ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 4, 2012

MWANZA WATAHADHARISHWA JUU YA EBOLA

SERIKALI mkoani Mwanza, imewataka wananchi kuchukua tahadhali kuhusiana na tishio la ugonjwa wa Ebola ambao umeripotiwa kuuwa watu kadhaa nchi jirani ya Uganda. 


 Tahadhali hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza,Mhandisi Evarist Ndikilo, alipozungumza waandishi wa habari kuhusuiana na ugonjwa huo. 

 Alisema serikali ya mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imepanga mikakati ya kukabiliana na tishio la ugonjwa huo hatari unaouwa kwa haraka.

 “Ukiangalia jiji letu la Mwanza lina mwingiliano mkubwa kutokana na kuwa kitovu cha biashara kwa nchi za Maziwa Makuu, hivyo wananchi wanapaswa kuchukua tahadhali kwa kujikinga na kutoa taarifa pindi wanapomwona mtu mwenye dalili za ugonjwa huo,”alisema Ndikilo Alisema shirika la Afya Duniani (WHO) tayari limethibitisha kuwepo kwa ugonjwa wa Ebola nchini Uganda, katika Wilaya ya Kibule, Magharibi mwa nchi hiyo ambapo watu 26 wameriptiwa kuambukizwa na kati yao 14 wamefariki dunia kwa kuambukizwa ugonjwa huo tangu Julai 28, mwaka huu.

 Mhandisi Ndikilo, alieleza kuwa ugonjwa huo huambukiza kwa kugusana na mtu mwenye kuathiriwa na virusi vya Ebola ambavyo hutokana na sokwe pamoja na jamii ya wanyama aina hiyo, ambapo kwa mara ya kwanza ulibainika kuwapo 1976.

 Dalili za ugonjwa huo ni homa kali ya ghafla,vidonda vya koo, upele katika ngozi na kutokwa damu sehemu mbalimbali za mwili na katika kukabiliana na maambukizi Ebola, wataalamu wa wizara ya Afya ambao tayari wapo jijini hapa, watafanya ukaguzi kwa wageni waingiao nchni kupitia njia ya anga, majini na nchi kavu bila usumbufu.

 “Hatua za kuchukua ni kuongeza kasi ya ufuatiliaji, kufanya ukaguzi bila usumbufu kwa wageni wanaosafiri kwa ndege, meli na mabasi kuingia nchini, kutoa elimu kwa wananchi na watumishi wa afya na upatikanaji wa vifaa vya kinga;”alisema Alisema ili kuwalinda wananchi, vipeperushi na vijarida vinavyohusu ugonjwa huo wa Ebola vitasambazwa ili wananchi wapate ufahamu wa dalili zake lakini pia wawe tayari kutoa taarifa pndi wanapomhisi mtu mwenye dalili za gonjwa huo.

 “Pamoja na juhudi za serikali, kupitia vyombo vya habari eneo la mikoa ya Kanda ya Ziwa tuchukue tahadhali kuhakikisha wananchi wanafahamu tatizo hili kwa kusoma vipeperushi na kupashana habari,”alisema Mkuu huyo wa mkoa Tayari watu 14 wamefariki dunia katka wilaya ya Kibule Magharibi mwa nchi ya Uganda tangu kuzuka kwa ugonjwa huo Julai 28 mwaka huu.

Mwaka jana mtu mmoja aliliripotiwa kufa nchini humo kutokana na kuambukizwa virusi vya ugonjwa wa Ebola. Mbali na Uganda, miaka kadhaa iliyopita Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) iliwahi kukumbwa na ugonjwa huo na watu kadhaa kuripotiwa kufa.

WA HAPA HAPA

Nanunua mzigo nami chomboni ni wafanyabiashara eneo la stand ya tax na daladala mbele ya lango kuu soko kuu Mwanza.

Chambo kwaajili ya kuvulia samaki anasakwa ndani ya mfereji mkuu wa maji eneo la Kirumba.

Mpango wa jiji safisha mitaro ya eneola barabara ya soko la Kirumba inaendelea.

Zoezi hili linafanyika leo jumamosi. Swali ni jeh! vifusi hivi vya mchanga na taka vitaondoka kwa muda sahihi? ngoja tuone endelea kufuatilia....

