ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 22, 2012

CHEREKO LA 'SEND OFF' YA VERONICA STIMA LAFANA, TABORA

Bibi Harusi mratajiwa Veronica Stima akiwa amesindikiza na kaka yake John Stima kuingia katika ukumbi kwa ajili ya sherehe ya kumuaga (Send Off) iliyofanyika Student Centre, Tabora. Ambapo Harusi yake ni Jumamosi Septemba 22, 2012.

Baba na mama yake mzazi Veronica Stima (kutoka kulia) wakicheza nyimbo ya kikabila la Kifipa.
Wakwe wa bibi harusi mtarajiwa wakiingia ukumbini kwa madaha.
Bi Harusi mtarajiwa Veronica Stima akiwa na kaka na dada zake aliomsindikiza katika sherehe yake ya send off iliyofanyika ukumbi wa Student Centre, Tabora.
Bibi Harusi Mtarajiwa Veronica Stima akimlisha mtarajiwa wake Bw. Allen Mnene
Wachanga nao hawakuwa nyuma kuonyesha umoja wao na ule wimbo wao wa kushikana mikono.

Bwana harusi mtarajiwa Allen na mkewe mtarajiwa Veronica Stima wakienda mbele kwa ajili ya utambulisho.
...akilishwa keki na mtarajiwa wake
Bibi harusi mtarajiwa akiaga wazazi wake, kujitayarisha kuungana na mwenzake
...hapa bibi harusi mtarajiwa alikuwa akitoa keki kwa mama mkwe wake mtarajiwa huku kaka yake akiwa amemsindikiza.
Mzee Prosper Stima ambaye ni baba bibi harusi mtarajiwa akitoa machache.

Mama Catherine Stima ambaye ni mama mazazi wa bibi harusi nae alipata wasaa wa kutoa machache kwa mwanae.

Kaka mkubwa John Stima akiongea machache kabla ya kumkabidhi dada yake kwa shemeji zake. Alisema, 'Nawakabidhi dada yangu mpendwa, hana hata doa... nawaombeni msije mkanyanyasa'.
...mara baada ya kuongea machache kaka mkubwa alikabidhiwa begi la nguo za bibi harusi, tayari kwa maandalizi ya harusi.

Aha... Bwana na Bibi Cathbert Angelo nao walikuwepo kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa.
Bibi harusi mratajiwa (wapili kutoka kulia) akiwa na dada zake.

Muda wa kupata show ulifika na mambo yalikuwa kama unavyopna mwenyewe.
Picha ya kumbu kumbu kwa wake na watoto wao. Nguzo zote za shughuli hiyo zimedizainiwa na na kushonwa na mwanamitindo Manju Msita

WAKAZI WA MBEYA WAFURIKA TAMASHA LA SERENGETI FIESTA SOKOINE STADIUM


Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Linah akiimba kwa hisia jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012 kwenye uwanja wa Sokoine,Mkoani Mbeya.


Mashabiki kibao.

Wasanii wa Filamu hapa nchini Aunt Ezekiel,Wema pamoja na Shilole wakiwasikiliza mashabiki wao wanataka nini.

Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Diamond akiwaimbisha mashabiki na wapenzi wa muziki huo waliojitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta,kwenye uwanja wa Sokoine,mkoani Mbeya.

 Shemejiii....Wema Sepetu akiwachetua kidogo wapenzi wa mambo ya filamu.

Msanii wa bongofleva kutoka THT,Barnaba akiwaimbisha mashabiki wake usiku huu kwenye tamasha la serengeti fiesta 2012 ndani ya uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.




Wadau wakifuatilia tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea usiku huu.

Watu kibao ndani ya sokoine usiku huu.

Mmoja wa wasanii mahiri wanaotikiza kwenye anga ya muziki wa bongofleva hasa katika miondoko ya R&B,Ben Paul akikamua vilivyo jukwaani huku mashabikiwa wake wakishangilia kwa shangwe. 

