ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 2, 2012

IVORY COAST YAIFUNGA TANZANIA 2-0

Copa
Kolo, Gosso, Souleman, Tiene
Gradel, Bony, Tiote, Yaya
Drogba, Gervinho

COTE D'IVOIRE
Kaseja
Cholo, Morris, Maftah, Nyomi
Kazimoto, Salum, Nurdin, Mkude
Mbwana, Ulimwengu

TANZANIA









Mpira umeisha katika uwanja wa Felixs Houphouet Boigny mjini Abdijan nchini Ivory Coast  kati ya timu ya taifa la Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya taifa hilo. Ivory Coast walijipatia bao la kwanza kwenye dakika ya 15 kipindi cha kwanza kupitia mchezaji Solomon Kalou, aliyetumia vyema makosa ya mabeki wa Taifa Stars waliojisahau na kucheza bila uelewano mara kadhaa, hivyo hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Ivory Coast walikuwa wakiongoza kwa bao hilo.

Kipindi cha pili dakika ya 70 Taifa Stars inacheza pungufu mara baada ya mchezaji wake kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na hatimaye akazawadiwa kadi nyekundu, muda mfupi baadaye (dakika ya 80) Didier Drogba akapachika bao la pili.
Didier Drogba

Huu ni mchezo wa kwanza kwa Didier Drogba kuonekana katika dimba la nyumbani tangu kuisaidia klabu yake ya Chelsea kushinda kombe la Uefa Champions League mwezi uliopita kitu ambacho kilitarajiwa kuwa chachu kwa mashabiki wake wa nyumbani kumshangilia kwa nguvu shujaa wao na ndivyo ilivyokuwa leo.

MISS NYAMAGANA KABAaaaaaAAAA HUYU HAPA...

Miss Nyamagana 2012 ni Aisha Eddy (katikati) akifuatiwa na Messy na  Happy Daniel.

Hawa ndiyo wanyange wote wa kinyanganyiro cha miss Nyamagana 2012.

Washereheshaji wa tukio sis Lulu Sanga na Masanja Mkandamiza wa OK.

Majaji: Kutoka kulia ni Mr. Geoge Greek (Rock Bottom Club), Mr. Meshack Bandawe (PPF), Lyn Dunn (Monarch Hotel & Pavallion) na  Ester wa Mwanza View.

 Majaji: Kutoka kulia ni Gabriel Lyotam (Sahara Media Group), Ester wa jarida la Mwanza View na Lyn Dunn (Monarch Hotel & Pavallion) 

Ze pipo in da area.....

Meza ya moja wa wadhamini miss Nyamagana 2012 (Sahara Media Group) wakiongozwa na Mr.Rafael Shilatu (mwenye t-shirt nyeupe).

Ze anaza area

Meza ya wadahamini wakuu kupitia kinywaji cha Reds TBL.

Kutoka kushoto ni wajasiliamani maarufu  jijini Mwanza, 'Wity' wa Whitney Fashion, 'Fulo' wa Flora Salon na Shost wao wakifuatilia yanayojiri.

Mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga akifungua mashindano.

Mwanamuziki toka nchini Tanzania Ditto akitoa burudani.

Flowers...

Free style...

Mwanamuziki toka nchini Tanzania mzaliwa wa Mwanza, Hafsa Kazinja akitoa burudani kwa wahudhuriaji miss Nyamagana 2012 ambapo alikosha vilivyo kiasi cha kurejea tena kutoa burudani.

Mc Masanja Mkandamizaji hakuona nongwa kujumuika katika dance la madensa wa Hafsa Kazinja.

Show ya kwanza kwa mwanadada Linnah tangu alipodondoka toka nchini Marekani ameifanya mkoani Mwanza ndani ya Miss Nyamagana.

Flowers part two'

Rais wa Channel Africa Muddy Mtabora naye alikuwepo...

G and Platnum

Mkurugenzi wa F-Pluss Entertainmen Mr. Promo aka Fabian Fanuel naye alikuwepo.

Miss Tanzania 2011-2012 Genevive Mpangala akiuliza maswali washiriki walioingia Top 5.

