ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 20, 2012

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTAMADUNI ATEMBELEA MAZOEZI YA MISS UTALII DODOMA 2012


Naibu Waziri wa maliasili na Utalii Mh. Lazaro Nyalandu alipotembelea Mazoezi ya Miss. Utalii Dodoma juzi na kuwapa nasaha warembo wanaoshiriki mashindano hayo yatakayofanyika Tarehe 09 November, 2012 katika ukumbi wa Royal Village Hotel.


Friday, October 19, 2012

TIGO YAZINDUA MAJUKWAA YA UJASILIAMALI NCHINI

Mwezeshaji wa Jukwaa kutoka Tigo Makao makuu  Hubert Luis  akifungua Jukwaa hilo ndani ya Hoteli ya Gold Crest Mwanza kwa niaba ya Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutirrez.
Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo leoimezindua majukwaa kwa ajili ya wajasiliamali wapya nchi nzima kama sehemu ya wajibu wake katika kusaidia na kukuza wajasiliamali wadogowadogo na wakati nchini.

Lengo la majukwaa hayo ni kuwaleta pamoja wajasiliamali na mashirika ya kibiashara kutoka sekta mbalimbali ili kupanua mitandao yao na kunufaika na suluhu mpya za mawasiliano kwa biashara. Biashara ndogo na za kati zitanufaika na warsha, mafunzo na mazungumzo ya mada zinazohusu masoko, menejimenti, fedha na uzalishaji.
Ridhiwani Kassimu mtaalamu wa biashara ndogondogo na kati kutoka benki ya NBC akitoa somo.
Pamoja na kufafanuwa kuhusu vifurushi maalum vya kiteknolojia vya mawasiliano, bwana Ridhiwani Kassimu mtaalamu wa biashara ndogondogo na kati alitoa somo kwa wajasiliamali na waendeshaji biashara kupitia mada ya "Jinsi ya kupata mitaji kwa biashara yako"
Hapa wadau walielimishwa madhara ya kuomba mkopo kwa muda mrefu, Ushauri kwa wafanysbiashara kuhusu mikopo, Masuala gani yanawanyima wajasiliamali mikopo, Vihusishi gani vinaisababisha benki kuwa rahisi kutoa mkopo pamoja na Miiko ya mjasiliamali anayopaswa kufuata wakati wa uombaji mkopo.

Mc wa Jukwaa hilo Costantine Magavila akitoa ufafanuzi.

Utambulisho kwa wadau muhimu wa Togo Kanda ya Ziwa.

Huyu ni Injinia wetu...si mtu wa maneno bali vitendo zaidi

Miongoni mwa suluhu bunifu za kibiashara zitakazozinduliwa kwenye majukumu haya ni vifurushi maalum vya kiteknolojia vya mawasiliano, 'Tigo TELCO Solutions', vinavyolenga kuwa sehemu moja pekee yakukidhi mahitaji yote ya mawasiliano ya kibiashara.

Vifurushi hivi vitatoa mbinu za kuwapa wajasiliamali ufanisi kwenye matumizi na kuwawezesha kupanga mipango yao ya kibiashara ndani ya bajeti zao. Pia inawapa wajasiliamali fursa kuwasiliana na wadau kwa unafuu zaidi pamoja na chaguo mbilimbali za kulipia bili.

Wadau mbalimbali wakiendelea kupata vitafunwa huku wakipokea somo kutoka Jukwaa la leo lililofanyika kwenye Hoteli ya Gold Crest mkoani Mwanza.

Jukwaa la leo limefanyika hapa Hoteli Gold Crest mkoani Mwanza. majukwaa mengine yatafanyika kwenye miji mingine Tanzania hadi mwisho wa mwaka hivyo wadau mikoa mingine kaeni tayari twaja.....

Wadau mbalimbali wakiendelea kupata vitafunwa huku wakipokea somo kutoka Jukwaa la leo lililofanyika kwenye Hoteli ya Gold Crest mkoani Mwanza.

Burudani nayo haikukosa nafasi kwani vijana wa Rock city Band walimwaga raha....