Ni biahsra katika eneo la Kamanga Ferry jijini Mwanza. Ramadhani hii imeangukia msimu wa mavuno, Alhamdulilah neema ya Mwenyezi Mungu imetumwagia.

Unaiju hii kitu ya Nyahindi?

Nasikia mchanganyo wake ukiutumia waweza tembea umbali mrefu bila kujistukia yaani full ganzi. Kama ni Dar- Mwenge hadi Posta, kama ni Zoo- Nyakato hadi Airport, na kama ni Ar- Sakina hadi Njiro... Babake...

Tofauti na miaka ya nyuma ambapo ukionekana kuokota makopo utawekwa kwenye kundi la watu wenye akili fulani but now days ni dili tena linalowahusisha wenye akili zao watengenezao fedha. 

Jamaa huyu muuza fagio yu mkarimu saana kwa wateja wake na ana lugha ya mvuto kwa biashara aliniambia jina lake any wayz wanaojua watanikumbusha....

CCM DMV WAFUTURISHA


CCM DMV Wafuturisha

Makada wa CCM wakiwa na kadi za  uwanachama kwa wanachama wapya  katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akipata picha na tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha CCM, katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha Mapenduzi CCM

Baadhi ya waTanzania mbali mbali waliohudhuria kwenye futari hiyo ilioandaliwa na tawi la CCM DMV

Baadhi ya waTanzania waliovalia rangi za chama cha CCM wakiwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

  Makada wa CCM Tawi la DMV shoto Mbunifu wa Ma Winny Casey Khanga Wrap Designer, pamoja na Peter Ligate (Picha ya kulia) wakiwa katika mpango mzima wa futari ya pamoja ilioandaliwa na wanatawi la CCM DMV

Watanzania  waliojumuika  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.


Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akiwakaribisha rasmi  wageni walikwa  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Baadhi ya wanachama wa  CCM Tawi la DMV wakipata picha ya pamoja baada ya futari walioiyanda

Wanachama wa  CCM Tawi la DMV na baadhi ya wageni wawili kutoka Londan Uingereza
Wageni wawili majirani wapendanao kutoka jijini London pia walihudhuria katika futari hiyo ilioandaliwa na  ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani

Katibu wa CCM DMV Jacob Kinyemi, kushoto akipata picha ya pamoja na  Halima baada ya kumkabidhi rasmi kadi ya uwanachama wa CCM, Jana Ijumaa  na kuwa mwanachama rasmi wa CCM. (Picha na http://swahilivilla.blogspot.com/)

Friday, August 3, 2012

SIKILIZA JINSI NGASA ALIVYOMALIZANA NA AZAM NA KUSAJILI RASMI SIMBA

Mara baada ya taarifa kutoka kwenye mitandao mbalimbali zikimzungumzia MRISHO Khalfan Ngassa kuuzwa Simba kwa dau la Sh. Milioni 25 nao Azam kukiri kuwa tayari wamekamilisha dili huku winga huyo akikanusha taarifa hizo hivyo kuwaweka njia panda wapenda michezo wengi nchini. 


Sports Extra ya Clouds Fm kupitia watangazaji wake Ibrahim Masoud 'Maestro' na Jof Leah wamelifuatilia sakata hilo na hatimaye kwa kina wamekuja na taarifa kamili juu ya winga huyo. 
 Kusikiliza bofya hapa chini:-

 

WENGI WATAJINYEA KWA MPANGO WA MWAKYEMBE

JANA Dk Mwakyebe alipiga marufuku suala la kuchimba dawa safarini na hasa wale wasafirio na mabasi yaendayo mikoani ambapo mabasi husimama pori na kuwaruhusu watu kwenda kujisaidi maarufu kwajina la kuchimba dawa.

