ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 15, 2012

LIGI KUU SOKA TANZANIA BARA YAANZA RASMI LEO.

Kwenye uwanja wa wa CCM kirumba jijini mwanza Toto Africans inaikaribisha JKT Oljoro kutoka Arusha

Toto Africans ndani ya dimba la CCM Kirumba muda huu.

JKT Oljoro kutoka Arusha ndani ya dimba la CCM Kirumba muda huu.

Ligi kuu soka Tanzania Bara inaanza leo jumamosi ambapo timu zote 14 zinazoshiriki michuano hiyo zitajitupa kwenye viwanja saba tofauti nchini. 

Kwenye uwanja wa wa CCM kirumba jijini mwanza Toto Africans inaikaribisha JKT Oljoro kutoka Arusha huku Kagera Sugar wakiwa wenyeji wa Azam Fc ya Dar es salaam kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Mabingwa wa kombe la Kagame Young Africans wataianza ligi hii ugenini dhidi ya Tanzania prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Mabingwa watetezi wa ligi hii Simba Sc wao wako uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam wakiumana na African Lyon.

Timu mbili za Morogoro Polisi Morogoro na Mtibwa Sugar zitapambana kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini humo, wakati MaMagombo JKT ikichuana na Costal Union mjini Tanga.

Pia Timu mbili za mkoani Pwani JKT Ruvu na Ruvu Shooting Stars nazo zinaanza ligi hii kwa kucheza kwenye uwanja wa Chamanzi.

SERENGETI FIESTA 2012 DODOMA FUNIKA BOVU


Baadhi ya mashabiki wakishangweka vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri,Dodoma.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya,mahiri katika miondoko ya miduara,IT akimrusha kimduara duara shabiki wake jukwaani usiku huu,huku shangwe za hapa na pale zikiwa zimetawala kutoka kwa watazamaji.

Wasanii mahiri wa filamu hapa nchini nao walikuwepo kuliunga mkono tamasha la Fiesta usiku huu ndani ya Dodoma,kutoka kulia ni Jacob Steven a.k.a JB,Wema Sepetu pamoja Aunt Ezekiel.

Ray Kigosi akilicheza sebene jukwaani.

Ray akimtambulisha Wema Sepetu kwa mashabiki.

Ray akiwaaga mashabiki wake mara baada ya kuwavunja mbavu mara baada ya kumaliza kulicheza sebene lake jukwaani.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Mh.Dr Rehema Nchimbi akisoma jina la mshindi wa gari aina ya Vitz inayotolewa na kampuni ya Push Mobile,ikiwa ni sehemu ya mchakato wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012,pichani kati ni Meneja masoko wa kampuni ya Push Mobile,Rodney Lugambo,Muwakili shi wa michezo ya bahati nasibu ya Taifa,Bwa.Humudi pamoja na Mkuu wa wilaya ya Dodoma mjini,Mh Lephy Gembe. 

Mkuu wa wilaya ya Dodoma mjini,Mh Lephy Gembe akiwasalimia wakazi wa Dodoma waliojitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,kwenye uwanjawa jamuhuri.

Pichani juu na chini Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Linah kutoka THT akitumbuiza jukwaani usiku huu wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea usiku 
Pichani juu na chini ni msanii anaetamba katika miondoko ya R&B hapa bongo,aitwaye Ben Paul akiwarusha wakazi wa mji wa Dodoma waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Serengeti Fiesta linaleondelea usiku huu kwenye uwanja wa Jamuhuri.
Msanii wa bongofleva aitwaye Shetta akiwaimbisha washabiki wake usiku huu.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Rich Mavoco akiwaimbisha washabiki wake kibao waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linalofanyika usiku huu ndani ya uwanja wa Jamuhuri.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Dayna akijitokeza kwa mbwembwe jukwaani usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linaloendelea hivi sasa kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma,ambapo wakazi wake wamejitokeza kwa wingi kuwashuhudia wasanii mbalimbali wanaotumbuiza kwenye jukwaa hilo.

