ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 13, 2012

NILIICHELEWESHA HII: NAPE AJIUNGA TWANGA PEPETA?

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye hivi karibuni alipata fursa ya kipekee kujiunga na Bendi ya Twanga Pepeta "Kisima Cha Buruduni" na kufanya nao mazoezi ndani ya ofisi za Aset.
Anamudu vilivyo gitaa la Solo

Hapa akionyesha mautundu katika Tumba, pembeni yake ni Victor Nkambi na Msafiri Diouf

Asha Baraka akimfurahia Nape wakati akifanya vitu vyake

Akipapasa Kinanda

Kija akimwangalia kwa makini Nape akipiga gitaa la Bass!

Nape Nnauye akipiga Drums huku Msafiri Diouf akiimba.

Baada ya kufanya makamuzi ya nguvu ilidhihirika wazi kwamba ukiachilia mbali siasa Nape ni msanii mkali wa kuimba, na kupiga vyombo mbalimbali vya muziki.

Aidha Mkurugenzi wa Aset Asha Baraka alifurahishwa na kumshukuru sana Nape kuja kuwatembelea na kuwapa sapoti, vilevile alimuahidi kuwa nafasi yake itakua wazi kwenye bendi mara tu atakapo amua kuachia ngazi kutoka katika jukwaa la siasa na kuamua kujiunga katika tasnia ya muziki.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.