Utamaduni huo umeota mizizi katika barabara zote kuu iwe Dar Lindi Mtwara, Dar Iringa Mbeya Tunduma, Dar Iringa Songea, Dar Mwanza na kwingineko nchini.
Mh. Mwakyembe

Akiongea wakati akijibu hoja za wabunge wakati wa kuhitimisha mjadala kwa wizara yake Dk Mwakyembe amesema basi lolote litakalokamatwa limesimama porini kwa ajili ya kuchimba dawa, kosa la kwanza atapewa onyo, la pili atapigwa faini kubwa na la tatu atafungiwa akatafute/ akafanye biashara nyingine.

Kauli hi imekuja wakati tukijua kwamba njia zote kuu za barabara ziendazo mikoni hakuna vituo maalum vya kupumzika abiria na kuchimba dawa na hata kama vipo hakuna vyoo na au vyoo havitoshi au havina usafi wa kutosha ukiacha vile vilivyopo kwenye mahoteli ya njiani.

Wadau hii imekaje... kipi kingeanza kupiga marufuku kusimamisha mabasi njiani au kungeanza mradi wa kujenga vyoo kwenye maeneo yale maarufu kwa kuchimba dawa?
Mwalimu Msungu 


Majibu :- 
@Mwezi uliopita nimesafiri kwa basi kutoka Dar hadi Tanga, Tanga hadi Arusha, Arusha hadi Dar, Dar hadi Songea, na Songea hadi Dar. Haiwezekani kufanya safari yoyote ya aina hiyo bila kuchimba dawa, na sisi wengine tunahitaji hata mara mbili au zaidi.

Napinga kabisa, na kwa nguvu zote uamuzi huu wa Mheshimiwa Mwakyembe. Nitakubaliana naye tu iwapo sehemu za kuhudumia wasafiri zitakuwa tayari zimejengwa, kama ilivyo sehemu kama Marekani. Mheshimiwa Mwakyembe ashinikizwe kutengua amri yake hiyo leo hii.
Joseph L. Mbele


@Nini vipaumbele vya wizara yake Mwakyembe? Suala la uchimbaji dawa kwangu mimi binafsi ni la baadae sana na angeliongelea mara tu baada ya kuweka miundo mbinu safi vikiwemo vyoo kwenye vituo kadhaa. Atachanganya mambo!! Suala la kuchimba dawa ni minor sana. 
Sent from my BlackBerry

@Mweshimiwa inaonekana dhahiri siku nyingi zaidi ya miaka mingi hajapanda usafiri wa basi zaidi ya hivi majuzi kuakti  (kutengeneza picha) picha la mweshimiwa kupanda treni naye akiwa stering wa lile muvi.

Muheshimiwa kazoea kupanda gari binafsi lenye hewa safi na kiyoyozi akijichagulia vyakula vya kula safarini tena hii ni kwa mara moja moja kwa safari ndefu, mara zote yeye ni juu kwa juu na pipa aka ndege,,, sasa sie akina kajamba nani kwenye basi lenye watu zaidi ya 60 kila mtu na tumbo lake na maji yake huyu yamechemshwa yule hayajachemshwa kisha vyakula vya njiani vya bana matumizi, karanga na makande makavu (ngararuu) wafanya mchezo.

 Alipaswa kufanya utafiti kwanza na kujua umbali wa kituo na kituo kwani maeneo mengi ni pori na hata ukikuta vijiji vyoo ni vya kaya havikidhi mahitaji ya nyomi ya wasafiri.

Serikali kupitia wizara yake ingetengeneza kwanza utaratibu wa kujenga vyoo kwa utaratibu ule ule wa utafiti kupitia madereva kugundua ni maeneo gani korofi kwa maana kwamba maeneo ambayo abiria wengi husumbua kuchimba dawa kisha katazo likafuata.

 Mie mwenyewe huwa nainjoi kuchimba dawa yaaani hata nisipochimba dawa basi nita piga picha basi tulilopanda, miti ya porini nini na nini na nini ...daaaah hakika kwa hili nitamisi sana hako kazoezi. Kwa mpango huu tutajinyea sana safarini.

Mwakyembe kachemka.
Jipange.

g to tha s.


