ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 6, 2012

TUZO ZA DIAGEO ZA WAANDISHI WA HABARI ZA BIASHARA AFRIKA 2012-ZAZINDULIWA RASMI.

Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Bi. Teddy Mapunda akifafanua kwa msisitizo namna ya kushiriki, kwenye uzinduzi wa tuzo za Diageo za Waandishi wa habari za Biasharara Afrika ((Diageo Africa Business Reporting Awards 2012). (Picha kwa hisani ya Michuzijr Blog)

----
*TUZO HIZI ZINAENZI UANDISHI WA HABARI ZA BIASHARA AFRIKA.

*Usajili wa tuzo sasa uko wazi kufanyika kwenye tovuti.

Kampuni ya Biaya Serengeti (SBL), ambayo ni kampuni tanzu ya Diageo, inayoongoza duniani katika biashara ya vinywaji vyenye kileo, leo wamezindua rasmi tuzo za habari za kibiashara kwa mwaka huu 2012.

Tuzo hizi zilianzishwa na Diageo mwaka 2004, kwa ajili ya kuwatambua waandishi wa habari na wahariri ambao wameweza kutoa taarifa zilizojitosheleza na za hali ya juu katika mazingira ya biashara Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Bi. Teddy Mapunda alisema“ Kampuni ya Diageo inaamini kwamba taarifa nzuri na zina mchango mkubwa wa kuinua mtazamo wa maendeleo na uchumi wa Afrika na changamoto zake.”

Habari hizo kwa kiasi kikubwa zinahamasisha nia ya kufanya biashara na zinaangaza mazingira mazuri na ya uhakika juu ya utajiri wa bara hili,”alisema Bi Mapunda.

Bw. Nick Blazquez, Raiswa Diageo Afrika, naye alitoa vielelezo kuhusu tuzo hizi na alikuwa na haya ya kusema: “Ni dhahiri kabisa sasa kwamba hamasa ya biashara Afrika imepanuka na dunia nzima sasa imeridhika na kiwango cha ukuaji wa uchumi barani Afrika.

Kama kampuni inayoendesha shughuli za kibiashara Afrika, tunaelewa umuhimu wa kuongezeka kwa taaluma ya uandishi wa habari za kiabishara na jinsi inavyounda mazingira mazuri na kuvutia kwa uwekezaji wa muda mrefu,” aliongeza.

“Nikiangalia miaka ya nyuma n amaendeleo ya tuzohizi, nimetambua uamsho wa hali ya juu na viwango vilivyomo katika uandishi wa habari za kibiashara na kuongezeka kwa juhudi za vyo mbo ya habari ndani na njeya Afrika ili kuhamasisha biashara na ujasiria mali barani humu.

Ninajivuniakwamba Diageo inatambua mafanikio haya na tunategemea kuona mchango wa hali ya juu kwa siku za usoni.”

Wakati tuzo hizi za waandishi wa habari za biashara Afrika kutoka Diageo zinakaribia kutimiza miaka kumi tangu kuanzishwa kwake, Diageo inaendelea kufikiria jinsi watakavyobadilisha uhalisia, matokeo na namna ya kuwafikia zaidi walengwa wa tuzo hizi.

Diageo inategemea kuboresha zaidi utoaji wa tuzo hizi kupitia mafanikio ya mwaka uliopita, kukaribisha usajili kutoka vyombo vyote vya habari na kutoka bara zima la Afrika na nje yaAfrika.

Mwaka huu, kundi la mfumo mpya wa utoaji wa habari limeondolewa na kuwa kundi linalojitegemea ili kuonyesha upana wa vyombo vinavyotumia mfumo huu wa utoaji habari.

Waandishi wa habari wanahamasishwa kutuma maombi yao. Habari ziwe zimetolewa kupitia mfumo wa vyombo vyote vya habari, ikiwa ni pamoja na gazetimtandazo (blogs) na habari zilizochapishwa kupitia tovuti mbalimbali pia wanaruhusiwa katika makundi yote, yaani 'categories'.

Sherehe yaTuzo hizi zitafanyika mjini London, Uingereza tarehe 28 mwezi Juni.Tarehe ya mwisho wa kupokelewa kwa maombi haya ni siku ya Ijumaa tarehe 23 mwezi Machi mwaka huu. Maombi yote yatumwe kupitia tovuti yetu: www.diageoafricabusinessreportingawards.com.

Hakuna kiingilio.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.