ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 11, 2012

MWANZA HOTEL YAFUTURISHA

                                         Kilichozungumzwa Futarini.
Mkurugenzi wa New Mwanza Hotel Bw. Christopher Mwita Gachuma akihojiwa na mtangazaji wa Metro Fm mara baada ya kufuturu, pembeni akishuhudiwa na Mwakilishi wa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza (RPC) Kamanda Rashidi na moja kati ya Wazee Maarufu jijini Mwanza.


Shekhe Mkuu wa Mkoa na Kadhi wa mkoa wa Mwanza Alhaji Fereji akitoa salamu kwa waislamu na wageni waalikwa baada ya futuru jana jioni ndani ya Mwanza Hotel.


Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza kwenye hafla hiyo fupi ya futuru iliyoandaliwa na Bw. Mwita Gachuma.


Baadhi ya waalikwa wakipata futari...


Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza (kushoto), katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Bi. Joyce Masunga, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza (RAS) Bi. Doroth Mwanyika, Jaji mfawidhi wa Mahakama kuu kanda ya Mwanza Bi. Sumari na Katibu msaidizi CCM Sekretarieti ya Maadili Mkoa baada ya kupata futari iliyoandaliwa na Gachuma katika ukumbi wa Makutano uliopo ndani ya Mwanza Hotel jana. 


Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga akizungumzia kuhusu Sensa baada ya kumaliza kupata futari.


Mzee maarufu akiwa anafuatilia kwa makini salamu za Kadhi Mkuu na Shekhe wa Mkoa wa Mwanza Alhaji Fereji.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.