@Interesting discussion. Wasioona adha ya kuchimba dawa ni sisi "wahuni" ambao tomezoea popote tu unasimama unatoa maungo yako na kukojoa au kunanii peupe. Mtu yeyote mstaarabu hawezi kushabikia kukojoa au kupata haja kubwa vichakani!!!! Mwakyembe kwa jinsi nilivyomuelwa hajakataza mabasi kusimama njiani abiria wapate kukojoa, alichosema yeye ni kuwa hayaruhusiwi kusimama porini ambapo kina mama, wazee na watoto wote wanalazimika kupata haja zao mithili ya wanyama. Mnaotetea kuchimba dawa porini naombe mtangaze maslahi yenu kwenye hili isije ikawa ni wapiga nanii!!!! 

Du Veda.
@Ni akili kidogo tu inahitajika kwa wenye mabasi. Leo hii Ndenjela Bus inasimama stendi ya  Makambako na kutoa dakika 10 abiria kujisaidia na kunywa chai wakati wengine wakifukuzana kuwahi pale porini!!!
Felix.
 
@Hapa dokta naye kaenda mbali, sasa kuchimba dawa na wizara yake wapi na wapi? Nilidhani hoja hii angeitoa daktali mwenzake Telezia wa Makamu wa Rais!! Labda angesema mabasi yawe na vyoo ndani kwani ni jambo lisilowezekana mtu kupanda basi Dar kwenda Mtwara ujisaidie Nangurukuru ndiyo kwenye vyoo urefu wa kilomita zaidi ya 200!!!
Wa Simbeye.

TSC SPORTS ACADEMY YATISHA NCHINI UJERUMANI

Nahodha wa TSC Madukuru akimkabidhi zawadi kutoka tanzania, meya wa jiji la Brackenheim nchini Ujerumani.

Badge ya TSC Academy pamoja na Zawadi kinyago kutoka Nyumbani Tanzania aliyokabidhiwa meya

TSC Academy

Salaaam kwa mheshimiwa Meya...

Wachezaji wakipewa zawadi za nguo na meya wa Brackenheim

Miraji Madenge akisaini kwenye kitabu cha wageni

Mkurugenzi wa TSC Mutani Yangwe, Mratibu wa TSC Ujerumani Jurgen Seitz wakifurahia jambo na Meya

Hapa ni kazi tu uwanjani...

TSC yatoa Kipa bora

Licha ya kipindi fulani kuwa katika mapunziko suala la mazoezi kwa timu ya vijana wa Mwanza TSC liko pale pale ndani ya ratiba.

Picha ya msafara mzima wa Timu ya TSC Academy Ulipomtembelea meya wa Brackenheim
Timu ya TSC Sports Academy U20, Yawatoa kamasi Vijana wenzao wa  Ujerumani
Timu ya TSC Sports Academy (U20) ya Jijini Mwanza, Iliyoko kwenye ziara ya michezo hasa mpira wa miguu, Imeendelea kutisha kwa kutoa dozi kwa baadhi ya timu inayokutana nazo kwenye manshindano mbalimbali.

Katika Mashindano ya maarufu ya Insel Cup 2012 yanayofanyika kila mwaka katika mji wa  Mannheim yakishirikisha timu mbalimbali kutoka Ulaya na hapa Ujerumani. Mashindano haya ya timu za miaka 20 yana umri wa miaka 55 toka yaanzishe katika mjii huu. Mashindano ya Mwaka huu yalishirikisha timu za
Maccabi Haifa-U20 ambao ni mabingwa wa vijana inchini Israel, Hijduk Split – U20 Mabingwa wa vijana Croatia, TSC Hoffenheim – U20 ambao wanashiriki na kushka nafasi bora za juu katika msimamo wa ligi ya vijana hapa Ujerumani, 1860 Munich timu ngumu kabisa ya vijana na moja ya timu tano bora hapa Ujerumani, timu nyingine ni wenyeji Waldhof Mannheim-U20 na Karsruher SC zote za hapa Ujerumani.
TSC Academy  Ilipangwa kundi A na timu za Maccabi Haifa, 1860 Munich, TSG Hoffenheim na kundi B lilikuwa na timu za Hijduk Split ya Croatia, Karlsruher na Waldhof Mannheim

Matokeo ya TSC yalikuwa yakuwa kama ifuatavyo:-
Group A
TSC Academy 2 –2 1860 Munich, TSC Academy 1- 1 TSG Hoffenheim, TSC Academy 0- 1 Maccabi Haifa Mshindi group hili alikuwa 1860 Munich  Point 4, akifuatiwa na Maccabi Haifa point 3 na TSC Academy point 2 magoli 3, TSC Hoffenheim Point 2 magoli 2

Na katika msimambo wa Jumly TSC ilishika nafasi ya 5 baada ya kucheza mechi nyingine ambayo tulicheza na Waldof Mannheim na kutoka 1-1.