Chief Judge Mr. Meshark Bandawe akitoa matokeo.
Do you know who is miss photo gennic?



 Aisha Eddy ambaye pia ni hatimaye alitawazwa kuwa Miss Nyamagana 2012, ndiye awali aliye nyakuwa taji la Miss photo Genic toka PHOTO SPOT.


Aliyekuwa Miss Nyamagana akiwa katika poz tayari kulivua taji la hilo, Ni mrembo ambaye pia anashikilia taji la Miss Mwanza ambalo siku si nyingi atalikabidhi kwa mrembo wa mchuano ujao.


Mwandaaji wa shindano hilo Muhksin Mambo toka Stopers Entertainmen akikaribishwa kusema jambo na Mc. Masanja Mkandamizaji.

Masanja Mkandamizaji akipata flash na www.gsengo.blogspot.com.

Winners...

Picha ya washindi na majaji.

HIKI HAPA KIKOSI KITAKACHO IVAA IVORY COAST LEO

Kocha Kim Poulsen ametaja kikosi cha Taifa Stars ambacho leo (Juni 2 mwaka huu) kitakuwa uwanjani kwenye Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny jijini Abidjan kuivaa Ivory Coast katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia.
Amefanya mabadiliko katika nafasi mbili kwenye kikosi ambacho Mei 26 mwaka huu kilicheza mechi ya kujipima nguvu na Malawi (The Flames) iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa suluhu. 

Amir Maftah atacheza beki wa kushoto badala ya Waziri Salum wakati Mrisho Ngasa atakuwa mmoja kati ya washambuliaji wa mwisho. Ngasa atacheza nafasi ya Haruna Moshi ambaye hayuko na Stars hapa baada ya kuumia mazoezini siku moja kabla ya safari.

 Kikosi kamili cha Taifa Stars ambayo itatumia mfumo wa 4-4-2   ni kama ifuatavyo:- 
Kipa; Juma Kaseja 
Mabeki; Shomari Kapombe, Amir Maftah, Aggrey Morris na Kevin Yondani 
Viungo; Shabani Nditi, Salum Abubakari, Frank Domayo na Mwinyi Kazimoto 
Washambuliaji; Mbwana Samata na Mrisho Ngasa 
Wachezaji wa akiba; Mwadini Ali, Waziri Salum, Juma Nyoso, Erasto Nyoni, John Bocco, Simon Msuva, Jonas Mkude, Christopher Edward na Ramadhan Singano. 

Kim amesema kikosi chake kimejiandaa vizuri kwa ajili ya mechi hiyo, na kilichobaki ni kwa wachezaji kudhibitisha maandalizi hayo kwenye dakika 90 za mchezo huo utakaoanza saa 11 kamili jioni (nyumbani itakuwa saa 2 kamili usiku). Mechi hiyo itaoneshwa moja kwa moja (live) kupitia televisheni ya RTI ambapo itaonekana katika nchi 58 duniani.

Mwamuzi; Slim Jedidi (Tunisia) 
Mwamuzi msaidizi namba 1; Bechir Hassani (Tunisia) 
Mwamuzi msaidizi namba mbili; Sherif Hassan (Misri) 
Mwamuzi wa akiba; Youssef Essrayri (Tunisia) 
 Mtathmini wa waamuzi; Rachid Medjiba (Algeria) 
Kamishna wa mchezo; Saleh Issa Mahamat (Chad)

Friday, June 1, 2012

TBF OFFICIALS AND HASHEEM THABEET @US EMBASSY AND KIPINGU's SCHOOL

 TBF Officials Magesa and Maluwe, Hasheem Thabeet and US Cultural Affairs Officer Ms. Dana Banks at US Embassy today , US Embassy hosted us today, donated 50 balls and signed a grant.

 TBF Vice President Phares Magesa exchanging grant documents with US Cultural Affairs Officer Ms. Dana Banks at US Embassy to support part of costs of Under 17 Arusha Basketball Clinic to be conducted by Coach Greg Brittenham on 9-10 June 2012.

