watakayotumia kila siku ikiwa ni sawa na 500% bonus ya muda wa maongezi. Uzinduzi huo umefanyika leo katika ofisi za makao makuu ya Airtel morocco.
Mkurugenzi wa Masoko Cheikh Saar akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa promosheni ya “Jipatie Mara 5” inayowawezesha wateja wa Airtel kupata mara tano ya wastani wa kiwango cha pesa watakayotumia kila siku. Uzinduzi huo umefanyika leo katika ofisi za makao makuu ya Airtel morocco. katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania Sam Elangalloor akifatiwa na Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Beatrice Singano Mallya


Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania Sam Elangalloor (katikati) pamoja Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Beatrice Singano Mallya (kushoto)  na Mkurugenzi wa Masoko Cheikh Saar (kulia) kwa pamoja  wakionyesha moja ya vipeperushi vya promosheni mpya ya “ Jipatie Mara “ wakati wa uzinduzi wa promosheni mpya inayowawezesha wateja wa Airtel kupata mara tano ya muda wa maongezi kutokana na  wastani wa kiwango cha pesa watakayotumia kila siku. Uzinduzi huo umefanyika leo katika ofisi za makao makuu ya Airtel morocco.
Press Release
Airtel yawazawadia 500% bonus ya Muda wa Maongezi kwa wateja wake
·         Wateja wa Airtel kupata mara tano ya muda wa maongezi
·         Hakuna haja ya kujiunga  kwenye “ Jipatie Mara 5”
Dar es salaam Octoba 2012 Kampuni ya simu za mikononi ya Airtel leo imezindua promosheni mpya kabambe itakayowazawadia wateja wake nchi nzima. Promosheni hii ijulikanayo kama “Jipatie Mara 5” itawawezesha wateja wa Airtel kupata MARA TANO  ya wastani wa matumizi ya kupiga simu kwa siku nzima.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo Mkurugenzi wa Airtel Sam Elangalloor alisema” Airtel tunayofuraha kuwazawadia wateja wetu nchi nzima mara tano ya wastani wa kiwango cha pesa watakayotumia kila siku promosheni hii ya “Jipatie Mara 5”.  Promosheni hii itawazawadia wateja wa Airtel mara 5 ya matumizi yao kama bonus ya muda wa maongezi itakayowawezesha kupiga simu kwenda namba yoyote ya Airtel kwa siku hiyo , hii ni sawa na asilimia 500 ya bonus.

”Tumefanya hivi ili kuendelea kuboresha huduma zetu na pia kuendeleza kudhibitisha dhamira yetu ya  kuwapatia wateja wetu nchini nzima uhuru wa kuongea  aliongeza Elangalloor .”

Akifafanua juu ya promosheni hiyo Mkurugenzi wa kitengo cha Mawasiliano Airtel Beatrice Singano Mallya alisema” kila mteja wa Airtel tayari ameshaunganishwa katika promosheni hii, kinachotakiwa kufanya ni kupiga simu upate bure salio mara 5 ya wastani wa matumizi yako ya siku kadri mteja anavyotumia simu yake kwa kupiga simu ndivyo anajipatia  nafasi  zaidi ya kuzawadia asilimia 500 ya bonus ya muda wa maongezi

“Jipatie Mara 5” ni promosheni kwa ajili ya wateja wa malipo ya awali, kila mteja atapata ujumbe utakaomjulisha wastani wake kwa siku na kisha kupokea ujumbe mara atakapopokea asilimia 500% kutoka Airtel. Kwa maelezo zaidi juu ya  huduma hii piga 0783001001 bure na kuunganishwa moja kwa moja na taarifa mbalimbali za huduma zetu”aliongeza Mallya.

Airtel inaendelea kuboresha huduma za mawasiliano nchini.  kwa kupitia huduma ya Airtel money, Airtel imewawezesha watanzania kupata  huduma za kifedha kirahisi  katika maeneo mbalimbali nchini. Kwa kuthibitisha uwezeshaji wa upatikanaji wa huduma za kifedha Airtel imewawezesha wateja wake kutuma na kupokea pesa chini ya shilling 100,000/= bure bila makato yoyote. Vile vile Airtel imeendelea kupanua zaidi  huduma za internet kwa  kuwezesha miji zaidi ya 30 nchini kupata internet yenye  kasi ya  3.75G .

PAMBA YAICHAPA POLISI MARA 3-2 DIMBA LA CCM KIRUMBA


NA ALBERT G. SENGO:MWANZA

Ikitumia Vyema uwanja wake wa nyumbani Pamba Fc ya Mwanza leo imeanza vyema  mchezo wake wa kwanza kundi C ya Ligi ya soka Daraja la kwanza ya Tanzania bara kwa kuichapa Polisi Mara kwa mabao 3-2.

Magoli ya Pamba yalifungwa na Mathayo William dakika ya 3, Shahban Makoba dakika ya 61 na Mashaka Kiumba dakika ya 70.

Upande wa timu ya Polisi Mara magoli yake yalifungwa na Kaichi Kaichi kwenye dakika ya 4, na Athumani Matutu aliyefunga bao la pili dakika ya 90.

Makocha wa timu zote mbili walipata fursa kuzungumza na Sports Xtra juu hali ya mchezo na nini matarajio kwa mechi zinazofuata za kundi C, Ligi soka Daraja la kwanza Tanzania bara. 


Msikilize Wa kwanza ni kocha wa timu ya Pamba ya jijini Mwanza Ibrahim Mulumba..

Naye kocha wa Polisi mara Hafidh Salim amewaumu wachezaji wake kuingiwa kitete na mchezo huo wakiacha maelekezo yake na kucheza kila mmoja kimpango wake... 

MWISHO

KWA WANAOPENDA FASHENI TATOO ZIMEPITWA NA WAKATI MAMBO YOTE BAGELHEAD (MTUNO USONI)



Ni fasheni ambayo ipo kwa muda mrefu sasa na imekuja juu mara baada ya Makala kuhusiana na mtindo huo mpya kuonyeshawa kupitia Chanel ya National Geographical ya nchini Japan ndipo hamasa ya wengi ikazidi.

Ilikuupata mtuno Unachomwa sindano yenye dawa (injecting saline) kwenye paji la uso ikiwa imeungangishwa na drip inayofunguliwa taratiiiibu isilete madhara.....

Mtuno unaendelea kujaaa..

Mtuno ukishajaa unauwezo wa kuuremba unavyotaka bila bila kupata maumivu...

Dekshia mambozZ.

Watu wanapenda kuwa exceptional aka kuwa na udiferenti... 

Donati usoni likikolezwa...

Wanachoma sindano yenye dawa cc400 ili kutengeneza mtuno wa duara, mtuno ukishajitokeza unatumia dole gumba kutengeneza mashimo (kama inavyokuwa kwa wavimbao miguu lakini hapa mbonyeo hudumu hadi mwisho)

Fasheni hii inadumu kwa muda wa saa 16 hadi 24 kurejea katika hali ya kawaida. 

Mituno na mibonyeo ya dole gumba mara baada ya huduma.
Fasheni ndani ya kumbi za burudani wabongo mUpO?.