Wakazi wa mji wa Dodoma wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,ndani ya uwanja wa jamhuri mjini Dodoma.
mmoja wa wasanii chipukizi katika anga ya muziki wa kizazi kipya,ambaye pia aliibuliwa na shindano la Serengeti Supa Nyota kutoka jijini Mwanza,aitwaye Young Killer akikamua jukwaani mbele ya umati wa wakazi wa mji wa Dodoma usiku huu.
Wasanii kutoka THT wakitumbuiza jukwaani usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
Anaitwa Recho kwa jina la kisanii kutoka nyumba ya Vipati THT,akiimba jukwaani kwa madaha kabisa,huku umati wa watu (haupo pichani) ukishangilia kwa nguvu.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya akiwa amebebwa juu  mara baada ya kujitokeza jukwaani na wasanii waliopa  mtafu kutoka THT.
Kwa hakika wakazi wa mji wa Dodoma wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye uwanja wa Jamuhuri,ambako ndiko tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea hivi,shangwe tuu.

Friday, September 14, 2012

KUWA MLEMAVU WA VIUNGO HAIMAANISHI WEWE NI MLEMAVU WA AKILI.

Mtoto mlemavu wa viungo akimudu maisha kwa kutumia viungo vyake na kumudu maisha ya kujitegemea mbali na kuwa tegemezi kwa kushiriki kupika chakula.

Mtoto huyo akiwa na familia yake tena kwa furaha teeeele.

Hivi ndivyo mwanawane anavyokula bila utegemezi naye maisha kayazoea anaishi kama wewe uliye na viungo vyote. 

Na maji ya kunywa akishushia.

Maisha yanategemea sanaa na jinsi unavyoyapokea  na changamoto zake zilizoko mbele yako vile unavyozikabili kwa mtazamo chanya katika mazingira hasi. Kinachohitajika ni kuona kinachowezekana katika kisichowezekana ili kukabili maisha ya amani na mafanikio, pichani akiwa na furaha mara baada ya kukabidhiwa baiskeli ya magurudumu matatu.

Pozi la umakini nyumbani.

Mtoto aliyezaliwa na ulemavu wa viungo akiwa na ndugu jamaa na marafiki wakifurahia pamoja maisha.  
MAISHA YANATEGEMEA SANAA NA JINSI UNAVYOPOKEA CHANGAMOTO ILIYOKO MBELE YAKO KWA MTAZAMO CHANYA KATIKA MAZINGIRA HASI. KINACHOHITAJIKA NI KUONA KINACHOWEZEKANA KATIKA KISICHOWEZEKANA ILI KUKABILI MAISHA NA KUISHI MAISHA YA AMANI NA MAFANIKIO.

IBF YAWAPONGEZA WADAU WANAOSAIDIA KUPROMOTI NGUMI TANZANIA/AFRICA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tarehe 14, Septemba, 2012 

Shirikisho la Ngumi la Kimataifa IBF lenye makao yake makuu katika jiji la New Jersey, nchini Marekani kupitia ofisi zake za Afrika, Mashariki ya Kati, Ghuba za Uarabu na Uajemi linachukua fursa hii kuwapongeza wadu wote wa ngumi wanaosaidia kuuendeleza mchezo huu hapa Afrika. 

IBF inachukua fursa hii kuwapongeza wafuatao kwa juhudi zao binafsi katika kuchangia kuuendeleza mchezo wa ngumi za kulipwa: 

Afrika ya Kusini: (Branco Milenkovic). Zambia: (Captain John Chewe, Anthony Mwamba). Zimbabwe: (Richard Hondo), Ghana: (Henry Mann-Spain, Michael Tetteh), Nigeria: (Ken Biddle), Ivory Coast: (John Ajaba). Misri: (Richard Nwoba), Oman: (Amin Saad Bait-Mabrook), Tanzania: Gabriel Nderumaki, Lucas Rutainurwa, Titus Kadjanji, Fidel Haynes, Yassin Abdallah (Ustaadh), Nemes Kavishe, Boniface Wambura, Godfrey Madaraka Nyerere, Shomari Kimbau pamoja na Msajili wa Wizara ya Mambo ya Ndani, BMT, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, BIDCO, Pepsi, Vyombo vyote vya habari vya magazeti, Radio, Television, Blogs na Websites pamoja na wengine wote ambao wamesaidia kwa njia moja au nyingine. 

