ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 28, 2012

YANGA BINGWA CECAFA 2012 BHAAAAASSsss..!!


Mashabiki wa Yanga mkoa wa Mwanza ambao walikuwa wakifuatilia mchezo huo kupitia luninga kwenye hoteli ya Annox iliyopo Furahisha Kirumba jijini Mwanza, wakishangilia mara baada ya timu yao kupachika bao la pili mfungaji akiwa Said Bahanuzi katika dakika ya 90. Hadi Mwisho Yanga iliibuka kwa ushindi kwa kuifunga Azam Fc 2-0

Kipre Cheche kulia Mchezaji wa timu ya Azam FC akikokota mpira mbelea ya beki wa Yanga Nidir Haroub Canavaro wakati wa mchezo wa fainali ya kombe la Kagame inayofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii, mpira umekwisha na timu ya Yanga imefanikiwa kutetea kombe la Kagame kwa mara ya pili mfurulizo baada ya kuitandika timu ya Azam FC goli 2-0 jioni hii.

Mashabiki wa timu ya Yanga wakishangilia mara baada ya timu yao kupata goli la kuongoza katika mchezo huo.
Mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadik akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Yanga na Azam FC pamoja na maafisa wa CECAFA na wachezaji wa timu zote mbili.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam akielekea kukagua timu kabla ya mchezo huo kuanza kulia ni , Crecentius Magori kushoto Makamu Mwenyekiti wa timu ya Yanga Clement Sanga na katikati ni Mwenyekiti wa Azam FC mzee Mohamed Said
Timu zikiingia uwanjani kuanza mpambano huo.
PICHA NA FULL SHANGWE.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.