Mc wa Jukwaa hilo Costantine Magavila akisalimiana na wadau walioalikwa kupokea somo.

Changamsha changamsha ya ChiaZZz kwa wadau wa jukwaa la leo lililofanyika kwenye Hoteli ya Gold Crest mkoani Mwanza.

ChiaZZz ya Leanne Martin-Pollock ambaye ni PR wa Trinity Promotion Ltd na wana habari Mwanza.

Huduma ziliboreshwa toka mlangoni.

Menyu ya mtikisiko dizaini ....

Baada ya jukwaa kumalizika Rock city Band walisababisha...

Tigo huduma.
Tigo ilianza biashara 1994 kama mtandao wa kwanza wa simu za mkononi Tanzania. Sasa inapatikana katika mikoa yote 26 Tanzania bara na Zanzibar. Tigo imejitahidi kuwa na ubunifu katika uendeshaji wa huduma zake za simu nchini Tanzania kwa kutoa huduma zenye gharama nafuu katika mawasiliano mpaka katika kutoa huduma za internet zenye kasi na huduma za fedha kwa njia ya simu kupitia Tigo Pesa.
Wadau wakijisevia.
Tigo ni sehemu ya Millicom International cellular S.A (MIC) na hutoa huduma za simu za mikononi kwa gaharama nafuu na inapatikana maeneo mengi kiurahisi kwa wateja zaidi ya milioni 30 katika masoko 13 yanayoibuka Afrika na Amerika ya Kusini.

KUFUKUZA KUKU: NANI ALISTAHILI NDEGE HUTU?



Mwanadada ambaye ni mshiriki kutoka Bandari ya Dar es salaam Bi. Oliver Ngumuo ndiye alitawazwa kuwa mshindi wa mchuano huu... na kuzawadiwa kuku wake ndani yaMichuano ya sita ya Bandari iliyofanyika ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo ambapo pia zawadi mbalimbali kama fedha na vikombe kwa washindi vilitolewa.

MICHUANO YA SITA YA BANDARI TANZANIA YAMALIZIKA LEO JIONI JIJINI MWANZA.

Michuano ya sita ya bandari imemalizika leo jijini Mwanza kwa washiriki mbalimbali kutunukiwa nishani zao, makombe na  zawadi za fedha.


Michuano hiyo kabla ya kufungwa iliambatanishwa na maandamano kwa wawakilishi wa timu zote kutembea umbali mfupi hadi uwanja wa CCM Kirumba hatimaye kupita mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga.

Timu ya Bandani Dar es salaam ikipita kwa maandamano mbele ya mgeni rasmi.

Timu ya Bandari Tanga.

Bandari Mtwara.

Bandari za Maziwa. 

Mshindi wa mbio za kufukuza kuku Oliver Ngumuo kutoka Bandari ya Dar es salaam akiwa na zawadi yake.

Timu ya Bandari za Maziwa. 

Timu ya Bandari ya Tanga.

Mashabiki nao hawakuwa nyuma katika kusapoti timu zao.

Katika mchezo wa kuvuta kamba Bandari Tanga (kulia) waliibuka kidedea kwa kuwazidi ubavu timu ya Bandari za Maziwa Makuu (kushoto).

Timu ya Bandari Dar es salaam ndiyo iliyotia fora kwa kunyakuwa vikombe vingi hapa Mh. Baraka Konisaga akikabidhi kombe la ubingwa kwa timu hiyo upande wa soka.

Timu ya Bandari Dar es salaam ndiyo iliyotia fora kwa kunyakuwa vikombe vingi hapa Mh. Baraka Konisaga akikabidhi kombe la ubingwa kwa timu hiyo upande wa mpira wa pete.



Timu ya Bandari Dar es salaam ndiyo iliyotia fora kwa kunyakuwa vikombe vingi hapa na hapa wakisherehekea tuzo na makombe waliyonyakuwa.

Timu ya pili kwa ushindi wa jumla ni Bandari Tanga.