IBF inaamini kuwa ushirikiano wetu wote utasaidia kuuendeleza mchezo wa ngumi za kulipwa na kuwezakujenga ajira nyingi kwa vijana wan chi zetu.  

Imetolewa na: 
Onesmo Ngowi

Rais,

IBF Afrika, Mashariki ya Kati, Ghuba za Uarabu na Uajemi

MWANDISHI AFUKUZWA UANACHAMA BAADA YA KUWASALITI WENZAKE


Na Mwandishi Wetu

MUSOMA

Maxmilian Ngesi
CHAMA cha Waandishi wa Habari mkoani Mara MRPC, kimemfukuza uanachama wa chama hicho, mwandishi wa habari wa radio Free Afrika mkoani Mara Bw Maxmilian Ngesi baada ya kukiuka makubalino ya chama hicho yaliyofikiwa juzi ya kutoandika kabisa habari za jeshi la polisi mkoani humo.
 
Akizungumzia kufukuzwa kwa Mwandishi huyo mwenyekiti wa chama hicho  Bw Emmanuel Bwimbo,alisema kuwa Ngesi amekiuka makubaliano ya waandishi wenzake na chama kwa ujumla baada ya kusikika akitangaza habari za jeshi la polisi kwa kumkariri kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara.
 
 “ Sisi kwa kauli moja tumekubaliana kutofanya kazi na Jeshi la Polisi Mkoani Mara baada ya Matukio kadhaa likiwemo ya kuuawa kwa mwandishi wa habari mkoani Iringa na kutunyima kibali cha Maandamano yetu ya Amani kupinga Mauaji hayo” alisema Bw Bwimbo
 
Bw Bwimbo alisema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi gani mwandishi huyo alivyokiuka makubaliano ya pamoja na kuwasaliti wenzake ambao wamekubaliana kwa pamoja kuwa hawataandika habari za jeshi hilo kutokana na kuzuiwa waandishi kutoandamana katika maandamano ambayo yaliitishwa nchini kote kulaani kitendo cha mauaji ya mwandishi wa kituo cha chanel Ten mkoani Iringa Daud Mwangosi.

Alisema Ngesi  kama mwanachama alitakiwa kutii maamuzi ya chama na tamko la chama chake kwa vile tamko hilo limewataka wananchama wote na siyo kwa mkoa wa Mara tu lakini pia baadhi ya mikoa imetoa matamko na misimamo hiyo lakini cha kushangaza yeye amekaidi na kwenda kinyume.
 
Aidha Mwenyekiti huyo alisema  kamwe chama hicho hakiwezi kuvumilia mwandishi atakaye kiuka agizo hilo na hatua ambayo imechukuliwa kwa Ngesi ni  mfano kwa waandishi wengine hadi hapo tamko hilo litakapo tenguliwa.
 
Jumatatu wiki hii waandishi wa habari walifanya maandamano nchi nzima wakilaani mauaji ya mwandishi mwenzao Daudi Mwangosi  ambapo kwa mkoa wa Mara maandamano hayo yaliuzuiwa na polisi hali iliyofanya chama cha waandishi wa habari kukataa kuandika habari za jeshi hilo mkoani Mara.
 

