ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 6, 2012

RAIS WA MALAWI AFARIKI DUNIA

Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika amefariki dunia kwa mshuto wa moyo akiwa Johannesbuerg nchini Afrika Kusini alipopelekwa kwa matibabu.

Akiwa ameandamana na mkewe na jamaa zake wa karibu, rais huyo alisafirishwa hadi Afrika kusini katika hali ya usiri mkubwa huku akiwa hana fahamu.

Hali iliyozua hofu na utata mkubwa nchini Malawi kwani kwa muda mrefu kumekuwa na shinikizo za kumtaka Mutharika ang’atuke.

Awali afisa mmoja mkuu wa serikali ya Malawi alinukuliwa akisema kuwa Rais Mutharika mwenye umri wa miaka 78 aliangua akiwa katika makaazi yake rasmi na kupelekwa hospitalini ambako aliwekwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Kuhusu nani ataongoza taifa hilo fuatia kifo cha rais huyo, kulingana na katiba ya Malawi, Makamu wake Bi Joyce Banda atalazimika kushikilia hatamu za uongozi kwa kipindi kilichosalia .

Hata hivyo Bi banda na rais Mutharika walikuwa hawasikilizani kwani walikosana mwaka wa 2009 na Makamu huyo wa Rais akalazimika kuhamia upinzani.

RIP MUTHARIKA.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.