ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 17, 2012

MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MWILI WA MAREHEMU MMACHINGA ALIYEUAWA KWA RISASI, MWILI WASAFIRISHWA LEO KUELEKEA KIBONDO.


Mstahiki meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula ambaye pia ni diwani wa kata ya Mkolani (CCM) akizungumza na wakazi wa Isegege 'A'  kata ya Mahina jijini Mwanza wakati wa ibada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Daudi Balenga Patrick (28) maarufu kwa jina la 'Greda' mmachinga aliyeuawa kwa risasi hivi majuzi kwenye purukushani za wamachinga na mgambo wa jiji la Mwanza. Ipate sauti Bofya Play.


Wakazi wa Isegege 'A'  kata ya Mahina jijini Mwanza waliokusanyika wakimsikiliza mheshimiwa Mstahiki Meya wakati wa ibada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Daudi Balenga Patrick (28) maarufu kwa jina la 'Greda' mmachinga aliyeuawa kwa risasi hivi majuzi kwenye purukushani za wamachinga na mgambo wa jiji la Mwanza.


Diwani wa kata ya Igoma Adam Chagulani (CHADEMA) akiongoza safu ya viongozi nyuma yake akifuatiwa na Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula kwenye hatua za wanajamii kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Daudi Balenga Patrick (28) maarufu kwa jina la 'Greda' mmachinga aliyeuawa kwa risasi hivi majuzi kwenye purukushani za wamachinga na mgambo wa jiji la Mwanza.


Bi. Flora Michael ambaye ni mke wa marehemu akilia kwa uchungu wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu mumewe Daudi Balenga Patrick (28) maarufu kwa jina la 'Greda' mmachinga aliyeuawa kwa risasi hivi majuzi kwenye purukushani za wamachinga na mgambo wa jiji la Mwanza.


Akina mama wakishiriki kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Daudi Balenga Patrick (28) maarufu kwa jina la 'Greda' mmachinga aliyeuawa kwa risasi hivi majuzi kwenye purukushani za wamachinga na mgambo wa jiji la Mwanza.


Ibada ya kutoa heshima za mwisho ikiendelea ambapo halmashauri ya jiji la Mwanza pamoja na kutoa usafiri (gari) kuusafirisha mwili wa marehemu hadi kijijini kwao Kumuhasha wilaya ya Kibondo kata ya Murungu mkoani kigoma, pia imetoa kiasi cha shilingi 500,000/= kama ubani kwa msiba huo uliotokea.


Marafiki wakiuaga mwili wa mpendwa wao.


Vijana wa kata hiyo nao wamehudhuria ...


Utaratibu wa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Daudi Balenga Patrick (28) maarufu kwa jina la 'Greda' ukiendelea.


Bi. Flora Michael ambaye ni mke wa marehemu akilia kwa uchungu huku akisaidiwa na nduguze.


Msemaji wa familia Bw. Onesmo Birago ambaye ni babu wa Marehemu akitoa utaratibu wa ndugu na jamaa watakao ambatana kuusafirisha mwili huo hadi  kijijini kwao Kumuhasha wilaya ya Kibondo kata ya Murungu mkoani kigoma kwaajili ya mazishi.
Mzee Patrick Balenga ambaye ni baba wa marehemu (wa tatu kutoka kushoto mwenye koti) akiwa na watoto wake sita waliobakia. Marehemu Daudi 'Greda'alikuwa ni mtoto wa kwanza.

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. Calabash Style Sea food - What on earth is
    it About?

    Feel free to visit my web site ... attorney leads
    Also visit my homepage ... lawyer search engine optimization

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.