ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 22, 2012

TUENDELEE KUMSAIDIA ANASTAZIA

*Pichani anaonekana Augustine Mgendi, akimkabidhi Mama wa binti anayeumwa Anastazia kiasi cha shilingi 10,000 fedha iliyotolewa na mama Abduweli wa Bandari ya Dar es Salaam, baada ya kukabidhi fedha hizo mama huyo alishukuru na kusema kuwa itasaidia kupiga Xray kwani hakuwa na kiasi cha shilingi 10,000 kupiga  X ray.

Jana Augustin Mgendi alituma habari na Picha za Anastazia binti anayesumbuliwa na uvimbe wa Mguu wa kushoto ambapo amekosa fedha za kupata angalau matibabu ya awali, napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wale wote walioonyesha kuguswa na habari hii na mpaka sasa kuna wengine wametuma na wemetoa ahadi ya kutoa fedha za kumsaidia Anastazia.

Mpaka sasa Mama Abduweli wa Mamlaka ya banadari Dar es Salaama mwenye namba 0713 689656 ametuma kiasi cha shilingi 10,000 huku dada Edna John kutoka Uingereza aliyesoma Blog ya Michuzi amesema atatuma fedha za kumsaidia Anastazia kwenye akaunti.

Hivyo basi watanzania tuendelee kumsaidia Annastazia ili aweze kurudi katika hali yake ya kawaida aungane na ndugu zake katika ujenzi wa familia yake,kama unamchango wowote unaweza kupitishia katika akaunti 022201093996 NBC au katika simu namba 0756 035 825

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.