MWANZA CITY YAONDOKA LEO KWENDA DODOMA KUSHIRIKI SHIMISEMITA INAYOANZA RASMI KESHO

Diwani wa kata ya Butimba Dismas Makungu kwa niaba ya Mstahiki Meya wa jiji hilo, akikabidhi bendera ya jiji kwa Afisa Utamaduni wa jiji la Mwanza Mama Makenke kwaajili ya ushiriki michuano ya SHIMISEMITA inayotarajiwa kuanza rasmi kesho mjini Dodoma. 

Timu hiyo inaondoka leo kuelekea mjini Dodoma kwaajili ya michuano hiyo inayoshirikisha michezo mbalimbali kama Football, Netball na michezo mingine ya ndani kama vile Bao, Kuvuta kamba na Karata. 

Mwanza City team ikiwa na jumla ya wachezaji 22, kocha wawili na kiongozi mmoja pia imekabidhiwa bango la Mwanza.

Diwani wa kata ya Butimba Dismas Makungu kwa niaba ya Mstahiki Meya wa jiji hilo, akikabidhi mpira wa mazoezi kwa kikosi cha timu ya mpira wa miguu cha Mwanza city Amidu Juma, kwenye makabidhiano yaliyofanyika mchana huu katika viwanja vya Halmashauri ya jiji la Mwanza.
  
 Diwani wa kata ya Butimba Dismas Makungu kwa niaba ya Mstahiki Meya wa jiji hilo, akikabidhi mpira wa mazoezi kwa kocha Rehema Menzukwa wa kikosi cha netiboli cha Mwanza city, katika  makabidhiano yaliyofanyika mchana huu kwenye viwanja vya Halmashauri ya jiji la Mwanza.


Kikosi cha timu ya mpira wa miguu cha Mwanza city.


Kikosi cha netiboli cha Mwanza city


Mkuu wa msafara huo ambaye ni Afisa utamaduni wa jiji la Mwanza Mama Makenke akizungumza na waandishi wa habari ameahidi kurudi na kombe la ushindi wa kwanza kupitia michezo hiyo ya Serikali za mitaa (Shimisemita) akisema sababu kuu ya kujiamini kwake ni ushiriki vyema wa timu hiyo kwenye michuano ya Polisi jamii iliyomalizika hivi karibuni kwa wilaya ya Nyamagana ambapo timu hiyo ilitwaa kombe ikizigalagaza baadhi ya timu kali za jiji la Mwanza.

SAFARI KANDO KANDO YA ZIWA VICTORIA

Ni safari kando kando ya ziwa Victoria kushuhudia harakati mbalimbali za ukuzaji uchumi pamoja na ustaarabu wa maisha.
Wavuvi wa biashara ya jumla ya zao la samaki eneo la Migori nchini Kenya.

Mtumbi wa wavuvi kandokando ya ziwa hili mara baada ya upakuzi kufanyika hapa ukingoja kupakiwa barafu kisha kuelekea ziwani kubeba samaki.
Kituo cha ununuzi wa zao la samaki Kisumu nchini Kenya.

Kibao elekezi.

Samaki wafugwao.

Samaki wafugwao.

Mamba wa kufugwa, kuna baadhi ya maeneo kando kando ya ziwa Victoria yana sifa kuwa na mamba wengi idara za mali asili imeweka uataratibu kukusanya mamba wanao ingia maeneo ya wavuvi na kuwafuga eneo maalum kwa usalama wa wavuvi badala ya kuwauwa mamba hao.  

 
Eneo la upimaji zao la samaki kwaajili ya biashara viwandani.

 
The Kingdom.

 
Ni moja kati ya sanamu zilizopo pembezoni mwa kanisa la kwanza la wamissionari waliofika katika mji huu ulio kando kando ya ziwa Vistoria.
Ni sanamu ya pili iliyo pembezoni mwa kanisa la kwanza la wamissionari waliofika katika mji huu ulio kando kando ya ziwa Vistoria.
Kandokando ya ziwa victoria na shughuli za uvuvi.

 
Matayarisho ya wavuvi na shughuli za uvuvi.