Kwa ujumla vijana walionyesha mchezo mzuri na kuvutiwa na mawakala na timu zote zilizokuwa katika mashindano, kwa maana ya kwamba TSC Academy ndio timu peek ambayo ilikuwa haishiriki ligi yoyote ya vijana kwetu Tanzania, lakini timu nyingine zinashiriki ligi kuu za vijana za nchi zao, wachezaji wa TSC waliongara sana kwenye mashindano hayo ni Abubakari Hasimu – wa TSC Academy ambaye alipewa zawadi ya kipa bora na vifaa vyenye thanmani ya EURO 400 kutoka kwa kampuni ya kutengeneza vifaa vya magolikipa hapa Ujerumani.

 Pia wachezaji wengine ni, Miraji Madenge, Striker, Karlos Protus Centre back, Emily Mugeta left back, frank Sekule, Japhet Makalai na Saidi Juma.

Pamoja na kuwa kivutio kwa watu huku Ujerumani pia tumeweza kuitangaza nchi yetu na mpira wetu vizuri sana, kwani watoto na watu wazima wamekuwa wakitusupport sana, na kuchangia vitu mbalimbali vikiwemo viatu na mipira.

Lalini pia tumeweza kutembelea mashule mambalimbali na kifanya presentation juu ya mradi wetu wa michezo, ikiwa ni pamoja na kuwaonyesha video mambalimbali za maisha ya nyumbani kuhusiana na soka, elimu na maisha ya kila siku, baadhi ya shule tulizo tembelea ni mapoja na shule za primary, secondary na chekechea. Pia tuliwafundisha kupika ugali, kushona mipira na vitu vingine vingi.

Pia tulikaribishwa kwenye hafla zote na mameya wa miji tuliyotembelea na kucheza mashindania, Meya wa Mannheim, Meya wa Brackenheim, na meya wa Wurzbarg

Asante story na
Mutani Yangwe
Mkurugenzi TSC.

Thursday, August 2, 2012

MAHOJIANO NA JOHNSON MZAVA NA NYIMBO ZA INJILI MJINI WASHINGTON DC

Mahojiano  na Aminiel Johnson Mzava. Pauline Johnson Mzava na Pastor Faye  Chandler  Washington DC wakiongelea uvumbuzi wa nyimbo za Injili.

  
Pauline Johnson Mzava (Kushoto) pamoja na Pastor Faye Pastor Faye Chandler, wakiimba nyimbo za injili ndani ya studio yao iliopo Washington DC.

Johnson Mzava akipata picha ya pamoja na mdhamini wa pendolake katikati pamoja na Pastor Faye Pastor Faye Chandler, wa kwanza kushoto pamoja na dogo Barack Johnson Mzava aliebebwa!

Johnson Mzava almarifu Aminiel, akizungumzia historia yake kwa ufupi, pamoja na uzinduzi wa Album ya nyimbo za Injili wakiwa pamoja na mdhamini wa pendo lake Pauline Johnson Mzava pamoja na pastor Faye Chandler jiji Washington DC Nchini Marekani  (Picha na http://swahilivilla.blogspot.com/)

REDDS MISS MWANZA 2012/13 KUFANYIKA AGOSTI 31


Pichani ni warembo walioshinda Miss Nyamagana 2012/13,


Pichani ni warembo walioshinda Miss Ilemela 2012/13
Mrembo wa mkoa wa Mwanza 2012/13 atapatikana ijumaa ya agosti 31 katika viwanja vya Yatch Club Mwanza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na muaandaji wa kampuni ya Sisi Entertainment John Doto, amesema shindano hilo linalovuta hisia za wengi ndani ya mkoa wa Mwanza na kanda ya ziwa kwa ujumla, litashirikisha warembo tariban 20 kutoka wilaya zote za mkoa Mwanza.