 At Kipingu's School Lord Barden Powell High School, School Director Col. Iddi Kipingu, Hasheem, Magesa and another tallest player in the country Julias Charles who is a student at Kipungu's school.

Hasheem talking to students at Lord Barden Powell High School.
 
 
Date: 31/05/2012

US Embassy in Dar Es Salaam today hosted Hasheem Thabeet and TBF Vice President Phares Magesa who was accompanied by TBF Assistant Secretary General Michael Maluwe, TBF Treasurer Ms. Marry Mbaga.

The US Embassy thanked Hasheem for agreeing to conduct basketball clinics in Tanzania.


During the event US Embassy in Dar donated 50 balls to be used at Under 17 basketball Clinic to be held in Arusha June 9-10, 2012.


Cultural Affairs Officer and first Secretary of the US Embassy in Dar Es Salaam Ms. Danna Banks handed over the balls to TBF Vice President Phares Magesa in the presence of NBA Player Hasheem Thabeet, Portland Trail Blazer Centre.


Also the US state department through US Embassy in Dar es Salaam has given a grant to support administrative cost of running the Arusha Clinic, the grant was signed today by Mr. Magesa and Ms. Banks at the Embassy.


The Arusha Clinic will be conducted by one of the very best US based coach details will be released later.


After the event at the Embassy Hasheem and Mr. Magesa went to Lord Barden Powell High School in Bagamoyo.


Hasheem promised to support various school projects including building of modern basketball court for the school, Col. Kipingu is the one who gave Hasheem the first schorlaship to study at Makongo Secondary when Kipingu was Head Master of that School early 2000.

On behalf of TBF we thank Hasheem for this great initiative.

Hasheem is in the country to conduct a clinic for 200 kids from 6 regions to be held at Don Bosco grounds on 1st and 2nd June, 2012.


We call upon other organizations to join us in developing our youth through various programmes like youth clinics, basketball courts construction/refurbishment etc.


Thank you,


Phares Magesa

TBF-Vice President

MISS UNIVERSE 2011 ‘NELLY KAMWELU’ KUCHANGIA MFUKO WA SARATANI YA MATITI

 
MISS UNIVERSE 2011 ‘NELLY KAMWELU’ KUCHANGIA MFUKO WA SARATANI YA MATITI

Mrembo anayeshikilia taji la Miss Universe Tanzania 2011/2012 Nelly Kamwelu kwa kushirikiana na Mfuko wa Saratani ya Matiti Tanzania (Breast Cancer Foundation) wameandaa hafla kwa ajili ya harambee ya kuchangia mfuko wa saratani ya matiti itakayofanyika tarehe 1/6/2012 siku ya Ijumaa katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam kuanzia saa moja jioni hadi saa nne usiku.

Vilevile katika hafla hiyo kutakuwa na mnada wa kito cha Tanzanite ambayo imetolewa maalum na kampuni ya Richland Resources kwa ajili ya kuchangia mfuko huu. Pia picha ya Mrembo wa Miss Universe Tanzania itanadiwa katika mnada huo.

Mrembo Nelly Kamwelu toka achukue taji la Miss Universe Tanzania 2011, amekuwa akifanya kazi bega kwa bega na mfuko wa saratani ya matiti ikiwamo kusaidia kutoa elimu katika shule mbalimbali ili kupunguza au kutokomeza uwezekano wa kuenea kwa saratani ya matiti. Mfuko huu umepanga kuendeleza elimu hii kwa shule za mikoa ya Mbeya, Ruvuma, Rukwa, Iringa, Mtwara na Lindi.

Kwa kusindikiza hafla hii kutakuwa na maonyesho ya mavazi yaliyotolewa na wabunifu wa hapahapa nchini ambao ni Escado Bird, Kemi Kalikawe na Subira Wahure vilevile kutakuwa na burudani ya muziki kutoka msanii Enika na mchekeshaji Evans Bukuku. Pia mrembo mwenyewe Nelly Kamwelu atatoa burudani ya dansi aina ya Belly Dance.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na waandaji wa Miss Universe Tanzania tell: 0714 441165 Mwanakombo Salim (Mratibu wa Kitaifa)