ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 21, 2012

TAIFA STARS KUONDOKA KESHO KUELEKEA CECAFA UGANDA, MASHABIKI MWANZA WAJIPANGA KWENDA KUTIA HAMASA.

 Kocha Kim Poulsen amekiri kuwa Stars kuweka kambi yake jijini Mwanza hakika lilikuwa ni wazo sahihi kwani hamasa imeongeza  kwa wachezaji wake na hata walimu nao wanaahidi kuhakikisha wanacheza kufa na kupona kwenye michuano hiyo kwa nia ya kuiletea sifa nchi ya Tanzania. Haya yamejiri kwenye hafla ya kuwaaga wachezaji wa kikosi chetu kinachoelekea Kampala nchini Uganda hapo kesho.


Mwakilishi wa Vilabu Mkoa wa Mwanza kwenye Mkutano Mkuu wa TFF Taifa Bw. John Kadutu (pichani mwenye miwani) licha ya kusema kuwa MZFA imejipanga kuhakikisha mpira Mkoa wa Mwanza unakua kwa kasi na kuzalisha wachezaji wengine kwa maslahi ya Timu za Taifa na vilabu mbalimbali pia alikuwa na nyongeza hii kwa mashabiki kuelekea nchini Uganda kushuhudia michuano ya CECAFA



Wachezaji a timu ya Taifa Tanzania bara pamoja na viongozi wakijadiliana na mastori kwenye hafla ya kuwaaga wachezaji wa kikosi kinachoelekea Kampala nchini Uganda hapo kesho..


Baadhi ya wachezaji wa Kilimanjaro Stars na viongozi wa soka Mwanza.


Hewa safi ya Hoteli Tilapia....na kuchati kwa chati....


Refreshment  kandokando ya ziwa Victoria


Fun 


Old is good..


Yes we are...


Bariz za hapa na pale....


Picha ya pamoja kati ya Kilimanjaro Stars na viongozi wa soka mkoa wa Mwanza MZFA

WAKATI huo huo chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) kimewataka mashabiki wanaohitaji kwenda kuishangilia na kuipa hamasa timu ya Taifa ya Kilimanjaro Stars inayoshiriki michuano ya CECAFA Challenge Cup 2012 inayotaraji kuanza jumamosi ya Novemba 24 mwaka huu Jijini Kampala nchini Uganda kujitokeza kwa wingi na kuonana na uongozi wa MZFA kwaajili ya taratibu za safari.

Kwa mujibu wa Katibu wa MZFA Bw.Nasbu Mabourk amesema kuwa  maandalizi ya taratibu za kupeleka washabiki nchini Uganda kuishangilia Kilimanjaro stars katika kila mechi itakazocheza zimekwisha kamilika na kuahidi kutoa gharama halisi ya kwenda nchini humo siku ya ijumaa, ikiwa ni pamoja na ile ya hati ndogo ya kusafilia toka Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mwanza  zitakazoratibiwa na MZFA kwa ajili ya kuwarahisishia mashabiki na kuwaondolea usumbufu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.