John Doto amesema warembo wote watakaa kambini kwa wiki mbili, ambapo kambi rasmi itaanza
tarehe 20 agosti mwaka huu katika hoteli ya Isamilo Lodge. Shindano la Redds Miss Mwanza 2012/13, lilisogezwa mbele kufuatia mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Wakiwa kambini warembo watapata fursa ya kujifunza Mitembeo, Tabasamu, ufahamu wa kujieleza pamoja na kuvumbua vipaji mbalimbali.

John Dotto pia amesema warembo watakua na ziara ya kwenda kwenye mbuga za wanyama Serengeti, kutoa misaada kwa watoto yatima, vikongwe pamoja na kufanya usafi kwenye moja ya Hospitali Jijini Mwanza na moja ya barabara za Mwanza.

Kwa miaka ya hivi karibuni, Mkoa wa Mwanza umekua ukitoa warembo wanaofanya vizuri
mashindano ya Taifa.

Itakumbukwa Mwaka 2008 Nasreem Karim na Mwaka 2009 Miriam Gerald waliweza kushika Mataji ya Miss Tanzania wakitokea mkoa Mwanza.

WAANDISHI WA HABARI MARA KUSHUKA DIMBANI LEO

Na Shomari Binda
Musoma,


Kikosi cha maangamizi cha timu ya soka ya Waandishi wa Habari Mkoani Mara leo kitashuka katika uwanja wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare nje kidogo ya Manispaa ya Musoma kucheza mchezo wa kujipima nguvu ikiwa ni maandalizi ya Bonanza la michezo litakaloandaliwa na Waandishi wa Habari wa Mkoa huo katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Akizungumzia mchezo huo nahodha msaidizi wa kikosi cha wanahabari Mara Augustine Mgendi alisema maandalizi yote kuhusiana na mchezo huo yamekwisha kukamilika na kikosi kizima cha timu hiyo kipo tayari kwa ajili ya kukabiliana na wanachuo hao.

Alisema wachezaji wote wapo katika hali nzuri baada ya kufanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya mchezo huo na ameahidi kikosi hicho kufanya vizuri katika mchezo kama ambavyo wamekuwa wakifanya katika michezo yao iliyotangalia katika siku za nyuma.

Aliongeza kuwa tayari kikosi cha maangamizi cha timu ya wana habari kimeshawekwa hadharani ambacho kitashuka dimbani hapo kesho kwa ajili ya mchezo huo ambao umekuwa ni gumzo katika maeneo mbalimbali ya mji wa Musoma kutokana na tambo kutoka upande wa timu zote mbili.

Mgendi aliwataja wachezaji watakaoanza katika mchezo huo kuwa ni kipa Cales Katemana,Makiwa Jumanne,Mabere Makubi,,George Maratu,Thomas Dominic,Paschal Michael,Lima Masinde,Richard Luhende,Shomari Binda,Augustine Mgendi pamoja na Fazil Janja.

Wachezaji wengine wataokuwa katika kikosi hicho ni Patrick Derick,Ahmed Nandonde,Emanuel Chibasa,Bigambo Jeje,Maxmilian Ngesi,Ahmad Kitumbo,Maxmilian Dominick,Dick Mohamed pamoja na Robert Simkoko.

Huu utakuwa mchezo wa pili katika siku za hivi karibuni kwa kikosi hicho cha wanahabari Mara ambapo katika mchezo uliotangulia waandishi hao waliwaadabisha wahesabu fedha wa benki ya NBC tawi la Musoma kwa kuwatandika mabao 3-0 mchezo uliofanyika katika viwanja vya posta mjini Musoma.

Kwa upande wake Katibu wa timu ya Waandishi wa Habari Mara Beldina Nyakeke akizungumzia kuhusiana na Bonanza alisema lengo lake ni kuleta hamasa ya michezo katika mji wa Musoma na Mkoa wa Mara kwa ujumla na kuwaomba wadau mbalimbali wa michezo kutoa ushirikiano katika kufanikisha.

