ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 14, 2012

TAIFA STARS YAIDUNGUA HARAMBEE STAR 1-0 CCM KIRUMBA MWANZA

Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, leo imeibika na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Harambee Stars ya Kenya katika mchezo wa Kimataifa uliokwenye kalenda ya FIFA uliofanyika leo katika uwanja wa CCM kirumba jijini Mwanza.

Kikosi cha Harambee Stars ya Kenya katika mchezo wa Kimataifa uliokwenye kalenda ya FIFA uliofanyika leo katika uwanja wa CCM kirumba jijini Mwanza ambacho kimefungwa 1-0 na Tanzania.
Mgeni rasmi wa pambano la kimataifa la kirafiki kwa mujibu wakalenda ya FIFA, Mkurugenzi wa jiji la Mwanza (wa tatu kushoto) akiwa katikapicha ya pamoja na viongozi wa TFF, FKF, MZFA, IDFA na kamishna mechi wakati nyimbo za mataifa hayo mawili zikipigwa.

Mgeni rasmi wa mchezo huo mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe akisalimiana  na wachezaji wa timu ya Taifa ya Kenya 'Harambee Stars'

Mgeni rasmi wa mchezo huo mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe akisalimiana  na wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'.

Kapteni wa Harambee Stars Denis Oliechi akiwaongoza wachezaji wenzake kukisalimiana na wenyeji wao Taifa Stars katika mechi ya kirafiki inayotambuliwa na FIFA iliyochezwa leo dimba la CCM kirumba Mwanza, Mbwana Samata ndiye alikuwa wa mwisho kusalimiwa pichani. Matokeo Taifa Stars waliibuka na ushindi wa 1-0.

Salaam muhimu.. ni baina ya Taifa Stars na Harambee Stars.

Mgeni rasmi wa mchezo huo mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe akisalimiana na Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen kabla ya mchezo kuanza.

Ilikuwani kona ndogo iliyochezwa vyema na Amir Maftah wakigongeana na Thomas Ulimwengu kisha mpira ukarudi kwa Maftah akamimina fupi ya juu ikamkuta beki wa timu ya Taifa ya tanzania 'Taifa Stars' Aggrey Moris (aliyeruka juu) aliyekuwa katikati ya mabeki wa Harambee Stars akatumia ufundi kuukwamisha mpira wavuni.

Bao la Stars lilipatikana mapema tu katika dakika ya 5 na sekunde kadhaa kipindi cha kwanza mfungaji akiwa ni Agrey Moris na kufanya timu hizo zikienda mapumziko Stars ikiwa mbele matokeo yaliyodumi hadi kumalizika kwa mchezo huo. 


Wachezaji wa Tanzania na sherehe  za goli.

Mfungaji wa goli la ushindi kwa Tanzania Aggrey Morris (6) akiserebuka na wachezaji wenzake mara baada ya kuipatia timu yake goli dakika ya tanotu ya mchezo.

Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania Simon Msuva akijaribu kutafuta mbinu za kumtoka mlinzi wa timu ya taifa ya Kenya Christopher Wekesa katika mechi ya kirafiki ya kimataifa ambapo Taifa Stars iliibuka na ushindi wa bao 1- 0.

Wanahabari wakitimiza wajibu wao wa kuripoti nao walijikuta wakipigwa picha ya matukio mbalimbali yaliyokuwa yakijiri katika uwanja wa CCM Kirumba katika mechi ya kirafiki ya kimataifa baina ya Taifa Stars 'Tanzania' na Harambee stars 'Kenya'.

Muosha huoshwa...! Mpiga picha wa kituo cha televisheni cha Star TV akiweka sawa na hatimaye kunaswa na blogu ya G. Sengo.

Mashabiki wa Taifa Stars waliokuwa wameketi katika jukwaa la mashabikiwa wa Simba wakifuatilia mtanange huo ambapo ushirikiano ulikuwa asilimia mia. 

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' akizungumza na waandishi wahabari mara baada ya mchezo kumalizika kwa timu yake kuibuka na ushindi.. Kumsikiliza Bofya Play...
Nyomi na shangwe zake.......baada ya goli.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.