ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 31, 2012

BANK OF AFRICA TANZANIA SASA KUSHIRIKIANA NA AIRTEL TANZANIA KATIKA KUTOA HUDUMA YA AIRTEL MONEY NA UTOAJI MIKOPO KWA WASAMBAZAJI WAKUBWA WA HUDUMA YA AIRTEL MONEY

Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando (kushoto) akiongea wakati  wa uzinduzi wa ushirikiano wa kampuni ya simu za Mkononi ya Airtel na Bank of Afrika katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi ya bank hiyo yote yaliyopo Tanzania. Uzinduzi huo ulifanyika jana katika Makao makuu ya Airtel Morocco Jijini Dar es Salaam. pichani kulia ni mkuu wa kitengo cha IT Bank of Afrika bwn. Willington Munyanga , akifatiwa na  Mkuu wa huduma za kibenki Mwanahiba Mzee  na anayefatia ni Meneja Airtel Money John Ndunguru.


Meneja Airtel Money John Ndunguru na Mkuu wa huduma za kibenki Mwanahiba Mzee  kwa pamoja wakikabidhiana mikataba mara baada ya makubaliano ya ushirikiano  wa Airtel na Bank of Afrika katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi ya bank hiyo yote yaliyopo Tanzania. Makabidhiano hayo yalifanyika jana katika Makao makuu ya Airtel Morocco Jijini Dar es Salaam. wakishuhudia Katikati ni Mmoja ya wakala mkubwa wa Airtel money kutoka kampuni ya Connexions bwn Shyamkumar Balakrishnan (katika) na kushoto ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando

Meneja Airtel Money John Ndunguru na Mkuu wa huduma za kibenki Mwanahiba Mzee wakipitia mkataba mara baada ya makubaliano ya ushirikiano  wa Airtel na Bank of Afrika katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi ya bank hiyo yote yaliyopo Tanzania.


BANK OF AFRICA TANZANIA SASA KUSHIRIKIANA NA AIRTEL TANZANIA KATIKA KUTOA HUDUMA YA AIRTEL MONEY NA UTOAJI MIKOPO KWA WASAMBAZAJI WAKUBWA WA HUDUMA YA AIRTEL MONEY

Dar es Salaam, 30 Oktoba 2012

Huduma bora na ubunifu wa huduma mpya zinazokidhi matarajio ya wateja ni moja ya silaha muhimu katika kukuza wateja waliopo pamoja nakuongeza idadi ya wateja wapya, Kutokana na msingi huu BANK OF AFRICA TANZANIA ina furaha kuanzisha ushirikiano na AIRTEL TANZANIA katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi yake yote yaliyopo Tanzania.
Ushirikiano huu wa kibiashara unatoa fursa kwa wasambazaji wa huduma za Airtel Money kupata PESA za mtandao pasipo usumbufu wowote. Katika tukio la leo baina ya BANK OF AFRICA na AIRTEL TANZANIA tunapenda pia kutangaza uanzishwaji wa mikopo kwa wasambazaji wa Airtel money ili kukuza mitaji itakayowawezesha kulikabili soko  shindani la biashara hii.
Makubaliano haya yanayotiwa saini leo yanaendelea kuboresha huduma za kifedha zitolewazo kupitia mitandao ya simu za mkononi kupitia BANK OF AFRICATANZANIA. Ushirikiano huu wa Huduma ya Airtel money unawalenga mawakala wakubwa na wa kati pamoja na wasambazaji wadogo  wa Airtel Money  katika kupata pesa za mtandao zitakazowawezesha kuendesha biashara zao kwa ufanisi zaidi, sambamba na hilo pia Mawakala na wasambazaji wa Airtel Money watapatiwa mikopo itakayowawezesha kukuza biashara zao, mikopo hiyo itakuwa kati ya shilingi  Millioni 10 hadi 100.

Kwa upande wake Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Airtel Money Godfrey Mugambi amesisitiza kwamba  ushirikiano wa Airtel Tanzania na BANK OF AFRICA TANZANIA  ni moja ya mkakati wa kampuni yake katika kuendelea kuboresha na kufikisha huduma za kifedha nchini kote. Hii ni njia rahisi sasa itakayowawezesha wasambazaji wetu wa Airtel Money wakubwa kuwafikia mawakala wengi na kuokoa muda na  gharama walizokuwa wanazipata kutafuta  pesa za mtandao. Airtel inatambua ongezeko la mahitaji ya huduma za kifedha zenye usalama, uhakika, katika soko la Tanzania na ni kwa sababu hizi  Kampuni ya Airtel imeingia makubaliano na BANK OF AFRICA TANZANIA kutoa huduma ya Airtel Money  nakurahisha zaidi upatikanaji wa huduma hii kwa wateja.

Huduma za Airtel Money  zitawawezesha  makundi yote nchini yaani yale yaliyofikiwa na taasisi za kifedha kama mabenki  na yasiyo fikiwa na mabenki kupata huduma za kifedha kwa  urahisi Kupitia mtandao wa simu ya mkononi.

Aidha Huduma ya Airtel Money inatoa fursa kwa taasisi, mashirika mbalimbali, kujenga uwezo wa matumizi makubwa ya teknologia ikiwa ni pamoja na kurahisisha huduma za mfumo wa malipo kwa ajili ya bidhaa au huduma mbalimbali.

Huduma za Airtel Money zinapatikana nchi nzima kwa wateja wote wa malipo ya kabla na ya baadaye,  Airtel money ina  mawakala zaidi ya elfu 20,000 nchi nzima  wakitoa huduma mbalimbali ikiwemo kuwaunganisha  Wateja na huduma ya Airtel Money bure bila ya malipo ya uandikishwaji.

Historia Fupi ya BANK OF AFRICA
BANK OF AFRICA ilifungua milango yake kwa wateja kwa mara ya kwanza mnamo mwaka  1982 ikiwa na makao yake makuu  Bamako, Mali. Kwa sasa kundi hili la mabenki lina wafanyakazi wapatao  4,000  ambao wanafanya kazi  katika nchi  15 .

BANK OF AFRICA kwa sasa inafanya shughuli zake  katika nchi za Africa   na barani Ulaya  zikiwemo  Benin, Burkina Faso, Burundi, Djibouti, DRC, France, Ghana, Ivory Coast, Kenya, Madagascar, Mali, Niger, Senegal, Tanzania pamoja na  Uganda. BANK OF AFRICA imejipanga na inatambulika zaidi kwa ubora wake katika maeneo yafuatayo 

  • Huduma bora kwa wateja
  • Wafanyakazi hodari na wanaofikika kwa Urahisi
  • Uimara wa mtaji
  • Mtandao wa matawi unaokua kwa kasi
  • Utaalamu wa  uboreshaji wa huduma za kifedha
  • Wawekezaji wa uhakika

BANK OF AFRICA ina wawekezaji  wa uhakika ambao ni pamoja na  BMCE Bank (Banque Marocaine du Commerce Exterieur - BMCE), PROPARCO, IFC (International Finance Corporation), West African Development Bank, Netherlands Development Finance (FMO), Belgium Investment Company for Developing Countries (BIO) and investment fund AUREOS. 
BANK OF AFRICA TANZANIA  ina mtandao wa matawi 17  ambapo  10 yanapatikana mkoani Dar es Salaam na   mengine 7 katika mikoa ya  Arusha, Mwanza, Kilimanjaro (Moshi), Morogoro (Morogoro mjini na  Mtibwa), Mbeya na Tunduma.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.