MUINGEREZA AKAMATWA UGANDA KWA USHOGA

David Cecil katika mahakama ya Makindye

Msanii moja toka Uingereza amekamatwa nchini Uganda kwa madia ya kuandaa na kuonyesha mchezo wa kuigiza kuhusu ushuga.
Mtayarishi David Cecil wa Uingereza alifikishwa katika mahakama moja mjini Kampala na kushitakiwa kwa madia ya kukaidi na kupuuza amri ya serikali. Polisi wanasema kuwa Muingereza huyo alionyesha mchezo huo wa kuigiza licha ya kwamba Uganda ilipiga marufuku kwa muda onyesho hilo.
Mahakama hiyo iliambiwa kuwa Bwana Cecil alionyesha mchezo huo kwa jina "The river and the mountain" katika ukumbi wa Tilapia Cultural Center taraehe 17 Agosti na pia katika ukumbi mwengine wa Mish Mash Cultural Center tarehe 26 Agosti mjini Kampala.
Mahakama hiyo ya Kampala ilikataa kuamuachilia Muingereza huyo kwa dhamana na badala yake kuagiza awekwe katika gereza la Luzira hadi siku ya jumatatu ,Septemba 17 ambapo kesi yake inatarajiwa kuendelea.
CHANZO: BBC Swahili.

Thursday, September 13, 2012

MADIWANI WALIOVULIWA UANACHAMA CHADEMA WATOA TAMKO

DIWANI wa Kata ya Kitangili Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza Henry Matata na Diwani  wa Kata ya Igoma Halmashauri ya Jiji la Mwanza (Nyamagana) Adam Chagulani wote kutoka Chama cha CHADEMA wametoa tamko lao kwa vyombo vya habari leo kupinga maamuzi ya Kamati kuu ya Chama hicho ya kuwavua uanachama hivi karibuni kwa madai ya kukisaliti chama na kula njama kukushinikiza kumung’oa aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza Josephat Manyerere (Nyakato).


Diwani wa kata ya Kitangili Henry Matata.

Diwani Matata (Kitangili) alisema kwamba kikao cha kamati kuu kilichoketi mwishoni mwa juma lililopita na kutoa uamuzi huo Jijini Dar es salaam kiligubikwa na ushabiki na pia ukiukwaji wa Katiba ya Chama hicho na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo wameamua kwenda mahakamani kufungua kesi ya kuzuia uamuzi huo wa Kamati kuu ya CHADEMA wa kuwavua uanachama ili kukosa madaraka (Udiwani)  ikiwa wao walichaguliwa na wananchi zaidi ya elfu nne.

Akifafanua Matata amedai kuwa moja ya sababu kubwa zilizowafanya kukimbilia mahakamani yeye na diwani mwenzake Chagulani ni kutaka haki itendeke kwa vile madai na tuhuma zilizotolewa dhidi yake ni za uongo ambazo hazina ukweli bali kwa shinikizo la wabunge wa chama hicho wa majimbo ya Ilemela, Nyamagana na Ukerewe kutokana na kuwepo kutokuelewana baina yao na madiwani hao wanaodaiwa kuwahofia kisiasa.

Diwani wa Igoma Adam Chagulani.
 Kwa upande wake Chagulani (Igoma) alieleza kuwa hatua hiyo imetokana na Kamati kuu ya chama hicho Taifa kukubaliana na mapendekezo yaliyotolewa na baadhi ya viongozi ambao wamekuwa akishirikiana na wabunge wa Chama hicho wa Majimbo ya Ilemela Haghiness Kiwia na Ezekia Wenje Nyamagana kutokana na wao kutofautiana nao kwenye vikao vya baraza la madiwani na vya chama wakati wa kuchangia hoja kwa lengo la kuwatumikia wananchi waliowachagua.

Chagulani alisema kwamba umefika wakati wa viongozi wa chama hicho kuacha kutumia ubabe wa kuamua kuwafukuza wawakirishi wa wananchi waliochaguliwa kwa kisingizio cha kukisaliti chama hicho bali watambue kuwa wao ni kiungo cha kuwatumikia wananchi na kuwawakilisha kwenye mabaraza ili kuzitafutia kero zao ufumbuzi na CHADEMA lazima itumie vikao vya chini na kuifuata vyema Katiba yake na hatua za wenye makosa kujadiliwa kuanzia ngazi ya kata, wilaya, mkoa na Taifa badala ya kuanzia juu kisha kutoa uamuzi hiyo si demokrasia hata kidogo bali ni udikiteta wa demokrasia ndani ya vyama vya siasa.