Pichani kulia ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya  Mh. Dkt. Norman Sigallah akimtaja mshindi wa gari aina ya Vits itolewayo na kampuni ya Push Mobile,ikiwa ni sehemo mojawapo ya mchakato wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012,anayeshuhudia ni Meneja masoko wa Push Mobile Rugambo Rodney na kulia ni Chiku Saleh kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha ,ambapo  katika bahati nasibu hiyo iliyochezeshwa,aliyeibuka mshindi ni   Eva B Mgovani. 

ni full kujiachi tuu ndani ya uwanja wa sokoine usiku huu.
Pichani kati ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya  Mh. Dkt. Norman Sigallah akiwa katika picha ya pamoja na Meneje vipindi wa Clouds FM,na mdau mwingine.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya anaefananishwa na mashabiki wake kama Ray C,aitwaye Recho kutoka THT akitumbuiza jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012 
Mashabiki wakishangilia vilivyo usiku huu,huku makamuzi ya wasanii yakiendelea jukwaani.
Msanii wa bongofleva anaetikisa kwa nyimbo kadhaa ikiwemo,Mama halima,Aifora na nyinginezo akiwaimbisha mashabiki wake kama waonekanavyo pichani usiku huu.
Mkali mwingine anaekuha juu katika mambo ya kuchana a.k.a kughani Stamina akiamsha kitim kitim kwa wakazi wa mji wa Mbeya usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta.

Friday, September 21, 2012

WENJE AJIBU MAPIGO MWANZA, AZUNGUMZIA PIA KUZOMEWA WAZIRI MKUU, ATOA SHAVU KWA LOWASA


"Hata Dokta Slaa akileta noma leo, hata Mbowe, hata Zito, hata Wenje, CHADEMA Itasonga !!! Kwani  CHADEMA ndiyo tumaini la Watanzania iliyobeba Wakristu na Waislamu ambao wana matumaini ya kufika wanapotaka kufika"... 
"Hiki chama ni kikubwa kuliko mimi Wenje ndiyo maana naibu Meya amewaambia kuwa mimi nani alikuwa ananijuwa? Chadema imeanza kabla yangu mimi nikafuatia...." Ni  kauli az Mbunge wa Nyamagana Mhe. Ezekiel Wenje aliyoitoa leo wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la wazi kata ya IGOMA wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza.


Akizungumzia kuhusu fedha za jimbo (CDCF) Mh. Wenje amesema kuwa kila kata kila diwani awe wa CCM awe wa Chama gani alipewa shilingi milioni tatu  kwa ajili ya maendeleo ya kata yake hivyo siku yaja ambapo kila diwani kwa mipango aliyowasilisha atakwenda kukaguliwa na migao hiyo ya milioni tatu, tatu ni suala la kitaifa.




WENJE Amsifu Lowasa kuwa na ndoto ya kukuza elimu nchini amponda Pinda na mpango wake kuhakikisha kila mtanzania anamiliki mizinga ya nyuki. (SIKILIZA)
Pigo la chini alilokuwa 'katupia pale kati' mhe. mbunge Wenje .....   


WENJE Ajibu shutuma za kununulia watu viroba wamzomee mhe Pinda mkutano wa Sahara Mwanza. (SIKILIZA)
WENJE  Ajibu shutuma za Pinda kuwa CHADEMA imeshindwa kuongoza Halmashauri ya jiji la Mwanza ndiyo maana wanafukuzana. (SIKILIZA)
Wananchi wakimsikiliza Mhe. Ezekiel Wenje katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo ijumaa eneo la Igoma jijini Mwanza.


Wadau kila mtu na umakini wake kusanyikoni...


Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje na watu wake...


Kilichonishangaza tofauti na zama zilizopita nembo, mavazi au alama za vyama vingine zilikuwa zikipigwa marufuku au kuchanwachanwa au hata kuteketezwa maeneo ya makusanyiko kama haya lakini safari hii utulivu amani vimeenea watu wakisikiliza sera. PIG UP!!!!

VUTA PUMZI - HADOLOLO...!!

Ni daladala inayofanya safari zake Igoma to Airport jijini Mwanza na hii ndiyo taswira ya eneo la suka wa mchuma huo yaani full mapambo. 

Midoli, kapu la maua na sanamu ya sato chunguza utabaini...

Ni wiki inayosubiriwa kwa hamu na wakazi wengi wa jiji la Mwanza, kiingilio ni bureeeee..... 

Vipaji mtaani.

Kweli machinga complex yahitajika kwa jiji hili... lakini hivi ni kweli litakuwa suluhisho kwa wadau kama hawa.
Haya tumalizie jikoni hoteli za uswazi... kwa mdafada anaye saga karanga.