ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 9, 2012

UKIKOSA SYRIA INTERNATIONAL EXHIBITION IN MWANZA USIJEKUJILAUMU MWANAWANE......!!!

Maonesho ya utamaduni na bidhaa za watu wa nchi ya Syria yanaendelea katika ukumbi mkubwa wa Gold Crest Hotel jengo la PPF barabara ya Kenyeta jijini Mwanza.

Bidhaa mbalimbali mapambo ukutani zinapatikana kwenye maonesho ambazo pia waweza kujinunulia. 

Perfumes na marashi mbalimbali yenye thamani yanapatikana hapa tena utanunua kwa vipimo. 

Suti kali rangi zote pia zipo. 

Mdau akionyesha pasi ya muundo wa kipekee yenye uwezo wa kunyosha nguo yenye kitambaa aina yeyote bila usumbufu hata vile vitambaa vyenye kuchagua pasi (hauhitaji kwenda dry creaner) inauzwa sh 65,000/= tu! 

Kushoto ni maboksi ya pasi zinazouzwa kwenye maonesho hayo ya Syria na kulia ni fagio/dekio maalum lisilotumia umeme lenye uwezo wa kufyonza uchafu aina zote, unakamua kwa kuvuta kishikio maalum 'hauhitaji kupinda mugongo mwanawane....' 

Akinadada wakijichagulia bangili, pochi, shanga, mikufu ya asili, hereni na mapambo ya ukutani ndani ya maonyesho haya. 

Vitendea kazi vyote vya jikoni, vikatio, vimenyeo na kadhalika. 

Hadi pipi... vitafunwa vyauzwa kwa kilogramu. 

Makobazi kwa wanaume yenye ubora wa hali ya juu bei poa. 

Sendoz nzuri kwa wanawake... 

Katika banda hili wadau wa Mwanza wakijinunulia poket na wengine wakanunua pochi. 

Mchuuzi katika pozi la kuwasikiliza wateja. 

Haya wale wa maharusi shela zinauzwa kwenye maonesho haya ya utamaduni wa watu wa Syria. 

Mavazi muntashar' kwa wanawake.

Soksi 'pure cotton' kwa watoto na watu wazima. 

Ushawahi ona sabuni za kuogea zinazotokana na malighafi ya miti asili na asali? 

Shanga, mikanda, bangili na na na na nanini...''' 

Maonesho ya wazi ya utamaduni wa Syria, yalioanza tarehe 1/05/2012 yanategemewa kufungwa rasmi tarehe 14/05/2012. Pliz' usije jilaumu kwamba sijakustua kwamba kuna mambo mazuri yanaendelea Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.