ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 22, 2012

ASHANTI NOMA YATEMBEZA BAKORA KUMI KWA MORO UNITED



TIMU ya Ashanti United jana iliivurumisha bila huruma Moro United mabao 10-1 kwenye mchezo wa ligi daraja la kwanza uliochezwa uwanja wa Karume, jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo ambao ulionekana dhahiri kuwa wa upande mmoja kutokana na wachezaji mahiri wa Moro United kutokuwepo, Ashanti walikwenda mapumziko wakiwa wanaongoza mabao 5-1.

Lambele Jerome 


Moro ambayo mlinda mlango wake alikuwa bonge la mtu alikuwa akijigararagaza kila wakati kwa madai akaumia.

Mabao ya Ashanti yalifungwa na  Lambele Jerome alifunga mabao sita dakika ya 35, 52, 71, 76, 81 na 89, Shabani Hatibu alifunga matatu dakika ya nane, 11 na 37, na Raju Mahmoud dakika ya 16.

Bao la Moro United lilifungwa kwa njia ya penalti  na Twahir Kiparamoto dakika ya 21.

Kwenye uwanja wa Mabatini mkoani Pwani Green Warriors na Polisi Dar es Salaam zilitoka sare ya kufungana bao 2-2.

Mabao ya Green Worriors yalifungwa na Said Asaa dakika ya 80  Edward Kheri dakika ya 89. 


 ZAIDI TEMBELEA http://pallangyor.blogspot.com/

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.