Bonanza hilo linatarajiwa kufanyika katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhamani kwa kushirikisha timu kutoka taasisi mbalimbali ambazo zitakuwa tayari katika kushiriki na litafanyika kwa siku moja.

Wednesday, August 1, 2012

SIKIA ALICHOONGEA NGASA NDANI YA SPORTS EXTRA KUHUSU KUUZWA KWAKE SIMBA KWA MKOPO

Mara baada ya taarifa kutoka kwenye mitandao mbalimbali zikimzungumzia MRISHO Khalfan Ngassa kuuzwa Simba kwa dau la Sh. Milioni 25 nao Azam kukiri kuwa tayari wamekamilisha dili Kipindi cha Sports Extra na Clouds Fm kimezungumza na wahusika kwa kina na kutoa uchambuzi wake kuhusu hilo sakata.
Bofya hapo juu kusikiliza...

NAIBU WAZIRI WA ARDHI AHUDHURIA MAADHIMISHO YA 50 SHULE YA MSINGI NYAKAHOJA MWANZA

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Goodluck Ole Medeye akishirikiana na ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza Mhashamu Yuda Thaddaeus Ruwa'ichi kukata keki ya kusherehekea Jubilee hiyo ya shule ya msingi Nyakahoja kutimiza miaka 50


Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Goodluck Ole Medeye (mwenye suti nyeusi katikati) pamoja na ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza Mhashamu Yuda Thaddaeus Ruwa'ichi wakiongozwa kuingia viwanja vya maadhimisho kusherehekea Jubilee ya shule ya msingi Nyakahoja kutimiza miaka 50


Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Goodluck Ole Medeye ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Jubilee hiyo ya shule ya msingi Nyakahoja kutimiza miaka 50 amewataka walimu kusitisha mgomo na kurejea kazini. Akisema kwamba walimu ni wazazi hivyo wanapaswa kuwa na utu, lakini pia wanapaswa kutambua kwamba mustakabali wa maisha ya wanafunzi yako mikononi mwao.


Masista na tabasamu la kutimiza miaka 50 Shule ya Msingi Nyakahoja.


Wageni na wazazi kwenye Jubilee hiyo.


Eneo mojawapo walioketi wanafunzi wa shule ya Msingi Nyakahoja.


Gwaride la wanafunzi wa Shule ya Msingi Nyakahoja wakitoa heshima wakati wa Wimbo wa Taifa la Tanzania.


Meza kuu na heshima za wimbo wa Taifa letu ndani ya Jubilee hiyo ya shule ya msingi Nyakahoja kutimiza miaka 50.


Gwaride la wanafunzi wa kike wa shule ya msingi Nyakahoja likipita heshima mbele ya halaiki ya watu waliohudhuria sherehe za kutimiza miaka 50 Shule ya msingi nyakahoja Mwanza. 


Hapa ni mwendo wa vipaji vya mmoja mmoja wanafunzi wa Prep Two.


Ni wanafunzi walioshiriki kama igizo flani hivi jukwaani kutoka kushoto ni Mwanafunzi, Dereva wa magari, Askari, Sister na Daktari kwenye pozi na flash ya blogu ya G. Sengo.


Kwaya ya Prep One.


Maigizo kijamii zaidi....


Ngoma za asili toka kwa wanafunzi wa shule ya msingi Nyakahoja zilihusishwa kwenye Maadhimisho ya 50.


Mc Mahiri mwenye sauti ya 'radi' Baba Paroko aliyesimamia zoezi hilo kikamilifu Mwanzo mwisho.


Ngoma iliyotia fora ndani ya maadhimisho hayo ya 50.


Mke wa Katibu Mkuu wa Chama cha CHADEMA Dk.Wilbroad Slaa, Josephine Slaa akimpa mkono ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza Mhashamu Yuda Thaddaeus Ruwa'ichi  kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari wasichana ya nyakahoja, harambee iliyofanyika ndani ya Jubilee hiyo ya shule ya msingi Nyakahoja kusherehekea kutimiza miaka 50


Watoto wetu wakipata flash na blog yako.


Nikiwa na second bon wangu Cuthbert anayesoma shuleni hapo.