BARUA ALIYOANDILIWA MH. DIWANI CHAGULANI KUVULIWA UANACHAMA CHADEMA


Diwani wa Kata ya Kitangili Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza Henry Matata (kushoto) na Diwani  wa Kata ya Igoma Halmashauri ya Jiji la Mwanza (Nyamagana) Adam Chagulani wote kutoka Chama cha CHADEMA wakizungumza na vyombo vya habari kutoa tamko lao kupinga maamuzi ya Kamati kuu ya Chama hicho ya kuwavua uanachama.

WASHINDI WA REDD'S MISS KINONDONI WAZAWADIWA MAPAMBO YA MWAKA MZIMA NA PERFECT LADY CLASSIC SALOON, DAR

Mkuu wa Itifaki wa Miss Tanzania Albert Makoye akifungua mashindano ya Redd's Miss Kinondoni Talent, pembeni yake ni Ssebo ambaye ni mmoja kati ya mwanabodi wa Redd's Miss Kinondoni 2012 na alikuwa ni mshereheshaji katika shindano hilo lililofanyika katika hoteli ya JB Belmonte, iliyopo jengo la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Mashindano hayo yalidhaminiwa na Perfect Lady Classic Saloon iliyopo Kinondoni jijini Dar na wametoa zawadi kwa washindi watatu waliopatikana kwa kupewa huduma kwa kipindi cha mwaka mzima ndani ya Saloon yao. Shindano rasmi la kumsaka Redd's Miss Kinondoni linatarajiwa kufanyika Ijumaa tarehe Septemba 14, 2012 katika Ukumbi wa Cassa Complex uliopo Mikocheni, Dar.

Mshiriki namba 6, Irene akionyesha manjonjo yake katika kucheza.
Mshiriki namba 3, Nahma Saidi yeye aliambua kuonyesha mambo ya Pwani.
Mshiriki namba 2, Ester Musa alionyesha kipaji cha kuimba.
 Mshiriki namba 1, akionyesha umahili wake wa kukata uno.

Mshiriki namba 4, Diana Hussein akionyesha jinsi ya kubuni vazi. 
Brigitter Alfred mshiriki namba 9 alionyesha umahili wake katika nyimbo za kihindi. 
Majaji wa shindano la Redd's Miss Kinondoni Talent Man Maji (kulia) na mwanadada wakifuatilia kwa makini.
Mshiriki namba 10, Kudra Lupatu akionyesha kipaji chake cha kubuni mavazi kwa staili ya kumvalisha mshiriki mwenzake.
Kudra Lupati katika pozi mara baada ya kumaliza kutambulisha vazi lake. 
Mshiriki wa Redd's Miss Kinondoni akichora mlima Kilimanjaro.
Ssebo ambaye ni mmoja kati ya mwanabodi wa Redd's Miss Kinondoni 2012 na alikuwa ni mshereheshaji katika shindano hilo la Talent akimkaribisha Mratibu wa Redd's Miss Kinondoni 2012, Vivien Sirikwa (kulia) kuongea machache.

Mkurugenzi wa Perfect Lady Classic Saloon, Ester Kiama ambao ndiyo waliokuwa wamedhamini Redd's Miss Kinondoni Talent akitangaza zawadi alizowapatia warembo walioshinda.
Wakiwa katika nyuso za furaha ni warembo walioshinda katika Kinyang'anyiro cha Redd's Miss Kinondoni Talent kutoka kulia ni Judith Sangu, Brigitter Alfred na Diana Hussein. Warembo hao wamepatiwa zawadi ya kupewa huduma Perfect Lady Saloon kwa kila mmoja kipindi cha Mwaka mzima.

Warembo wakiserebuka mara baada ya shindano hilo kuishi.

...Hapa ni mwendo wa Kwaito...
Muziki umenoga kwa mwalimu na mwanafunzi.
Ssebo ambaye ni mmoja kati ya mwanabodi wa Redd's Miss Kinondoni 2012 na alikuwa ni mshereheshaji katika shindano hilo la Talent akiongea machache na Mkurugenzi wa Perfect Lady Saloon, Ester Kiama.
Show Love nayo ilikuwepo kwa muaandaji na mdhamini.